Mwanaume ni sababu zipi zinakufanya ushindwe kabsa kuwa sehemu ya maisha ya mtoto wako?

Mwanaume ni sababu zipi zinakufanya ushindwe kabsa kuwa sehemu ya maisha ya mtoto wako?

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Kama mwanaume, inakuwaje unakubali na kuamua kuwa watoto wako walelewe na mke wako pekee na si wewe pia kama baba katika familia?

Nadhani ni muhimu kuuliza, kwa nini mwanaume angeweza kuchukua maamuzi ya kumwacha mke wake peke yake kubeba jukumu la malezi ya watoto kwenye ulimwengu huu?
images (97).jpeg


Katika jamii nyingi, familia ndo msingi mkuu wa jamii zote duniani, kupitia familia ndo tunapopata viongozi, kupitia familia ndo tunapata walimu, madaktari na wahandisi.

Na imekuwa kawaida kuchukulia familia kama muundo wa pamoja baina ya baba na mama, ambapo wawili hao wanasaidiana katika kulea na kuleta watoto duniani.

Ni wazi kwamba jukumu la mama ni muhimu sana, lakini je, jukumu la baba linapaswa kupuuzwa kiasi hiki? Kuna watu ambao wanaamini kuwa baba wanapaswa kuwa na jukumu kubwa zaidi katika malezi ya watoto, si tu kwa kutoa fedha na usaidizi mwingine, bali pia kwa kuwa na ushawishi katika kukuza tabia na maadili ya watoto wao haswa mchango wa mawazo.
images (98).jpeg


Hii inaweza kuwa na maana tofauti kwa kila mtu, lakini ni nini kinachofanya mwanaume kuwa na mtazamo wa kumwacha mke wake pekee katika jukumu hili? Je, kuna changamoto maalum zinazowafanya baadhi ya wanaume kujiona kuwa si sehemu ya malezi ya watoto wao?

Je, ni mambo ya kijamii au tamaduni ambayo yanawazuia wanaume wengi kuchukua jukumu la malezi kwa namna inayofaa?

Mara kadhaa tumepata vijana wengi walioharibika kimaisha ukiwauliza kuhusu wazazi wa kiume, wataishi kusonya na kudai baba hakuwahi kuwa sehemu ya maisha. Kuna tabia walizo nazo vijana wengi mtaani zinatokana na kutokuwepo kwa baba ndani ya nyumba.
images (99).jpeg


Kuna tabia ndani ya jamii zinaibuka kutoka kwa watu waliokosa father figure, na mbaya ni kuwa mwanaume unaweza kumsomesha mtoto wako na kumpa matunzo wakati akiwa kwa mama yake ila mchango wako wa kumkuza kimaadili ni mkubwa sana. Mama ana mchango wake tofauti kabsa na Baba kwenye makuzi ya mtoto.

Kwa mwanaume ni sababu zipi zinakufanya ushindwe kabsa kuwa sehemu ya maisha ya mtoto wako? Na je, kuna umuhimu gani kwa baba kuwa sehemu ya malezi ya mtoto katika familia? Je ni maadili na tabia za mwanamke? Je ni tabia yako binafsi?
 
Kama mwanaume, inakuwaje unakubali na kuamua kuwa watoto wako walelewe na mke wako pekee na si wewe pia kama baba katika familia?

HII NI SPACE YA WANAUME PEKEE!

Nadhani ni muhimu kuuliza, kwa nini mwanaume angeweza kuchukua maamuzi ya kumwacha mke wake peke yake kubeba jukumu la malezi ya watoto kwenye ulimwengu huu?
View attachment 3228052

Katika jamii nyingi, familia ndo msingi mkuu wa jamii zote duniani, kupitia familia ndo tunapopata viongozi, kupitia familia ndo tunapata walimu, madaktari na wahandisi.
Na imekuwa kawaida kuchukulia familia kama muundo wa pamoja baina ya baba na mama, ambapo wawili hao wanasaidiana katika kulea na kuleta watoto duniani.

Ni wazi kwamba jukumu la mama ni muhimu sana, lakini je, jukumu la baba linapaswa kupuuzwa kiasi hiki? Kuna watu ambao wanaamini kuwa baba wanapaswa kuwa na jukumu kubwa zaidi katika malezi ya watoto, si tu kwa kutoa fedha na usaidizi mwingine, bali pia kwa kuwa na ushawishi katika kukuza tabia na maadili ya watoto wao haswa mchango wa mawazo.
View attachment 3228053

Hii inaweza kuwa na maana tofauti kwa kila mtu, lakini ni nini kinachofanya mwanaume kuwa na mtazamo wa kumwacha mke wake pekee katika jukumu hili? Je, kuna changamoto maalum zinazowafanya baadhi ya wanaume kujiona kuwa si sehemu ya malezi ya watoto wao? Je, ni mambo ya kijamii au tamaduni ambayo yanawazuia wanaume wengi kuchukua jukumu la malezi kwa namna inayofaa?

