Mwanausalama Tanzania aaibika kutumia nguvu na mwanausalama wa Obama kumlinda mwandishi

walijua kabisa kwamba policcm intelijensia yao ni sufuri, sana sana wangewaharibia , wakawapiga chini.
Hii mi policcm ovyoo kabisa,yaani pamoja na kupelekwa Marekani kozi kwa makundi enzi ya IGP aliyepita akili zao zinawaza-ulinzi shirikishi,utii bila shuruti,kubambikia watu kesi na jioni kulewa pombe,utadhani sala ya kila siku,we mwite polisi yeyote afandee mwone atakavyokwitikia' UTII BILA SHURUTI EEEH'.Utadhani alikuwa usingizini.
 
Jana nilikuwa pale IFM wakaja FFU mbona walizuiwa kuingia pale makumbusho hata baada ya kuuingia bado walikaguliwa na MBWA wa wanausalama wa Marekani
 

Huyu Mwanausalama wa US Angemsikia Pinda na kauli zake angezimia kabisa. Nchi hii ingawa inasingiziwa kuwa nchi ya amani, Ina manyanyaso mengi sana kwa Rai na Waandishi wa Habari.
 
Ndivyo mnavyofundishwa katika utendaji wenu? Haya ni maneno mazito sana kuhusu maafisa wa usalama wetu.

Yap, ndivyo wanavyofundishwa, kutumia maguvu bila akili.

Rejea kauli ya waziri mkubwa wa Tanzania, "ukiambiwa usifanye hiki na wewe husikii, unajiona wewe ndio wewe, wewe ndiye jeuri, utapigwa tu, na mimi ninasema wawapige tu,maana hakuna namna nyingine, tumechoka sasa''.

Mkuu, fikiria waziri mkuu anasema hakuna namna nyingine inayoweza kuwa mbadala badala ya kupiga tu.

Sio kosa la huyo mwanausalama, ndivyo serikali inavyowafundisha kufanya.
 

Hayo ni yote nayaelewa hoja ni matumizi ya nguvu je unakubali hata hapa US yapo? Matokeo ya baadaye nini kinafanyika tutayajadili; mada kuu ni matumizi ya nguvu sasa kama unakiri yapo waleleze makamanda kwasababu wengi wao wamejenga hoja kana kwamba hivyo vitu havifanyiki hapa USA!
 
Maadam ni wa gazeti la uhuru, angeuwawa tu, make huwa wanawasifia polisi wanapovunja maandamano ya chadema.
 
Matumizi ya nguvu yapo lakini yana tiba yake. Ingekuwa hapa Marekani leo Kamhunda asingepandishwa cheo. Angepelekwa mahakamani na kama si kufungwa jela angelipa fidia ya mamilioni kwa familia ya Mwangosi.
 
Sioni tofauti kati ya hao waandishi na hao mapoliccm kwasababu wote hujifanya wao simiongoni mwetu watanzania tunaonyanyasika kila kukicha WAACHENI WAFU WAZIKANE WENYEWE
 
Matumizi ya nguvu yapo lakini yana tiba yake. Ingekuwa hapa Marekani leo Kamhunda asingepandishwa cheo. Angepelekwa mahakamani na kama si kufungwa jela angelipa fidia ya mamilioni kwa familia ya Mwangosi.

Unachanganya mada! matumizi ya nguvu yapo pande zote sasa waeleze makamanda kwamba hali hiyo hata huku ipo tena huku imechanganywa na ubaguzi sasa waelemishe makamanda halafu turudi kwenye adhabu na hatima za wahusika wanaotumia nguvu!
 
Hivi huwa wanafundishwa wapi?

.......Kwenye Msitu wa Mabwepande chini ya Mtaalamu wa mambo ya usalama kutoka CCM, Bwana Nchemba. Huwa wanapewa mafunzo ya kutumia maguvu kukabiliana na mambo yasiyohitaji nguvu, jinsi ya kung'oa meno na kucha bila ganzi, jinsi ya kutoboa macho bila ya kuziathiri kope, kumwagia watu tindikali na kutumia poronium kuwadhuru viongozi wao wenyewe.

BIG UP!! kwa Lameck Madelu Nchemba matunda ya mafunzo yako yameonekana leo kwa huyo mwanishi wa habari
 
​angejua wanafundishwa na kung`oa meno sijui ingekuaje
 
mi kila siku nasema tanzania police no manners😛ainkiller:😛ainkiller:
 
TISS ni nzuri ila tatizo inatumia WINDOWS 98 wakati dunia ya leo iko windows 8... madhara yake ndo hayo sasa..
 
Huyu Mwanausalama wa US Angemsikia Pinda na kauli zake angezimia kabisa. Nchi hii ingawa inasingiziwa kuwa nchi ya amani, Ina manyanyaso mengi sana kwa Rai na Waandishi wa Habari.

Hiyo signature yako kiboko... Dhaifu alijiumbua "live". Kama lugha si yako si uiache? Wakalimani mbona wapo? Rais wa China kaongea Kichina. Wewe wamjibu Kiingereza. Yaani wathamini Kizungu kuliko Kiswazi? Duuuuuu!
 
Aibu!, Aibu!, another thing an american was shocked was to see tht moron push and use such force on a WOMAN!

Arizona state troopers WA kiume wameshtakiwa kumkagua maeneo nyeti WOMAN wakitafuta bangi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…