Mwendokasi (BRT) msiishie kujenga barabara tu

Mwendokasi (BRT) msiishie kujenga barabara tu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Usafiri wa mwendo wa haraka ni jambo jema kwa uchumi kwakuwa unapunguza muda wa kukaa njiani na kuongeza muda wa kufanya kazi kwa siku, wiki, mwezi na mwaka.

Pamoja na kazi na kasi hii ya kujenga usafiri wa haraka lakini lazima ujenzi huu uzingatie pia kujenga vituo vikubwa vya kuegesha magari ya watu binafsi kutoka pembezoni mwa mji yasifike katikati ya mji sambamba na mabasi yenu ya BRT.

Hivi ni vituo ambavyo magari madogo ya watu binafsi kutoka maeneo yasiyofikiwa na mradi yataegeshwa hapo kwa malipo kidogo wakati mwenye gari hilo anabadilisha usafiri kutoka gari lake binafsi kwenda kwenye BRT kuendelea na safari yake kuelekea city center.

Hii itapunguza msongamano, moshi wa magari, kelele za magari na magereji katikati ya mji. Pili magari ya mwendo wa haraka yawe na ratiba inayofahamika kwa muda na siku.

Tatu, magari ya mradi wa BRT yote yatumie gesi ili kutunza mazingira kwa kupunguza Moshi katikati ya mji na kupunguza gharama za uendeshaji wa mradi kwa kuwa gesi ni rahisi lakini haibiwi na madereva wa magari kama ilivyo kwa mafuta ya magari.

Ndugu zangu kujenga nchi sio lazima uteuliwe na Rais na kupewa maagizo. Tujiongeze.
 
nchi iuzwe tu kwani nini
Duniani kote watu wanachojali ni maisha mazuri na huduma nzuri baasi. Huko Japan, Korea kusini, Taiwan, Dubai, Onan, Marekani, nk wageni ndio wanaomiliki mali, kazi ya serikali ni kukusanya Kodi na kuhudumia wananchi. Hakuna mtu Yuko tayari kuuza na kununua nchi na watu wake wote. Kimachotakiwa ni kujenga taasisi (katiba, mahakama, bunge na serikali) zenye nguvu na Bora kabla ya kubinafsisha miundombinu yetu.
 
waarabu waambiwe walete MABUS tushajenga barabaraaaa 😀 😀 😀shtihole country
Tulikosea sana kuwanyang'anya Wazungu Yale mashamba makubwa ya mkonge, ngano na chai ambayo Sasa hivi yamegeuka maporimwitu. Hawa wasomi wetu wanaopinga bandari kubinafsishwa hawasaidii kutoa ushauri wa namna ya kufufua Yale mashamba ya mkonge, viwanda vya nguo, viwanda vya magurudumu ya magari vilivyokufa, hawatoi ushauri juu ya kusaidia wakulima waondokane na jembe la mkono.

Wasomi wetu hawana tofauti na raia wa kawaida linapokuja swala la siasa na uchumi. Hebu Ona, kule bungeni zinakotungwa sheria wako akina Musukuma, majimarefu na wananchi wa kawaida TU wakati wasomi wetu uchwara wako ofisini kusubiri kutekeleza sheria zilizotungwa na akina Musukuma na Mpina.
 
Duniani kote watu wanachojali ni maisha mazuri na huduma nzuri baasi. Huko Japan, Korea kusini, Taiwan, Dubai, Onan, Marekani, nk wageni ndio wanaomiliki mali, kazi ya serikali ni kukusanya Kodi na kuhudumia wananchi. Hakuna mtu Yuko tayari kuuza na kununua nchi na watu wake wote. Kimachotakiwa ni kujenga taasisi (katiba, mahakama, bunge na serikali) zenye nguvu na Bora kabla ya kubinafsisha miundombinu yetu.
MIMI sijui why tulifukuza sultan, leo tunamrudisha tena kivingine
 
Duniani kote watu wanachojali ni maisha mazuri na huduma nzuri baasi. Huko Japan, Korea kusini, Taiwan, Dubai, Onan, Marekani, nk wageni ndio wanaomiliki mali, kazi ya serikali ni kukusanya Kodi na kuhudumia wananchi. Hakuna mtu Yuko tayari kuuza na kununua nchi na watu wake wote. Kimachotakiwa ni kujenga taasisi (katiba, mahakama, bunge na serikali) zenye nguvu na Bora kabla ya kubinafsisha miundombinu yetu.
Waafrika wamefeli kujisimamia Nini kifanyike,Ni kubinafisha au kununua management ya kutusimamia na kununua management ya kuisimamia hio management ya kutuongoza sisi tubakie kula gawio tu.
Hili tuachane kutegemea zaidi Kodi kama chanzo Cha mapato kwa kuwakamua watu masikini,kwani Kodi ni kikwazo Cha mtu mmoja mmoja kujikwamua.
 
