Mwanaume huna msaada,ishi kwa imani

Mwanaume huna msaada,ishi kwa imani

Jack Daniel

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2021
Posts
2,912
Reaction score
12,904
Hizi ni maada zimejadiliwa sana , ni kwamba narudia tu ili kuzidi kuweka mambo barazani ili kuwakumbusha wanaume wenzangu kuwa wanaume tumebeba majina na maana halisi ya maisha,hata katika visa kibao tunavyosoma ni kwamba mwanaume ndiye aliyebeba maana nzima ya kitu kinaitwa Dunia (ulimwengu)

Abeli (Habili) alikumbana na wivu toka kwa nduguye na kupelekea yeye kufa.

Ibrahim alikumbana na jaribu tena kutoka kwa Mungu mwenyewe,(wewe unayesoma hapa ungeweza)

Siyo hayo tu,Nuhu alilazimika kujenga Safina huku wengine wakimuangalia tu,lakini ndiyo majukumu halisi ya mwanaume bila kuhitaji Tag ubavu (msaada)

Samson akiwa na nguvu alizopewa na Mungu,bado alikumbana na mitihani na mitego kibao hadi akanasa,ndiyo uanaume, angefanyaje sasa?

Ayubu naye alikutana nacho kutoka kuwa tajiri hadi masikini wa kutupwa hizi ni mambo za kiume

Yesu naye pamoja na unyenyekevu wote bado akikutana nacho,ikiwa ni sehemu ya mbilinge za kiume.

Mtume Muhammad S.A.W naye alikutana na mbilinge kiasi cha kukimbizana kutoka ,Side A to Side B yote hiyo ni mitihani ya kiume ili tu kutimiza makusudi na maazimio yetu

Si kwamba wanawake hawakukutana na mitihani lahasha ila ya wanaume ndiyo yenye namba kubwa.

Tuna hawa hapa kwetu

Azory Gwanda,
Ben Saanane,

Yule mwandishi aliyeuawa kule Iringa kwa kipigo.

Wapo wengi sana na wote ni wanaume.

Sikia mwanaume mwenzangu,

Usipokufa kazini,utafia baharini.

Usipofia kwenye harakati za maisha utafia kwenye daladala,

Usipokufa popote utakufa hata kitandani ili mradi tu utaitwa Marehemu.

Usiseme Mimi siwezi kufanya hiki kisa nitakufa,kama ni Cha halali au ni madai ya halali wewe Fanya ili mradi huvunji Sheria mwanakwetu.

Pumzika kwa Amani Mzee Mohamed Alli kibao

Mungu akupunguzie adhabu ya kaburi.
 
Back
Top Bottom