Munch wa annabelletz47
JF-Expert Member
- Aug 13, 2019
- 1,885
- 3,227
Kabsa bint alikupendaInasikitisha sana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kabsa bint alikupendaInasikitisha sana
Nipo tight na kazi mkononi nataka nitulie nisome yoteee..Kisaikolojia mwanaume huwa hapendi sana isipokuwa Mwanamke ndiyo ambaye huwa anapenda sana.
Ikitokea mwanaume anampenda sana Mwanamke husababisha migogoro ya kimapenzi yenye kujirudia rudia, mwanaume huanza kulalamika, kususa,kununa, kutishia kujiua, kutishia waachane,kulia,kupiga magoti lakini muda huo mwanamke anakuwa hana hisia zozote kwa mwanaume huyo.
Mwanaume mwenye hisia kali sana ambaye huwa anaweza kulia, kupiga magoti, kutishia kujiua,kutuma sms mfululizo,kupiga simu mfululizo,kutumia fedha nyingi sana ili kuzuia mahusiano kuvunjika huwa ni DHAIFU SANA kwa sababu anakuwa hajui namna ya kusimama kama mwanaume Rijali ndani ya nyumba.
Mwanaume hatakiwi kupenda sana badala yake anatakiwa kumjali, kumhudumia,kumlinda, kumtetea mwenza wake dhidi ya maneno ya mama mkwe pamoja na maneno ya mawili.
Mwanaume kupenda sana ni UDHAIFU badala yake anatakiwa kuwa muadilifu tu.Mwanaume mwenye hisia kali sana za mapenzi huwa hawezi kufikiria kwa usahihi hasa kutoa hukumu baina ya makosa ya mwenza wake pamoja na migogoro ya kifamilia.
Haijalishi mabadiliko ya sayansi na teknolojia yatatokea kwa kiwango gani lakini uhalisia wa maisha ni kwamba mwanaume yeyote ambaye huwa anapenda sana huwa anateseka ukilinganisha na wanaume ambao huwa wanapenda kiasi kidogo sana.
Kisaikolojia mwanamke pale ambapo anajua anapendwa sana kuliko mtu yeyote huanza kuonyesha dharau, majivuno, kiburi, jeuri na ujuaji kwa sababu anakuwa anajua hata akifanya makosa makubwa sana anaweza kugeuza kibao kwa mwanaume kisha mwanaume ataomba msamaha,tabia hii ipo hata kwa watoto wadogo wenye kudekezwa sana .
Vilevile kwa wanaume ambao hawajielewi wakiona wanapendwa sana wanakuwa wanyanyasaji.
Mwanaume haitaji kupendwa anahitaji HESHIMA tu,kisha mwanaume anatakiwa kuwa muadilifu tu.
Kisaikolojia kuhusu kupenda sana au kupenda kidogo ni kwamba
Mtu ambaye huwa anapenda kidogo sana huwa na nguvu ya kutawala mahusiano kwa sababu hana cha kupoteza lakini yule ambaye anapenda sana huwa mwenye hofu ya kupoteza.
Mtu ambaye anapenda sana hujitoa mhanga kuokoa mahusiano lakini yule ambaye hapendi sana huwa hana muda wa kujali mahusiano.
Kwa asili mwanaume anakuwa na majukumu ya kuhakikisha anamjali Mwanamke,anamlinda, kumhudumia, kumuongoza njia iliyonyooka.
Mwanamke hana uwezo wa kumuongoza mwanaume katika mahusiano kwa sababu asili ya Mwanamke ni kutii mamlaka ya mwanaume na endapo Mwanamke akiona mwanaume anamnyenyekea sana huanza kumdharau,kumjibu vibaya, kumdhalilisha, kumfokea, kumtukana, kumkashifu, kumkaripia, kumgombeza, kumsaliti mwanaume kisha anageuza kibao kwa mwanaume.
Mwanaume hana uwezo wa kumpenda sana Mwanamke na kumuongoza kwa wakati mmoja.Badala yake mwanaume akipenda Mwanamke kupitiliza husababisha anakuwa mvumilivu sana wa fumanizi, matusi, kugombezwa, kukaripiwa, kutolewa dosari za muonekano, kunyimwa unyumba n.k
Utagundua kwamba wanaume wenye kuvutia kwenye jamii huwa wanapenda kidogo sana kisha kazi ya kupenda sana inakuwa ya Mwanamke siyo mwanaume.
Uwezekano wa kuachana huongezeka kama mwanaume anampenda sana Mwanamke kuliko Mwanamke anavyompenda mwanaume.
Mwanaume anatakiwa kuongozwa na akili siyo hisia za mapenzi..
Mwanamke akipenda anapenda kweli kwa hisia lakini kwa mwanaume ni tofauti.
Mwanamke akipenda hajali kipato, historia,tabia ya mwanaume,hajali maneno ya watu wengine.
Wanawake ambao huonekana wenye kiburi, majivuno, jeuri na dharau huwa wanaijua kanuni hii kwamba mtu ambaye huwa anapenda sana katika mahusiano huwa ndiyo ambaye anateseka sana,huwa anavumilia chochote ilimradi aepuke mahusiano kuvunjika.
