unachoongea ni ukweli mkuu,watu wengi wanapenda kujazana pale mlangoni alafu huku mbele na katikati kunakuwa na nafasi kubwa tu ila watu hawaendi,mtoa mada akiambiwa mambo madogo kama hayo na mlinzi wa darasa la nne anaona kaonewa na Phd yake.Hayo magari watu wanajazana mlangoni ndani kweupe sana ingekuwa wanagunguwa mlango mmoja watu wanaingia kwa mstari miwili uku na uku then kati kati, ila utaratibu mbovu na watu hawaendi bila kusimamiwa
VIpi kuhusu kuendesha biashara kaa hasara kwa kigezo cha huduma bora. Sema huduma stahiki kulingana na uwezo wake sio boraMwananchi ana haki ya kupata huduma bora kwa bei nafuu, sio bora huduma
Kabisa yani,, subiri uchaguzi ukaribie hapo ndo utashangaa!Ili kiongozi aonekane anafanya kazi ni lazima awape matatizo ili siku akitatua mmpigie makofi
[emoji848]Ccm hakuna wanachoweza zaidi ya uchawi..na uganga..hata wewe ni ccm utakuwa mchawi tu
kiujumla Tanzania mambo mengi yenye manufaa kwa wananchi yamefeli!, taasisi za serikali tunazozitarajie zituhudumie ni rushwa na utendaji mbovu! USAFIRI - tumeshindwa hata na rwanda au kenya. public transport zipo zinawasubiri abiria wapande, watanzania tuna kuwa kama mifugo kwenye suala la usafiri. USALAMA WA CHAKULA - TBS inayomifumo ya kudhibiti usalama wa chakula lakini TBS hiyo hiyo haitekelezi mifumo yake hiyo ambayo inafanana na mifumo ya kimataifa hamna wa kuwauliza tunaoumia ni watanzania mfano mzuri juisi ya AZAM embe mwongozo unakataza CMC lakini AZAM EMBE inawekwa CMC kinyume na matakwa ya kiwango na TBS wamethibitisha usalama wake pamoja na kwamba ame declare kabisa kuitumiaSamahani Leo nimeamka sio poa!
Unafika kivukoni mabasi sita yamepaki mnasubiriwa mjazane dakika ishirini nzima mmekaa tu mmejaa hasira Kali eti mnasubiri bus na mnayaona yamepaki hatimae ghafla wanaachia basi moja la kimara wote mnakimbilia spidi kali kupanda kama wanyama pori manyumbu wengine mnapamia wazee wanaanguka mnaombana samahani, wengine wanaangusha cm na pochi hawajui masikini akili iko kwenye kuwahi siti dirishani basi abiria mnajazwa kama nyanya bus linaondoka humo ndani kuna harufu Kali mmejaa kama nyanya mtu hata kuhema mtu huwezi umebanwa hugeuki ukikaa vibaya unaibiwa cm na pochi! Halafu pale kuna Mgambo wa darasa la nne wanafokea watu na PhD zao, wanakwambia wewe panga mstari haraka uingie kwenye bus alaaa!!
Saa zingine mara uko fire gari zinàkuja za kwenda kimara watu wamejaa hata mlango haufunguki gari ikifika fire ukiwaangalia abiria walioko ndani wamebanwa wametoa macho kama mijusi imebanwa na mlango wanapumua kwa shida majasho yanawavuja bàlaa wote wamekunja uso zao! Na hawataki wewe uingie!
Sasa Pale fire asubuhi labda unaumwa sana Sasa unasubiri bus la kwenda Muhimbili utakaa pale nusu saa nzima bus haliji mpaka unazidiwa na unaweza kudedi kama vipi eti mpaka mjazane kwanza ndo wapige cm eti mara ghafla utaona wanaleta bus moja tu mjazane kama nyanya mara wagonjwa wangine wako hoi! Ukiwauluza kwanini mabasi ya Muhimbili ni machache sana asubuhi saa zingine wanasema eti trafiki wa fire akiconcerntrate kuruhusu magari ya morogoro road tu basi mabasi yanayotoka Muhimbili kwenda Gerezani yanakwama kwenye foleni na kusababisha uhaba wa mabasi ya kwenda Muhimbili. Basi wanaohusika please mwambieni yule trafiki anazingua.
