Mwandishi aliyeandika tuhuma za RC Simiyu adaiwa kukamatwa na Polisi
Hakumsingizia, tafuta hukumu uisome. Binti alikuwa kidato Cha pili na alikuwa na miaka 16, alikuwa na boyfriend bodaboda, walikubaliana aondoke kwao Ili amuoe..wakakamatwa na polisi. Kwakuwa alikuwa underage bodaboda alifunguliwa kesi ya ubakaji. Katika ushahid mahakamani huyu binti hakusema kwamba alibakwa, alisema walifanya mapenzi na walikubaliana atoroke kwao Ili waende Moro amuoe. Yule jamaa alihukumiwa miaka 30 jela kwa kubaka lkn badae alikata rufaa akapunguziwa kifungo Hadi miaka Saba.
alimsingizia period, hutaki kajinyonge.
 
hako kabinti ni issue!, kalimfunga dereva boda boda akapigwa mvua 30 kwa kesi ya kubaka wakati in reality ni yeye mwenyewe alitoroka kwao akahamia kwa dereva boda!. Ushahidi wa kubakwa ni uchunguzi wa hospital na kukutwa hana seal!hivyo boda akafungwa miaka 30!.

P
Ndugu Mayalla, kama hutojali wewe kama mkongwe wa habari za uchunguzi unaweza kutuwekea hapa kisa hicho kikiwa kamili ili jamii ipate picha ya kilichotokea na wanaume wapate funzo. Nafahamu kuwa pamoja na hako kabinti kuwa na tabia za ajabu ajabu hazifuti kosa lililofanywa na RC lakini angalau jamii itapata picha ya mabinti wanaotetewa kwamba wanafanyiwa ukatili na kudhalilishwa
 
ni kwamba RC anataka kusafishwa au nini? si na maza kamfukuza au na maza naye amekosea atatakiwa akamatwe kwa kumwondolea cheo?
 
Duh...!, hizi mambo zimeanza tena?!..., au Maza nae anaelekea kuwa like Maza like Faza?!.
Tusubirie taarifa ya Edwin Soko wa MPC, kuthibitisha hao waliomkamata ni polisi kweli... maana... Waandishi wa Habari na Kupotea/Vifo vya Kutatanisha, Toka Katabalo, Saanane, Gwanda, Mwangosi, Isango. Ni Ama Tuombe Mungu Atunusuru ama...
P
Wangemuita kuweza mhoji source ya story yake and sio kumkamata ingawa mwandishi hatakiwi kusema source ilikumlinda mtoa taarifa,changamoto iliopo kwenye technology zetu lazima wawe na kifaa they can’t hack kwakua uwezo huo haupo kwa sasa TZ,otherwise wala wasingemkamata wangehack tu simu yake and kupata kila kitu then ikigundulika nimhalifu ndio angekamątwa but they can’t
 
Nina hakika hata huyu RC alikuwa Black Mailed. Watu wanashangilia hayajawakuta.
Hii dunia ndiomaana tunaambiwa kiumbe chenye jinsia ya ke ishi nacho kwa akili sana hata kama mjusi. We fikiria mtu kama RC mwenyekiti wa ulinzi na usalama mkoa, anao hata uwezo wa kujitengenezea walinzi wake binafsi na watoa taarifa binafsi anakuwa "blackmailled" na binti mdogo wa miaka 21 first year?!

Kama anapenda dogo dogo anashindwa nini kuajili watoa taarifa binafsi wa engo hizo yaani kabla hajaokota hivyo vidadazi ajikusanyie taarifa za kutosha kwanza kujihakikishia usalama wake kwasababu ukishakuwa kiongozi lazima ujue namna ya kulinda baadhi ya mambo yako ya hovyo yasije kwenye jamii (naamini wanaotembea na vitoto sio peke yake)

Kupata taarifa za binti kiruka njia sio kazi ngumu kama wamekutana toka mwezi wa pili huko kupitia watu wake angeshajua mengi kukahusu hako kabinti kama yanayosemwa ni kweli na pengine angetafuta njia nzuri ya kukadhibiti kama sio kukapa onyo kabisa

Kama hizo skendo za kutoroka kwao na kuhamia kwa boda boda ni za kweli, na hizi za kulawitiwa nazo zikawa za kweli, huyu binti hajaanza leo kushiriki kinyume na maumbile yake ya asili RC kaangushiwa jumba bovu
 
Back
Top Bottom