Mwanamke hawezi kumlinda mwanaume isipokuwa mwanaume ndiyo anamlinda mwanamke dhidi ya maneno ya mama mkwe pamoja na mawifi,ikitokea mwanaume anampenda sana Mwanamke huwa anashindwa kumuonya pale ambapo amefanya makosa kwa kuhofia mahusiano kuvunjika.
Mwanamke anaweza kukaa kimya,kutenda wema , kumjali mwanaume,kujitoa mhanga kwa mwanaume kama njia ya kuonyesha kwamba yeye ni Wife material lakini kwa mwanaume hawezi kutumia njia hizo kutaka upendo wa Mwanamke.
Mwanaume anahitaji kuheshimiwa tu haitaji kupendwa. Mwanaume ambaye anataka kupendwa huparamia wanawake wenye tabia za ubabe, udikteta, udhalilishaji, dharau, majivuno, kiburi na jeuri kwa sababu siyo hulka ya Mwanamke kuona ananyenyekewa bali Mwanamke huwa anajikuta anakuwa mnyenyekevu mbele ya mwanaume ili apate kupendwa,apate kulindwa,apate utetezi na msaada.
Kwa mwanaume Rijali mwenye malengo ya kutaka kupata Mwanamke mwenye tabia njema kama upole, huruma, kujali, kunyenyekea, kusamehe makosa, uvumilivu n.k unatakiwa kuzingatia kanuni hii Mwanaume anapenda kidogo kisha Mwanamke anapenda sana endapo ukienda kinyume na kanuni hii utaparamia Mwanamke ambaye hataki kuzaa,hataki kujenga familia,hataki kudumu na MWANAUME kwa sababu bad boy wanaijua kanuni hii kwamba majukumu ya mwanaume siyo kumpenda Mwanamke bali kumlinda, kumhudumia, kumjali, kumheshimu, kumtetea dhidi ya maneno makali sana ya mama mkwe pamoja na mawifi zake japokuwa eneo la uadilifu wanaume ambao ni Bad boys huwa hawana muda kabisa hapo ndipo utasikia wanawake ambao ni Wife material wanalia, kuteseka lakini hawawezi kuondoka.
Mwanamke haondoki kwa mwanaume kirahisi kama amefanya uwekezaji mkubwa lakini kama hajafanya uwekezaji mkubwa anaondoka kwa kumtukana , kumkashifu, kumkaripia, kumgombeza, kumsaliti,kumjibu vibaya,kuiba pesa kisha anatokomea kusikojulikana lakini alipata ujauzito na kutekelezwa anarudi kuomba msamaha anajua kwa sababu anapendwa sana msamaha atapewa tu.
Haiwezekani kwa Mwanamke mwenye tabia ya ubabe, ukali kupitiliza, kiburi, majivuno jeuri na dharau kurudi kuomba msamaha akae na mwanaume mbabe, mgomvi mgomvi,jeuri, mwenye kiburi na majivuno siku zote utaona anataka kurudi kwa mwanaume mpole kupitiliza, mvumilivu sana, mnyenyekevu kupitiliza, mwenye kusamehe makosa haraka kwa sababu anajua atakuwa salama tu haijalishi atafanya makosa ,atafanya vurugu, atamdhalilisha mwanaume mara ngapi bado anakuwa na uhakika wa kusamehewa.
Usidanganyike kwamba mwanaume na Mwanamke ni sawa Haiwezekani.
Mwanamke akifika miaka 35 bila ndoa,bila mtoto,bila mwanaume wa kueleweka lazima utaona amechanganyikiwa lakini kwa mwanaume ni tofauti kabisa.
Mwanaume anaweza kufikisha miaka 45 kisha anaona mtoto wa 2000 lakini kwa Mwanamke ni vigumu sana kuolewa na mwanaume mwenye umri mdogo sana kwa sababu ataonekana ni mshangazi.
Hivyo fahamu kwamba mwanaume hatakiwi kupenda bali anatakiwa kuwa muadilifu tu.
Mwanaume anaweza kuishi na Mwanamke hata kama hampendi ilimradi tu amfanyie uadilifu lakini kwa Mwanamke ni ngumu sana kwa sababu mwanamke anaongozwa na hisia.
Mwanaume anaweza kuwa na wanawake hata wanne kwa wakati mmoja kisha kila mmoja akapata haki yake ikiwa mwanaume ni muadilifu lakini kwa maumbile ya Mwanamke haiwezekani.
Mwanamke akiwa na mwanaume zaidi ya mmoja huanza kuonyesha dharau, majivuno, kiburi, jeuri,ataibuka na ugomvi wa mara kwa mara bila sababu,anaweza kutoroka kwenda nyumbani kwao mara kwa mara kusingizia kesi za uongo,atafanya manyanyaso kisha anageuza kibao kwa mwanaume lakini mwanaume kwa maumbile yake kama anajielewa kiakili anaweza kuishi na wanawake zaidi ya mmoja bila kunyanyasa yeyote japokuwa zipo imani za dini haziruhusu mwanaume kuwa na Mwanamke zaidi ya mmoja lakini haiondoi uhalisia kwamba mwanaume haridhiki mfano Baltasari Ebang Engonga amethibitisha hilo kwa kulala na wanawake 400+.
