Mwanaume unaemkataza mkeo kufanya kazi unafanya makosa makubwa

Mwanaume unaemkataza mkeo kufanya kazi unafanya makosa makubwa

Engager

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2011
Posts
1,522
Reaction score
3,255
Pengine wewe ni mwajiriwa ama umejiajiri. Unauwezo kifedha. Umemzuia mkeo kufanya kazi kwa sababu wewe unamtimizia haja zake zote kifedha. Unahudumia familia, na yeye as an individual unamhudumia. Pengine zaidi ya hata angefanya hiyo kazi. Kazi kwa maana ya shughuli yoyote inayoweza kumfanya yeye apate pesa yake. Iwe ya kuajiriwa ama kujiajiri.

Kunawengine wana biashara kubwa tu. Lakini hawawashirikishi wake zao. Kwamba mke anapaswa akae nyumbani alee watoto. Basi mke anakuwa ni wa kupokea tuu.

Nakushauri, hata kama unauwezo wa kuhudumia familia na mkeo kwa kila kitu, yaani kwamba mkeo hata akitaka leo ukajenge kwao huo uwezo unao na hutetereki, mwache tuu mama huyo nae aparangane.

Sio kwamba uache kumhudumia, endeleza huduma ila mwache aparangane, wakati mwingine kama unamuona ni mzito, msaidie awe mparanganaji japo kidogo, kwa maana hatuijui kesho.

Hivi kwamfano, wewe si ndo kichwa cha familia? Si unamhudumia mkeo, hutaki aparangane, yeye awe ni mpokeaji tuu. Vipi kama ikitokea umetangulia mbele za haki ukamwacha na hao wanao?! Do you know how helpless will she be?! Atawalea vipi hao machalii na wewe ulimzoesha kupokea tu? Ulisha wahi kufikiria ataanzia wapi?!

Sometimes hisia za mapenzi kwenye ndoa tuziweke kando. Tuache wake zetu waparangane hata kama tunauwezo wa kuwahudumia kwa kila kitu. Ni kwa manufaa ya kizazi chako.
Ni makosa makubwa kumzuia mke kufanya kazi.
 
Wanawake wengi hata wafanye kazi za kulipwa mamilioni ya pesa, lakini ndani ya nyumba wanaishi kwa kutegemea kila kitu kwa mwanaume.

Mshahara wake ni kwa ajili ya makeup, na kutunzia mashosti kwenye kitchen party... Mwanamke wa namna hiyo ni bora akae ndani alee watoto!
 
Wanawake wengi hata wafanye kazi za kulipwa mamilioni ya pesa, lakini ndani ya nyumba wanaishi kwa kutegemea kila kitu kwa mwanaume. Mshahara wake ni kwa ajili ya makeup, na kutunzia mashosti kwenye kitchen party... Mwanamke wa namna hiyo ni bora akae ndani alee watoto!
Kweli kabisa au labda mshahara wake uendeshwe na mume
 
Wanawake wengi hata wafanye kazi za kulipwa mamilioni ya pesa, lakini ndani ya nyumba wanaishi kwa kutegemea kila kitu kwa mwanaume. Mshahara wake ni kwa ajili ya makeup, na kutunzia mashosti kwenye kitchen party... Mwanamke wa namna hiyo ni bora akae ndani alee watoto!
Huyo siyo mwanamke bora bali ni takataka waste.
 
Wanawake wengi hata wafanye kazi za kulipwa mamilioni ya pesa, lakini ndani ya nyumba wanaishi kwa kutegemea kila kitu kwa mwanaume. Mshahara wake ni kwa ajili ya makeup, na kutunzia mashosti kwenye kitchen party... Mwanamke wa namna hiyo ni bora akae ndani alee watoto!
Muache afanye kazi, usiitolee macho pesa yake. Ukiashaanza kuitolea macho pesa ya mwanamke unakaribisha migogoro.
 
Muhimu kuweka mambo kisheria na mkeo ajue sheria...kama mirathi ...Nani msimamizi wa mirathi ...mwanasheria wa familia yupi?
Haki zako za kazin aanzie wapi etc
Hata akichukuwa hiyo mirathi, hata kama ni milioni 500 kama za mbunge. Kama hana mentality ya uparanganaji akilini mwake zitapotea kama upepo.
 
