Mwandishi wa STAR TV ajuta kumfahamu Joseph Mbilinyi

Nimemsikiliza huo mjadala vizuri, Sugu amenyoosha maelezo vizuri, mpaka kuna muda Star tv wakakata hicho kipindi.
Kawaida yao hao. Niliwachukia tangu wakati ule wa dr. Slaa. Kukimbia chama
 
Mwaka 2020 siku cheche kabla ya uchaguzi vijana waliitwa na viongozi wa ccm pale kinondoni kwenda kupiga kura za ndiyo kwa magufuli na chama chake. Malipo yalikuwa 5000/= hawajapewa mpaka leo. ( ushahidi mdogo wangu alikuwepa kwenyezoezi Huskies, Kura zilizokamatwa kwenye mabegi kunduchi nk)
Vituoni; Vito vilifunguliwa saa 9 usiku badala ya sa 12 asubuhi. Wasimamizi wakisokomeza kura zilizopigwa kwenye masanduku, pia kulikuwepo na makada chama ambao walikuwa walipiga kila kituo na kuingia na kura zilizopigwa na kuziingiza kwenye masanduku . Hii imekuja baada ya kuhakikisha vituoni hakuna makala wa vyema vingine ( ushahidi waliokuwemo kwenye Vituo kama wasimamizi lakini wasiopendezewa na dhulma)
Wasimamizi : ma DED walihakikisha wasimamizi ni wale watumishi wenye mlengo wa ccm ama kwa.kujipendekeza au kutojitambua kwao hii ilifanyika ili kurahisisha niliyoyaandika hapo juu. Ushindi upo unawajua kwa majina mana unaishi nao na kufanya nao kazi.
Endelea kuishi binafsi kuamini kwamba ccm nilishindwa kihalali
 
Ficha ujinga woke wew, unafikiri walipo kata rufaa Mahakamani walikwenda bila fomu za matokeo ambayo ktk Uchafuzi uliopita walinyimwa kupewa mawakala na hata kubandika hawakubandika?
Mwenda kuzimu alifanikea kuwapumbaza sana wajinga
 
Alisema fomu walinyimwa mawakala wa upinzani,sasa mahakamani utathibitisha vipi.

Magufuli alibana hadi kajiibia mwenyewe
Poleni sana watanzania kwa aina ya Rais mliyekuwa naye
 
Wa
Wewe wanaangalia watu wa kuoji, Kuna vichwa lazima ujipange,chadema imepika watu sio mchezo,mwafaa ,alisema mwendazake
 
Mwandishi alimuuliza mbona kama wananchi hawakupiga makelele ya kupinga ushindi wa tulia ina maana wananchi hawakumchagua....Sugu akamwambia wananchi walipinga sana sema enzi za mwendazake ilikuwa hakuna uhuru wa habari na hakuna chombo chochote kingeweza kutoa hiyo taarifa na hata wewe(mwandishi) usingeniita hapa maana mngepigiwa simu kibao kwanini umenileta.
 
Hoja yako ni dhaifu sana.

Mbona hao akina Mbowe walikata rufaa walipohukumiwa kulipa fidia baada ya zile vurugu za Kinondoni. Je, hiyo rufaa walikata wakati wa utawala wa nani?
Huna taarifa tu lakini rufaa inakatwa hata kwenye mifumo ya Aina zote, mizuri na mibaya na usichokijua zaidi rufaa ni haki inayotoka ndani ya mtu kukutafuta na haitegemei eti mfumo uwe mzuri au mbaya. Akili ya mtu ikimwelekeza kuwa umeonewa hapa na ikimsukuma kuwaambia watesi wake kuwa wamemwonea huwezi kuzuia hilo. Ni ya kifilosofia zaidi hii.
 
Kama mnao ushahidi kwanini hamkwenda mahakamani kufungua kesi???
Hilo ndilo swali langu la msingi.
 
Ficha ujinga woke wew, unafikiri walipo kata rufaa Mahakamani walikwenda bila fomu za matokeo ambayo ktk Uchafuzi uliopita walinyimwa kupewa mawakala na hata kubandika hawakubandika?
Mwenda kuzimu alifanikea kuwapumbaza sana wajinga
Kunyimwa fomu ni ushahidi pia na unaweza ukatumika mahakamani. Na ndiyo maana nawauliza kwanini hamkufungua kesi mahakamani?

Tatizo lenu CHADEMA mmezoea kukaririshwa ujinga na viongozi wenu na ninyi mnakariri tu kama vitoto vya chekechea.

Mimi nakwambia hivi hao CHADEMA kama wangekuwa na ushahidi wa kuibiwa kura wasingeacha kufungua kesi Mahakamani kupinga matokeo ya Ubunge ambayo kisheria yanaruhusiwa kupingwa.
Jibu ni dogo, hawakwenda Mahakamani sababu hawakuwa na ushahidi wa madai yao.
Mtu kama Mbowe akose Ubunge kwa kudai kuibiwa halafu asiende Mahakamani? Seriously??

Mtu kama Zitto Kabwe aibiwe kura halafu asiende mahakamani??

Endeleeni kushikiwa akili na wanasiasa "wahuni" .
 
Sasa mbona mnajichanganya na hoja zenu dhaifu?
Kama haki ya rufaa inaweza kupatikana ndani ya mfumo huo huo dhaifu iweje basi haki zingine zisipatikane kama ushahidi upo??

Tusidanganye hata kidogo. Hao akina SUGU hawakuibiwa kura, walishindwa kihalali na ndiyo maana hawakuwa na ushahidi wa kwenda mahakamani kupinga matokeo ya Ubunge.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…