Tumrudishe Sultan tu kwa kweli.
 
MIMI sijui why tulifukuza sultan, leo tunamrudisha tena kivingine
Ilikuwa mihemko TU, hatuwezi bhana!! Watu wetu wanapoteza muda Mwingi kwa kucheza ngoma na kuimba kwenye vikao na mikutano yetu ya kufanya maamuzi badla ya kutumia muda huo kutafakari na kuzalisha. Hatuko makini ni kunengua TU kila mahali.
 
Usafiri wa mwendo wa haraka ni jambo jema kwa uchumi kwakuwa unapunguza muda wa kukaa njiani na kuongeza muda wa kufanya kazi kwa siku, wiki, mwezi na mwaka.

Pamoja na kazi na kasi hii ya kujenga usafiri wa haraka lakini lazima ujenzi huu uzingatie pia kujenga vituo vikubwa vya kuegesha magari ya watu binafsi kutoka pembezoni mwa mji yasifike katikati ya mji sambamba na mabasi yenu ya BRT.

Hivi ni vituo ambavyo magari madogo ya watu binafsi kutoka maeneo yasiyofikiwa na mradi yataegeshwa hapo kwa malipo kidogo wakati mwenye gari hilo anabadilisha usafiri kutoka gari lake binafsi kwenda kwenye BRT kuendelea na safari yake kuelekea city center.

Hii itapunguza msongamano, moshi wa magari, kelele za magari na magereji katikati ya mji. Pili magari ya mwendo wa haraka yawe na ratiba inayofahamika kwa muda na siku.

Tatu, magari ya mradi wa BRT yote yatumie gesi ili kutunza mazingira kwa kupunguza Moshi katikati ya mji na kupunguza gharama za uendeshaji wa mradi kwa kuwa gesi ni rahisi lakini haibiwi na madereva wa magari kama ilivyo kwa mafuta ya magari.

Ndugu zangu kujenga nchi sio lazima uteuliwe na Rais na kupewa maagizo. Tujiongeze.
Bahati mbaya wateule hawana fikra wala kujiongeza!
 
Duniani kote watu wanachojali ni maisha mazuri na huduma nzuri baasi. Huko Japan, Korea kusini, Taiwan, Dubai, Onan, Marekani, nk wageni ndio wanaomiliki mali, kazi ya serikali ni kukusanya Kodi na kuhudumia wananchi. Hakuna mtu Yuko tayari kuuza na kununua nchi na watu wake wote. Kimachotakiwa ni kujenga taasisi (katiba, mahakama, bunge na serikali) zenye nguvu na Bora kabla ya kubinafsisha miundombinu yetu.
Tz tuko kwenye mdororo wa akili, hatuna lolote lililo bora, linaloonesha kujiandaa na kuendana na zama za teknolojia, si Katiba inayosimamia, si taasisi zinazojisimamia, si uongozi bora wenye weledi na maadili.
 
Waafrika wamefeli kujisimamia Nini kifanyike,Ni kubinafisha au kununua management ya kutusimamia na kununua management ya kuisimamia hio management ya kutuongoza sisi tubakie kula gawio tu.
Hili tuachane kutegemea zaidi Kodi kama chanzo Cha mapato kwa kuwakamua watu masikini,kwani Kodi ni kikwazo Cha mtu mmoja mmoja kujikwamua.
Ukiangalia huu tunaouita msongamano wa magari DSM utagundua kuwa ni magari yenye mtu mmoja TU na siti nyingine 4 za gari ziko tupu, huyo mtu anaamua kutoka Kibaha hadi postal na gari lake kwakuwa usafiri wa umma hauna hadhi, haujapangwa na haifahamiki basi lipi linakuja na kuondoka muda gani.
 
Back
Top Bottom