Mwanza: Mgambo Waliowapora Machinga ndizi wasimamishwa, Waziri aingilia, Halmashauri yaomba radhi

Mwanza: Mgambo Waliowapora Machinga ndizi wasimamishwa, Waziri aingilia, Halmashauri yaomba radhi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

Kufuatia Video iliyosambaa mitandaoni ikionyesha Mjasiriamali mdogo wa ndizi akichukuliwa bidhaa zake na mgambo wa Halmashauri ya Mwanza, kuna matamko kadhaa yametolewa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa

WAZIRI AAGIZA MKUU WA MKOA AINGILIA
"Nimeona video inayosambaa mitandaoni ikionesha matunda aina ya ndizi ya mfanyabiashara mdogo yakipakiwa na mgambo kwenye gari aina ya Toyota Hilux.
"Inasemekana tukio hili limetokea Jijini Mwanza. Namuagiza Mkuu wa Mkoa, Mhe. Eng. Gabriel Luhumbi kufuatilia kubainisha wahusika na hatua kali zichukuliwe dhidi yao.

"Ninaendelea kuwaelekeza Wakuu wa Mikoa kote nchini kuhakikisha zoezi la kuwapanga wafanyabiashara wadogo wa machinga linafanyika kwa utulivu na amani na kujali utu.
"Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya mpaka haya yanatokea kwenye maeneo yenu mjitathimini kama mnatosha," - Waziri Bashungwa.



Tamko Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kupitia barua kwa umma jana Jumamosi Aprili 16, 2022, umelaani vikali kitendo cha kinyama kama kinavyoonekana katika video inayosambaa mitandaoni kilichofanywa na baadhi ya Askari Mgambo wa Halmashauri, kuchukua bidhaa aina ya ndizi za Wajasiriamali wadogo yaani Machinga.

Bidhaa hizo zilizokuwa zinauzwa katika toroli na zinaonekana kutupiwa katika gari ya Halmashauri na Mgambo hao kinyume na taratibu za Oparesheni ya kuwaondoa Machinga katika maeneo yasiyo rasmi tukio ambalo ni la unyanyasaji na linahatarisha usalama wa mali za Wafanyabiashara ikiwemo kupoteza ubora na kuharibika kabisa.

Halmashauri ya Jiji la mwanza haihusiki kwa namna moja au nyingine kuagiza Askari kuendesha zoezi hili kwa namna linavyoonekana bali ni utashi na nía ovu ya Askari Mgambo hao jambo mbalo ni kinyume kabisa cha maelekezo ya oparesheni.

Kufuatia hili Uongozi wa Halmashauri umechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwasimamisha Askari Mgambo waliohusika kutojihusisha katika Oparesheni ya kuwaondoa machinga katika maeneo yasiyo rasmi wakati taratibu nyingine za kisheria zikiendelea kufanyika dhidi ya wahusika wote.

Halmashauri inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa umma hasa wafanyabishara waliopata kadhia hii na kusisitiza kuwa Halmashauri inaongozwa kwa miongozo, sheria na taratibu kwa kuzingatia utu na maadili na inatoa wito kwa Askari Mgambo kuwa waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingatia miongozo, sheria na taratibu.


Source: Global Publishers
 
Watafute namna ya kudeal nao kuliko kuwapora bidhaa zao, then wanaenda uza au gawana mbele
 
Nchi ya kunyanyasana,hata sungusungu nao wanaadhibu machinga.
Bado watanzania waliowengi hawana upendo baina yao. Tubadilike
 
Jana niliona Kariakoo machinga wamerudi wanauza bidhaa zao kama kawaida! Mwanza acheni upole wa kisukuma, rudini mtaani mtakufa na njaa....
Royal Tour ni kwa manufaa ya watanzania daraja la kwanza sio nyie kapuku!
 
Hapa inabidi iwe jino Kwa jino ,haiwezekani ukatili kama Io unafanyika alafu wanaangalia tu ,apo ilibidi iyo gari ichakazwe Kwa mawe na ao kina chacha wachapwe bakora wasahau kabisa iyo kazi ya mgambo
 
Social media inazid kupata nguvu kama sio nguvu ya facebook Twitter instagram telegram WhatsApp hakuna ambae angefahamu
 
Jana niliona Kariakoo machinga wamerudi wanauza bidhaa zao kama kawaida! Mwanza acheni upole wa kisukuma, rudini mtaani mtakufa na njaa....
Royal Tour ni kwa manufaa ya watanzania daraja la kwanza sio nyie kapuku!
Wanauza lakini ile mijamaa inapita kuunga hata jero ukiwapa wanasepa
Ubaya lile gari likitimba la /Dfp hawakuachiii
 
Mtafanya Nini hamna uwezo wa kuiondoa CCM kupitia sanduku la kura
Sijaskia kauli ya kufidia mhanga(status quo)!
Tatzo ni mbinu zote zilizobak hazijadiliki eneo kama hili! Sijui itakuweje kukombolewa!
Tatzo kubwa ni hakuna kiongoz wa msafara wa safar ya ukomboz kwa njia iliyobaki, licha ya wahanga:
a) nia wanayo
b) sabab wanayo
c) uwezo wanao
Kwa sasa tuendelee na maomb ya tumaini la simba kushiba swala tukapita!
......THERE MUST BE CLASSES ON EARTH AS IN HEAVEN, BUT LET THEM BE NATURAL!
 

