Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
ok soon Napost Kingine...
tonight....
Braza Rakim kwanza pole sana na majukumu ya maisha na Mungu akuzidushie na akupeckila uliombalo lenye heri ivna wewe
Nimesoma madarasa yako yote ni mazuri na elimu. Ahsnte kwa elimu
Mimi kwa sasa nimeanza kuingia kwenye ulimwengu wa ndoto ninaota ndoto nyingi sana zinazohusiana na maisha yangu na kilichonishangaza zaidi kipindi hiki kila ikifika muda wa kusali asubuhi naingiwa na. mbu wa pua au mashikioni ninaamka na kusali.
Mara nyingine namsikia mtoto wangu ananiita na mara nyingine nimeota mtoto wangu ananiambia na mm nataka kutia udhu muda huo wote huwa ni karibu na sala.
Jana niliota kuna mtu ananidai nikamuona usingizini nikamwambia sina pesa lkn nitakulipa siku ya Jumatano.
Nisaidie nina tatizo gani au faida gani?
Mkuu Rakims
Kwanza nashukuru kwa somo lako
hasa kuhusu Meditation. Nimeelewa na leo nimefanya meditation ya kukagua mwili wangu na yafuatayo ni matokeo yake.
Nilikuwa nimelala kama pozi langu la
kumeditate. Wakati nameditate nilikuwa nataja jina la Mungu kwa mujibu wa iman yangu baadae
nikajikuta nageuza kichwa changu upande wa kulia. Kisha mkono wangu wa kulia ukaanza kunyanyuka ukapanda hadi kifuani kisha ukarudi nilipokuwa nimeuweka baada ya kama sekunde tatu kichwa kikageukia upande wa kushoto nikajikuta nainua mkono wa kushoto hadi kifuani na kuurudisha ulipokuwa. Baada ya kama sekunde kumi nilikigeuza kichwa
kilipokuwa na kuanza kutingisha kama mtu mwenye pepo. Kilipotulia mikono
yote ikaanza kuinuka hadi kifuani ukitangulia mkono wa kushoto na wakulia juu yake. Baadae nikajikuta natoa mkono wa kulia kifuani na kuupeleka kama mtu anayetaka
kupokea kitu kisha mikono yote ikarudi
mahali ilipokuwa.
Naomba muongozo wako hapo je niko
sahihi kwa mtokeo hayo?
Haya Umefika Muda Wa Kurudi Darasani Chap Chap PM namba Yako Nikuingize Whatsapp Group Ya Meditation...
"Rakims"