Sisemi mke kufanya kazi za kuongeza kipato ni mbaya,la hasha

ila nasema hivi,nikiwa na pesa (ile pesa kweli kweli) nitamfungulia

mke biashara ambayo ataingia baada ya kumaliza kazi za nyumbani

na huko kazini atakaa masaa machache tu,atarudi nyumbani Kulea na kuandaa mazingira

ya mimi "mume" nikirudi nyumbani nikute ile atmosphere ya nyumba iliyo na MAMA/mke

Kazi ya mwanamke kutoka nyumbani 12 asubuhi to 1 usiku,Kwangu ni NO

Kazi ya mwanamke kwenda kupambana (kama msemavyo) kurudi kwangu mbili usiku ni NO

Ki ufupi siafiki u busy wa kutafuta kipato kwa mke wangu,naruhusu tu afanye biashara (kwa muda huo mchache)

ili tu asiwe bored na pesa atayopata kwenye hiyo biashara ataamua mwenyewe aifanyie nini

Ushoga umezidi kutokana na mwanamke kuruhusiwa eti kupambana,Watoto wanajilea wenyewe.

Dunia inaharibika kwasababu ya mwanamke kupewa majukumu ya mwanaume

Mimi wanangu hawawezi haribikiwa na nitaanza na mama yao,Atoke nyumbani watoto wameshaenda shule

ARUDI nyumbani watoto hawajarudi shule,ili wakirudi wachafu awazabue,wakirudi na kasoro awanyoooshe

Kazi pekee ya mama ni FAMILIA,kAZI PEKEE ya BABA ni kuitunza familia...Maswala ya kifo yapo ila kila mtu

asimamie eneo lake,BABA kuitunza Familia, MAMA kulea Familia,Kwisha..U supa woman sio kwangu mimi.
 
Basi mruhusu mkeo afanye kazi kaka, kama Kuna mtu anamkataza mkewe we muache tu. Kila mtu ana misingi yake ya ndoa na kwa kuwa hawatakuja kukuomba msaada hata Hao waume zao wakifa basi we jiachie tu.

By the way kwani ni sheria au lazima atangulie baba kufa? Vipi kwa zile ndoa ambazo baba anamkataza mkewe kufanya kazi alafu anatangulia mama kufa?

Mkuu ishi leo ufurahie maisha acha kuishi kesho.
 
Pengine wewe ni mwajiriwa ama umejiajiri. Unauwezo kifedha. Umemzuia mkeo kufanya kazi kwa sababu wewe unamtimizia haja zake zote kifedha. Unahudumia familia, na yeye as an individual unamhudumia. Pengine zaidi ya hata angefanya hiyo kazi. Kazi kwa maana ya shughuli yoyote inayoweza kumfanya yeye apate pesa yake. Iwe ya kuajiriwa ama kujiajiri.

Kunawengine wana biashara kubwa tu. Lakini hawawashirikishi wake zao. Kwamba mke anapaswa akae nyumbani alee watoto. Basi mke anakuwa ni wa kupokea tuu.

Nakushauri, hata kama unauwezo wa kuhudumia familia na mkeo kwa kila kitu, yaani kwamba mkeo hata akitaka leo ukajenge kwao huo uwezo unao na hutetereki, mwache tuu mama huyo nae aparangane.

Sio kwamba uache kumhudumia, endeleza huduma ila mwache aparangane, wakati mwingine kama unamuona ni mzito, msaidie awe mparanganaji japo kidogo, kwa maana hatuijui kesho.

Hivi kwamfano, wewe si ndo kichwa cha familia? Si unamhudumia mkeo, hutaki aparangane, yeye awe ni mpokeaji tuu. Vipi kama ikitokea umetangulia mbele za haki ukamwacha na hao wanao?! Do you know how helpless will she be?! Atawalea vipi hao machalii na wewe ulimzoesha kupokea tu? Ulisha wahi kufikiria ataanzia wapi?!

Sometimes hisia za mapenzi kwenye ndoa tuziweke kando. Tuache wake zetu waparangane hata kama tunauwezo wa kuwahudumia kwa kila kitu. Ni kwa manufaa ya kizazi chako.
Ni makosa makubwa kumzuia mke kufanya kazi.
Naunga mkono hoja[emoji817]
 
Basi mruhusu mkeo afanye kazi kaka, kama Kuna mtu anamkataza mkewe we muache tu. Kila mtu ana misingi yake ya ndoa na kwa kuwa hawatakuja kukuomba msaada hata Hao waume zao wakifa basi we jiachie tu.

By the way kwani ni sheria au lazima atangulie baba kufa? Vipi kwa zile ndoa ambazo baba anamkataza mkewe kufanya kazi alafu anatangulia mama kufa?

Mkuu ishi leo ufurahie maisha acha kuishi kesho.
🤣🤣🤣🤣 haya bana.
 
Back
Top Bottom