Kufuatia Video iliyosambaa mitandaoni ikionyesha Mjasiriamali mdogo wa ndizi akichukuliwa bidhaa zake na mgambo wa Halmashauri ya Mwanza, kuna matamko kadhaa yametolewa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa

WAZIRI AAGIZA MKUU WA MKOA AINGILIA
"Nimeona video inayosambaa mitandaoni ikionesha matunda aina ya ndizi ya mfanyabiashara mdogo yakipakiwa na mgambo kwenye gari aina ya Toyota Hilux.
"Inasemekana tukio hili limetokea Jijini Mwanza. Namuagiza Mkuu wa Mkoa, Mhe. Eng. Gabriel Luhumbi kufuatilia kubainisha wahusika na hatua kali zichukuliwe dhidi yao.

"Ninaendelea kuwaelekeza Wakuu wa Mikoa kote nchini kuhakikisha zoezi la kuwapanga wafanyabiashara wadogo wa machinga linafanyika kwa utulivu na amani na kujali utu.
"Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya mpaka haya yanatokea kwenye maeneo yenu mjitathimini kama mnatosha," - Waziri Bashungwa.



Tamko Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kupitia barua kwa umma jana Jumamosi Aprili 16, 2022, umelaani vikali kitendo cha kinyama kama kinavyoonekana katika video inayosambaa mitandaoni kilichofanywa na baadhi ya Askari Mgambo wa Halmashauri, kuchukua bidhaa aina ya ndizi za Wajasiriamali wadogo yaani Machinga.

Bidhaa hizo zilizokuwa zinauzwa katika toroli na zinaonekana kutupiwa katika gari ya Halmashauri na Mgambo hao kinyume na taratibu za Oparesheni ya kuwaondoa Machinga katika maeneo yasiyo rasmi tukio ambalo ni la unyanyasaji na linahatarisha usalama wa mali za Wafanyabiashara ikiwemo kupoteza ubora na kuharibika kabisa.

Halmashauri ya Jiji la mwanza haihusiki kwa namna moja au nyingine kuagiza Askari kuendesha zoezi hili kwa namna linavyoonekana bali ni utashi na nía ovu ya Askari Mgambo hao jambo mbalo ni kinyume kabisa cha maelekezo ya oparesheni.

Kufuatia hili Uongozi wa Halmashauri umechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwasimamisha Askari Mgambo waliohusika kutojihusisha katika Oparesheni ya kuwaondoa machinga katika maeneo yasiyo rasmi wakati taratibu nyingine za kisheria zikiendelea kufanyika dhidi ya wahusika wote.

Halmashauri inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa umma hasa wafanyabishara waliopata kadhia hii na kusisitiza kuwa Halmashauri inaongozwa kwa miongozo, sheria na taratibu kwa kuzingatia utu na maadili na inatoa wito kwa Askari Mgambo kuwa waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingatia miongozo, sheria na taratibu.


Source: Global Publishers
Pamoja kuomba radhi haitoshi!
Wahusika wametumia unyanyasaji na maytumizi mabaya ya vyombo vya umma (gari) wanapaswa adhabu wa kusimamishwa miezi kadhaa kwanza.

Sent from my SM-A115AZ using JamiiForums mobile app
 
Kumbe kurekodi video kunasaidia sana.

Ndani ya siku hizi chache wananchi waliorekodi video za uonevu dhidi yao, video zao zimewasaidia kwa namna moja/nyingine.

Wakuu kama kuna jambo haliko sawa turekodi.
 
Sijaskia kauli ya kufidia mhanga(status quo)!
Tatzo ni mbinu zote zilizobak hazijadiliki eneo kama hili! Sijui itakuweje kukombolewa!
Tatzo kubwa ni hakuna kiongoz wa msafara wa safar ya ukomboz kwa njia iliyobaki, licha ya wahanga:
a) nia wanayo
b) sabab wanayo
c) uwezo wanao
Kwa sasa tuendelee na maomb ya tumaini la simba kushiba swala tukapita!
......THERE MUST BE CLASSES ON EARTH AS IN HEAVEN, BUT LET THEM BE NATURAL!
Hapo yupo na Mbunge wa Nyamagana na Mkuu wa Mkoa natumaini atafidiwa zaidi
IMG-20220417-WA0032.jpg
 
Back
Top Bottom