Uchaguzi 2020 Mwanza Huduma adaiwa kumwaga pesa kama Njugu Bunda Mjini akisindikizwa na Viongozi wa CCM Wilaya

Uchaguzi 2020 Mwanza Huduma adaiwa kumwaga pesa kama Njugu Bunda Mjini akisindikizwa na Viongozi wa CCM Wilaya

chuki

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2011
Posts
2,715
Reaction score
534
Katika hali ya kushangaza Zury Nanji maarufu kama Mwanza Huduma Mfanyabiashara wa Jijini Mwanza ameonekana Bunda Mjini akigawa pesa hadharani.

Huku akiwa na mabaunsa, wapambe na wanakwaya wakimsindikiza Mwanza Huduma amepita Vijiwe vya Kahawa na Maegesho ya Magari na kugawa kati ya shilingi Elfu 50 na laki moja kwa watu hadharani, Pia amepita kwa baadhi ya Mabalozi wa nyumba kumi na kumwaga laki mbili na laki tatu.

Akionekana kujiamini amekusanya baadhi ya wazee katika nyumba moja ya Balozi Semeni Kasuku na kutoa Laki NNE.

Wapambe wa karibu nae wamekabidhiwa shilingi Milioni Moja na kuanza kugawa Elfu kumi Au Elfu kumi na tano kwa Vijana wa Bodaboda na Wanakwaya maalum kwaajili ya kumpamba 'mgombea' huyo.

Kabla tukio hilo la kujitokeza hadharani, Baadhi ya Viongozi akiwemo Mwenezi wa CCM Wilaya Ndugu Bonavencha Makanga akiwa na wasaidizi wake walipita kwa Makatibu wa Kata na kuwapatia posho (rushwa) na baadhi ya Wenyeviti kama sehemu ya salam za Mhindi huyo ambae ameanza kampeni mapema kabla ya muda.

Leo walipoulizwa kwanini wanafanya mambo hayo hadharani bila kuogopa Mpambe wa karibu ajulikanae kama Masalu na Mwingine Selemani Nasoro walisema wamepata kibali kwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya hivyo hawatishwi na mtu.

Hali hii isipodhibitiwa Bunda Mjini wagombea watatoana Taya maana Rushwa kwa viongozi wengi inatisha kama Corona.
 
Hauna Kapicha mkuu hata ka hao wazee wakati wakigaiwa hizo ntongoro
 
Sasa nan wa kukataa Pesa na wewe....yaan mi nipewe laki moja niikatae et nalinda kura ya Ester Bulaya huo ujinga siwezi
 
WanaCCM halisi wapo! Na wapo kila kona!! Hata kwenye makambi ya vyama vya upinzani bado wapo wengi, kuhamahama huku ulikoona majuzi hakujawamaliza! Wapo hata umo nyumbani mwenu! Popote ulipo ukitaka kumgundua mwanaCCM damudamu we mpe mtihani mmoja: MWEKE KWENYE MTUMBWI AU NGALAWA, KISHA HUMO NDANI WEKA BOX LA HELA LENYE ANGALAU SH. LAKI MBILI NA PIA MWEKE MAMA YAKE MZAZI AU HATA NDUGUYE WA KUZALIWA. ALAFU wasokomeze kwenye mto uendao kasi au bahari iliyochafuka dhoruba.

NAKUAPIA KABLA ROBO SAA HAIJAPITA JAMAA ATAKUIBUKIA UFUKWENI AKIWA AMEBEBA BOX LAKE LA HELA HUKU ANASHANGILIA!!!! Hapo umuulize mama yake au nduguye kamwachaje kufa maji atakupa maelezo meeeengi ila hutakosa kumsikia akitaja neno "maendeleo" na usishangae akikwambia pia ametekeleza naniliu! MSUKULE NA MWENYE MSUKULE NI NDUGU WA DAMU!!!

Don't make a promise you can't fulfill...
 
Naamni TAKUKURU wamo humu watakua wameona uzi huu wa kizarendobna wataufanyia kazi na tutapata mrejesho
 
chuki, Mkuu Chuki, acha chuki.
Maadam wanufaika na fedha hizo ni wananchi, hakuna ubaya wowote kwa mwenye fedha yoyote kugawa fedha zozote kwa wananchi wahitaji kwa nia yoyote au bila nia yoyote, cha muhimu ni wananchi watapata pesa za bure bure.

Tena nitaishauri CCM ifungue fursa, kila mwana CCM yoyote mwenye fedha ya kumwaga, inayomuwashawasha, na angependa kuitumia hiyo fedha yake kama means ya kutangazia nia ya kugombea jimbo lolote, aruhusiwe, iwe rukhsa kujipitisha pitisha kumwaga fedha, wananchi wanufaike.

Kwavile mwisho wa siku, wanaopitisha majina ya wagombea ni vikao vya juu vya chama, na sifa za kupitishwa sio umegawa fedha kiasi gani, bali chama kitawapitisha wagombea bora, na ikitokea wewe mgawa fedha ndio umepitishwa, unakuwa umepitishwa kwa kukidhi vigezo na sio kwasababu iligawa fedha.
P
 
KATIKA KUJIPANGA KWAKO, FROM NOW ONWARDS PIMA VIZURI MANENO YAKO, KABLA HUJAYAANDIKA, YATAKUJA KUKUSAKAMA NA KUKUKOMOA.

HAPA CHINI IS AN EXAMPLE OF A VERY POOR COMMENT, IT SHOWS YOU CONDON CORRUPTION AND A GREAT SUPPORTER OF IT.
Mkuu Chuki, acha chuki.
Maadam wanufaika na fedha hizo ni wananchi, nitaishauri CCM, kila mwana CCM mwenye fedha na nia ya kugombea jimbo lolote, rukhsa kujipitisha pitisha kumwaga fedha, wananchi wanufaike.
P

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkirindi, Mkuu Mkirindi, mimi ni realist na muumini wa free speech na freedom of expression, hivyo I always speak my mind freely and expresses my opinions truthfully.

Kama kuna watu wana pesa zinazo wawasha, wanagawa fedha hizo kama njugu kwa wananchi for whatever reasons, wafaidika na wanufaika wa fedha hizi ni wananchi wa maeneo hayo, kuna ubaya gani?.

Nachukia rushwa ambayo ni adui wa haki, lakini sina tatizo kabisa na takrima, as long as uwezo wa kutoa takrima, sio kigezo cha kupitishwa kuteuliwa kuwa mgombea. Huu mimi nauita ni uwezeshaji wananchi Kiuchumi. Acha wenye fedha wagawe fedha kwa wananchi ili wananchi wanufaike na fedha hizo. Kuna ubaya gani haoo?.
P
 
Back
Top Bottom