Hivyo basi Mwanaume simamia uadilifu,tenda haki, heshima mwenza wako,hudumia mwenza wako kulingana na uwezo wako lakini jukumu la kupenda muachie Mwanamke ,kupenda sio jukumu la mwanaume.
Haiwezekani kwa mwanaume kupenda sana kisha awe muadilifu kwa pamoja lazima atafanya upendeleo.
Wakolosai 3:18 Enyi wake, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana. Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao. mujibu wa Kitabu kitakatifu cha Biblia jukumu la kupenda ni la mwanaume, mwanamke kazi yake ni kumtii mume wake.Naheshimu, nailinda na kutetea kupenda ni jukumu la Mwanamke
Hii kitu nilifanyaga hii nilimpiga chini wakati ambao hakutarajia mbona alijuta?Unampa kibuti wakati asiotarajia
Hii kitu nilifanyaga hii nilimpiga chini wakati ambao hakutarajia mbona alijuta?Unampa kibuti wakati asiotarajia
Utasikia mbona hivoo wakati nilikufanyia kila ninaloliweza jamanii?, sijuii nnHii kitu nilifanyaga hii nilimpiga chini wakati ambao hakutarajia mbona alijuta?
Kuna kupenda na kuna kuvutiwa tofautisha hilo mzee. Unapompenda sana mwanamke unakuwa mdhaifu mbele yake. Mwanamke mwenye mvuto tu anatosha kukufanya usikie burudani kumgegeda hata kama humpendi.Kama hupendi mwanamke basi hu enjoy mapenzi.
Hakuna kitu kitamu kama kugegeda mwanamke unayempenda sana aisee.
Wakolosai wangejua hii mbegu ya nyanda za juu kusini ilivyo na drama wasingehata shauri juu ya kuwa mpole.Wakolosai 3:18 Enyi wake, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana. Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao. mujibu wa Kitabu kitakatifu cha Biblia jukumu la kupenda ni la mwanaume, mwanamke kazi yake ni kumtii mume wake.
haha sasa mwanamke akiwa mtiifu kwako ukali utatoka wapi au mimi ndio sijui nini maana mtiifu.Wakolosai wangejua hii mbegu ya nyanda za juu kusini ilivyo na drama wasingehata shauri juu ya kuwa mpole.
Hahahah mwanamke mbishi lazma udili nae kwa ukali😄haha sasa mwanamke akiwa mtiifu kwako ukali utatau mimi ndio sijui nini maana mtiifu.
ila sisi wanawake wakati mwingine huwa hatujui tunataka nini. mwanaume aiwa mpole sana hatupendi. binafsi kuna wakati nataka nimjaribu kidogo mwanaume akikufokea kidogo utajisikia raha. yaani kuna muda mtu anataka ufokewe kidogo, kuna muda unataka ubembelezwe yaani hatueleweki. 😀 😀😀Hahahah mwanamke mbishi lazma udili nae kwa ukali😄
Dah na alininyoosha kweli ila alijutia na akataka kurudi ila wakati huo nlkuwa nshafunga dirisha la usajili 😂Sisterhood is proud of her
Alijua kukunyoosha 😀
Mwanamke ni kwenda nae kitaliban tuu. Lazima ashike adabuMwanamke hana uwezo wa kumuongoza mwanaume katika mahusiano kwa sababu asili ya Mwanamke ni kutii mamlaka ya mwanaume na endapo Mwanamke akiona mwanaume anamnyenyekea sana huanza kumdharau,kumjibu vibaya, kumdhalilisha, kumfokea, kumtukana, kumkashifu, kumkaripia, kumgombeza, kumsaliti mwanaume kisha anageuza kibao kwa mwanaume.
Hamna la maana zaidi ya ujinga ujinga tu😄ila sisi wanawake wakati mwingine huwa hatujui tunataka nini. mwanaume aiwa mpole sana hatupendi. binafsi kuna wakati nataka nimjaribu kidogo mwanaume akikufokea kidogo utajisikia raha. yaani kuna muda mtu anataka ufokewe kidogo, kuna muda unataka ubembelezwe yaani hatueleweki. 😀 😀😀
Mkuu nadhani Bado hujajuwa tofauti ya make love na sex.Kuna kupenda na kuna kuvutiwa tofautisha hilo mzee. Unapompenda sana mwanamke unakuwa mdhaifu mbele yake. Mwanamke mwenye mvuto tu anatosha kukufanya usikie burudani kumgegeda hata kama humpendi.
Ndio maana wanaume tunanunua malaya na kutongoza ma slay queen ili tufurahie sex ila haimaanishi tunawapenda.
saUtasikia mbona hivoo wakati nilikufanyia kila ninaloliweza jamanii?, sijuii nn
simu haziishi afu nakuwa napokea siongei chochote imeishaaa hiyoo