Mara kadhaa tumepata vijana wengi walioharibika kimaisha ukiwauliza kuhusu wazazi wa kiume, wataishi kusonya na kudai baba hakuwahi kuwa sehemu ya maisha. Kuna tabia walizo nazo vijana wengi mtaani zinatokana na kutokuwepo kwa baba ndani ya nyumba.
View attachment 3228054

Kuna tabia ndani ya jamii zinaibuka kutoka kwa watu waliokosa father figure, na mbaya ni kuwa mwanaume unaweza kumsomesha mtoto wako na kumpa matunzo wakati akiwa kwa mama yake ila mchango wako wa kumkuza kimaadili ni mkubwa sana. Mama ana mchango wake tofauti kabsa na Baba kwenye makuzi ya mtoto.

Kwa mwanaume ni sababu zipi zinakufanya ushindwe kabsa kuwa sehemu ya maisha ya mtoto wako? Na je, kuna umuhimu gani kwa baba kuwa sehemu ya malezi ya mtoto katika familia? Je ni maadili na tabia za mwanamke? Je ni tabia yako binafsi?
Kuna sababu ya Uchumi, nyingine wengine wanazaa nje ya ndoa hivyo ili kulinda ndoa zao wanatelekeza au kukana watoto wao na kingine ni hii issue ya 50/50 Kuna tabia ya baadhi ya wanawake kutafuta mwanaume wa kumzalisha tu na baada ya hapo wanakata contact wanaenda kulea watoto peke yao hii inatokana na wanawake now kuwa na financial independence hivyo wengine hawapendi kukaa na Mwanaume wa kumcontrol. Na mengine mengi ya dizaini hiyo
 
Kuna sababu ya Uchumi, nyingine wengine wanazaa nje ya ndoa hivyo ili kulinda ndoa zao wanatelekeza au kukana watoto wao na kingine ni hii issue ya 50/50 Kuna tabia ya baadhi ya wanawake kutafuta mwanaume wa kumzalisha tu na baada ya hapo wanakata contact wanaenda kulea watoto peke yao hii inatokana na wanawake now kuwa na financial independence hivyo wengine hawapendi kukaa na Mwanaume wa kumcontrol. Na mengine mengi ya dizaini hiyo
Safi sana Mkuu
 
shida ni tamaa ya kutaka kila kitobo, ndio inapoanzia, baadhi ya wanaume hawataki kuwajibika pale wanaposababisha mimba, wana kuna msemo wa kidwanzi "eti akikua atanitafuta" sawa atakutafuta kujua tu umekufa au uko hai lakini ile Chemistry ya baba na mtoto haipo, na pengine akakutafuta wakat tayari ameharibika itasaidia nini wakati ulikuwa na nafasi ya kumletea katika namna vile unapenda
 
Tatizo wanawake wanatumia mtoto kama kitega uchumi. Mtoto anaishi kwa Mama tu, anazuiwa kwenda kwa Baba hata wakati wa likizo. Hapo ni lazima Mwanaume alale mbele tu.
 
Tatizo wanawake wanatumia mtoto kama kitega uchumi. Mtoto anaishi kwa Mama tu, anazuiwa kwenda kwa Baba hata wakati wa likizo. Hapo ni lazima Mwanaume alale mbele tu.
mwanamke atamtumia mtoto kama kitega uchumi kama ushirikiano wako ni sifuri, lakini kama ushirikiano ni mkubwa wala, lakini kingine ambacho hakijulikani ni mwanamke kumtumia mtoto akuvute uwe kwake yaani kama umeoa mwanamke mwingine basi hapo atatumia nafasi hiyo kuhakikisha anakufanya unakuwa Bize kwa ajili ya mtoto kumbe ni yeye anataka attention kwako
 
Ni kukosa akili na hekima ya kiume tu. Una achaje bao lako linalelewa kiholela wewe upo?
 
mwanamke atamtumia mtoto kama kitega uchumi kama ushirikiano wako ni sifuri, lakini kama ushirikiano ni mkubwa wala, lakini kingine ambacho hakijulikani ni mwanamke kumtumia mtoto akuvute uwe kwake yaani kama umeoa mwanamke mwingine basi hapo atatumia nafasi hiyo kuhakikisha anakufanya unakuwa Bize kwa ajili ya mtoto kumbe ni yeye anataka attention kwako
Hilo ni kosa ndugu Mwandishi
 
Back
Top Bottom