Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Bado tuu ruti ya kiboriloni,Aisee moshi imezid kwa bajaji, sidhani kama kuna mji una bajaji nyingi kama mji wa moshi manispaa
Mbeya kuna bajaji si mchezoAisee moshi imezid kwa bajaji, sidhani kama kuna mji una bajaji nyingi kama mji wa moshi manispaa
Hii route usiku kuanzia Buzuruga hadi Bwiru kona sawa ila mchana vinapiga Buzuruga Kiloleni siyo mbayaMadereva wanao lalamika route yao haina abiria wengi
NYASAKA MZUNGUKO
Wapumbavu kabisa, waonyeshe abiria waliosajiliwa kwenye daladala zao
waache uzuzu biashara ushindani wapambane. Sasa wanamgomea nani, je hizo bajaji wakirasimishiwa hiyo biashara hayo magari yao watayafanyia nini. Ningekuwa serikali atakayetoa gari lake barabarani atajua pakuipeleka maana haitarudi barabarani.
Hapa Iringa Bajaj zilimstaafisha Mkuu wa Wilaya Dr KaseselaWazire bajaji ziendelee na kazi.
Oyaa tuliza makasesera hayo.Hapa Iringa Bajaj zilimstaafisha Mkuu wa Wilaya Dr Kasesela
Mbeya kuna bajaji si mchezo
yaani abiria wa jiji la mwanza wahudumiwe na bajaji una chekesha kweli!!halafu huo umbali unaosafiri kwa daladala kwa nauli ya 500,ndio hiyo hiyo utalipia kwa bajaji?!!Sasa daladala zikigoma kupakia si ndio itakuwa sherehe ya bajaji kupakia kwa raha au wakati wamegoma watazizuia bajaji kupakia?
Aisee moshi imezid kwa bajaji, sidhani kama kuna mji una bajaji nyingi kama mji wa moshi manispaa
🤣 🤣 🤣 🤣 Aisee. Kuna moja niliona mtandaoni. Imeandika Iringa to Arusha nadhani.Kuna siku bajaji watataka kwenda mikoani
dala dala mlitutesa sana mala mkatize luti matusi kwa makonda wizi nk bajaji kwanza wanaenda na muda hacheni kuogopa ushindani hakuna kazi ya pekeyoko
Wamiliki na madereva wa daladala jijini Mwanza wamesema watasitisha kutoa huduma ya usafiri kwa wakazi wa jiji hilo kufuatia uwepo wa bajaji mjini zinazobeba abiria katika vituo vya daladala na kupelekea wao kushindwa kufanya kazi.
Hayo yamebainishwa kwenye kikao maalum kilichowakutanisha madereva wa daladala, pikipiki na bajaji pamoja na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), kikao ambacho kimelenga kusikiliza changamoto walizonazo madereva na kuzitafutia ufumbuzi ambapo madereva wa daladaa wamesema uwepo wa bajaji mjini pamoja na faini za makosa ya barabrani umepelekea wao kufilisika.
Zakayo Mashamba ni dereva bajaji naye akazungumza kuhusu malalamiko yaliyotolewa na wamiliki na madereva wa daladala.
"Wanaoendesha hiache na costa nashukuru leo wamekuwa wawazi tulikuwa tunaona wanazirusha bajaji tulikuwa hatujui kumbe kuna namna, nashukuru leo tumejua, wote sisi ni Watanzania mipaka haiongezeki lakini watu wanaongezeka sasa sisi watu wa bajaji tukale wapi?," amehoji Mashamba.
Wakijibu malalamiko ya wamiliki na madereva wa daladala Mkurugnezi wa Huduma za Uchukuzi kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Aron Kisaka, pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa LATRA Habibu Suluo, wamesema kama madereva wa bajaji wanapakia abiria kwenye vituo vya daladala wanafanya makosa.
Chanzo: EATV
hata iringa[emoji28][emoji28]naona bajaji siku izi zina taka kuchukua utawala kwa kasi kama kule moshi
hao wenye vipanya mwanza sio wafanya biashari ya usafirishaji wa abiriya sababu wanaogopa ushindani
Wamiliki na madereva wa daladala jijini Mwanza wamesema watasitisha kutoa huduma ya usafiri kwa wakazi wa jiji hilo kufuatia uwepo wa bajaji mjini zinazobeba abiria katika vituo vya daladala na kupelekea wao kushindwa kufanya kazi.
Hayo yamebainishwa kwenye kikao maalum kilichowakutanisha madereva wa daladala, pikipiki na bajaji pamoja na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), kikao ambacho kimelenga kusikiliza changamoto walizonazo madereva na kuzitafutia ufumbuzi ambapo madereva wa daladaa wamesema uwepo wa bajaji mjini pamoja na faini za makosa ya barabrani umepelekea wao kufilisika.
Zakayo Mashamba ni dereva bajaji naye akazungumza kuhusu malalamiko yaliyotolewa na wamiliki na madereva wa daladala.
"Wanaoendesha hiache na costa nashukuru leo wamekuwa wawazi tulikuwa tunaona wanazirusha bajaji tulikuwa hatujui kumbe kuna namna, nashukuru leo tumejua, wote sisi ni Watanzania mipaka haiongezeki lakini watu wanaongezeka sasa sisi watu wa bajaji tukale wapi?," amehoji Mashamba.
Wakijibu malalamiko ya wamiliki na madereva wa daladala Mkurugnezi wa Huduma za Uchukuzi kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Aron Kisaka, pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa LATRA Habibu Suluo, wamesema kama madereva wa bajaji wanapakia abiria kwenye vituo vya daladala wanafanya makosa.
Chanzo: EATV