TANZIA Mwandishi wa habari wa TBC Joachim Kapembe amefariki dunia

Kwenda gym kumbuka upo level ile ile ila kupanda mlima kila siku elevation ina change na kadri unavyopanda kumbuka oxygen inapungua
 
Kuna Siri gani Kati ya kishuka mlima Kilimanjaro na kifo?. Kuna rafiki yangu naye alifariki wakati wanashuka mlima Kilimanjaro.
Msukumo wa damu ukiwa kileleni ni mkubwa kuliko unapokuwa huku chini, sasa kama hauko vizuri unapata mushkeli unapobadili mazingira.
 
Hapo kwenye Km 40,000, rekebisha, ni chini ya Km 400
 
Kilimanjaro the roof of afrika ni mlima niliopanda zaidi ya miaka Saba nilianza kupanda nikiwa darasa la sita nimebahatika kupanda njia zote katika njia hizo marangu rout au cokacola rout ni njia pekee yenye nyumba za kulala maji ya bomba na umeme wa Sola na ndio njia kongwe na ni njia ya gharama kuliko zote sema pia ndio njia hatari Kwa vifo kuliko zote hasa kutokana tabia ya Hali yake ya hewa kubadikabadika wakati wowote haswa kipande Cha kutoka horombo hut mpaka kibo hut hichi kipande unaweza kuamka uko fit na gafla ukaitwa marehemu hakina ujanja wa Jimu sijui mazoezi mlima ukikukataa hakuna namna hata kama ukiwa na madaktari bingwa utakufa tu nakumbuka Ile kipindi ya elnino mwaka 2000 nilishuhudia watu wawili wakikata roho na mzungu mmoja alikua daktari akijaribu kuwasaidia lakini ikashindikana mzungu akachanganyikiwa na yeye mwenyewe haelewi iacheni Kilimanjaro iitwe Kilimanjaro
 
Kuna Siri gani Kati ya kishuka mlima Kilimanjaro na kifo?. Kuna rafiki yangu naye alifariki wakati wanashuka mlima Kilimanjaro.
Kwa maeleo ya Gerson msigwa.

Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa amesema kifo cha Mwandishi wa Habari wa TBC Joachim Kapembe aliyefariki jana akiwa Mlimani Kilimanjaro kimetokana na ajali ya Baiskeli na sio madhara ya kupanda Mlima Kilimanjaro.

"Nimesikitishwa sana na kifo cha Rafiki yangu
Joachim Kapembe tuliyekuwa nae kwenye
safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro, Kapembe
amefariki kwa ajali ya baiskeli wakati akitoka
katika kambi ya Kibo kuelekea kambi ya
Horombo baada ya kupanda mlima hadi kufika
kileleni kwa mafanikio na ni mmoja wa Watu
ambao hawakupatwa na madhara ya kupanda
mlima (mountain sickness)" --- Msigwa.

"Baada ya kufanikiwa kufika kileleni
Kilimanjaro na kushuka, Watu wote tulifika
kambi ya Kibo ambako tulipaswa kuendelea
kwenda kambi Horombo, wachache waliamua
kutumia baiskeli badala ya kutembea kwa
miguu akiwemo Joachim Kapembe bahati
mbaya akiwa anateremka mteremko wa
kutoka Kibo ndipo akapata ajali iliyosababisha
apoteze maisha"


"Natoa pole kwa Familia, Mkurugenzi Mkuu,
Wafanyakazi wa TBC, Waandishi wa Habari
wenzangu, ndugu jamaa na marafiki wote,
Mwenyezi Mungu amweke mahali pema
peponi... Bwana alitoa, Bwana ametwaa, jina
lake lihimidiwe, Amina" @gersonmsigwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…