Mwanza: Daladala kugoma Februari 16, wanadai bajaji zinakwapua abiria wao na kuwamaliza

Mwanza: Daladala kugoma Februari 16, wanadai bajaji zinakwapua abiria wao na kuwamaliza

Wivu tu na wao wakati abiria wapo wa kutosha mpaka wanasimama kwenye hizo daladala
 
waache uzuzu biashara ushindani wapambane. Sasa wanamgomea nani, je hizo bajaji wakirasimishiwa hiyo biashara hayo magari yao watayafanyia nini. Ningekuwa serikali atakayetoa gari lake barabarani atajua pakuipeleka maana haitarudi barabarani.

IIiwahi kutokea hii ya kufutiwa leseni mwaka 2003 kule kwa akina yakhee wasemaje atii.
 
Hivi hawa dala dala wanafikiri uamzi wao huo utakuwa ni mwarobaini? Wapambane na hali zao hats hao bajaj wanauhitaji ule ule kama wao hivyo kila mmjoja atumie fulsa anayoipata.
 
Na waachwe tu kutoa Huduma, huwezi nishawishi nipande matatu kulingana na uharaka nilionao, na usafiri wa haraka na bei nafuu nauona
 
Sasa daladala zikigoma kupakia si ndio itakuwa sherehe ya bajaji kupakia kwa raha au wakati wamegoma watazizuia bajaji kupakia?
yaani abiria wa jiji la mwanza wahudumiwe na bajaji una chekesha kweli!!halafu huo umbali unaosafiri kwa daladala kwa nauli ya 500,ndio hiyo hiyo utalipia kwa bajaji?!!
 
Biashara huria unakuta gari inapakia massa kibao halafu wanalugha chafu
 

Wamiliki na madereva wa daladala jijini Mwanza wamesema watasitisha kutoa huduma ya usafiri kwa wakazi wa jiji hilo kufuatia uwepo wa bajaji mjini zinazobeba abiria katika vituo vya daladala na kupelekea wao kushindwa kufanya kazi.

Hayo yamebainishwa kwenye kikao maalum kilichowakutanisha madereva wa daladala, pikipiki na bajaji pamoja na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), kikao ambacho kimelenga kusikiliza changamoto walizonazo madereva na kuzitafutia ufumbuzi ambapo madereva wa daladaa wamesema uwepo wa bajaji mjini pamoja na faini za makosa ya barabrani umepelekea wao kufilisika.

Zakayo Mashamba ni dereva bajaji naye akazungumza kuhusu malalamiko yaliyotolewa na wamiliki na madereva wa daladala.

"Wanaoendesha hiache na costa nashukuru leo wamekuwa wawazi tulikuwa tunaona wanazirusha bajaji tulikuwa hatujui kumbe kuna namna, nashukuru leo tumejua, wote sisi ni Watanzania mipaka haiongezeki lakini watu wanaongezeka sasa sisi watu wa bajaji tukale wapi?," amehoji Mashamba.

Wakijibu malalamiko ya wamiliki na madereva wa daladala Mkurugnezi wa Huduma za Uchukuzi kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Aron Kisaka, pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa LATRA Habibu Suluo, wamesema kama madereva wa bajaji wanapakia abiria kwenye vituo vya daladala wanafanya makosa.

Chanzo: EATV
dala dala mlitutesa sana mala mkatize luti matusi kwa makonda wizi nk bajaji kwanza wanaenda na muda hacheni kuogopa ushindani hakuna kazi ya pekeyoko
 
Kule Unguja wakati zinaingia bodaboda na bajaji walipiga majungu sana, mara vibaka, mara wanabeba ovyo wake za watu, mara hawana leseni, mara mara kibaoo.

Kuna binadamu walidhani mpaka mwisho wa dunia ni mwendo wa Vespa, leo kila sehemu, mtu ana namba ya bodaboda wake na mpaka mheshimiwa Dr. Mwinyi anaalikwa kwemda kugawa bodaboda za mikopo.
 

Wamiliki na madereva wa daladala jijini Mwanza wamesema watasitisha kutoa huduma ya usafiri kwa wakazi wa jiji hilo kufuatia uwepo wa bajaji mjini zinazobeba abiria katika vituo vya daladala na kupelekea wao kushindwa kufanya kazi.

Hayo yamebainishwa kwenye kikao maalum kilichowakutanisha madereva wa daladala, pikipiki na bajaji pamoja na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), kikao ambacho kimelenga kusikiliza changamoto walizonazo madereva na kuzitafutia ufumbuzi ambapo madereva wa daladaa wamesema uwepo wa bajaji mjini pamoja na faini za makosa ya barabrani umepelekea wao kufilisika.

Zakayo Mashamba ni dereva bajaji naye akazungumza kuhusu malalamiko yaliyotolewa na wamiliki na madereva wa daladala.

"Wanaoendesha hiache na costa nashukuru leo wamekuwa wawazi tulikuwa tunaona wanazirusha bajaji tulikuwa hatujui kumbe kuna namna, nashukuru leo tumejua, wote sisi ni Watanzania mipaka haiongezeki lakini watu wanaongezeka sasa sisi watu wa bajaji tukale wapi?," amehoji Mashamba.

Wakijibu malalamiko ya wamiliki na madereva wa daladala Mkurugnezi wa Huduma za Uchukuzi kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Aron Kisaka, pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa LATRA Habibu Suluo, wamesema kama madereva wa bajaji wanapakia abiria kwenye vituo vya daladala wanafanya makosa.

Chanzo: EATV
hao wenye vipanya mwanza sio wafanya biashari ya usafirishaji wa abiriya sababu wanaogopa ushindani
 
Back
Top Bottom