Kiukweli wenye wanaendesha huu mradi wa mwendokasi na viongozi waliowapa tenda wote wataenda jehannam maana si kwa kutesa watu hivi .
Kiukweli viongozi wengi wa Tanzania wanatesa sana raia wa nchi hii masikini. Watu wanateseka sana na inajulikana watesi wao wengi wakifa watafikia jehannam sababu wamejaa kiburi na viongozi wengi hudhani wataishi duniani milele kumbe wakifika miaka 70 tu wengi wao hufa kwa pressure na kupooza sababu ya kuwa na matumbo makubwa yaliyoshiba sukari iliyonunuliwa kwa Tozo za watu masikini. Hawa viongozi wakifa huwa Kuna dawa inaitwa Formalin wanapakwa Ili miili yao iliyokwisha kuanza kuoza isitoe harufu Kali. Nawakumbusha formalin inatusubiri duniani tunapita tu!
Mimi ni sisiem na Nina smart Kadi namuomba Bimkubwa Mh Rais Samia najua Yuko bize ila siku moja tu aje pale fire just one morning weekday saa moja aone mateso ya abiria wa mwendokasi.
Idadi ya mabasi ni ndogo mno kulinganisha na abiria kama vipi mabasi yaongezwe!
Nyie wababe UDART Wekeni route ya Kivukoni - Muhimbili kama vipi just for fun ikiwapendeza!
Good day!
Unapatikana Hai au kongwa ndugu ?Lengo kuu la mwendokasi ni kubeba abiria wengi. Unayaona hayo mabasi yamejaa ila watu wengi hujaa milangoni.
Zingatia bolded.Mimi ni sisiem na Nina smart Kadi namuomba Bimkubwa Mh Rais Samia najua Yuko bize ila siku moja tu aje pale fire just one morning weekday saa moja aone mateso ya abiria wa mwendokasi.
Good day!
Kuna tofauti kubwa ya Tanzania na nchi nyingine zinazotuzunguka, mfano jiji la Mombasa au hata Nairobi kuna matatu za serikali, kwa sababu wana ruzuku ya serikali basi huwa zinapuyanga barabarani kila baada ya 10mins.Udart wanajidalalia wenyewe kwa bus zao hapo ingekua ni Kampuni inayojitambua hizo mambo za watu kujazana zisingekuwepo maana kila dakika bus linalipita hasa asubuhi na jioni wao kazi yao ni kubeba tu abiria bara bara yao ila wanashindwa ingekuwa pana ushindani sijui ingekuwaje?
Fire kwenda muhimbili nayo ya kulalamika?si unatembea tu km ata moja inaweza isifike,vijana wa siku hizi nyoro nyoro sana
Kwanza bajaj unawah kushinda hayo.Ukiwa unatoka morocco , kivukoni au gerezani usku , ukashukia Kimara , kama una safari ya kwenda mbezi Bora ufanye mazoezi ya kuzunguka Tu daraja ukapande bajaji zinazoenda mbezi , ukisubir mwendo kasi ya mbezi utajutaaa ..yaan mabasi yapo tuu yamesimama na abiria mmesimama zaidi ya nusu saa Magari yanazunguka zunguka tuu , madereva nao sifa kibao....
Kama huna kigari au TVS basi panda bajaji ndo usafr murua kabisa Kwa DSM
Nadhan wazo zuri. Wale wale migambo wao wa kampuni ya China town sijui security wawe wanasaidia kufanya gar kwa mfano itoke level seat kwa kivukon.ili.kusudi na wa vituo vinafata wapate nafasi.Mwendokasi nahisi ni mradi wa mtu ambaye hawezi kuguswa. Ukitafuta nyuzi za kero za mwendokasi na ushauri wa kuboresha mwendokasi hazipungui hamsini humu JF lakini hakuna hatua zozote zimewahi kuchukuliwa walau hata kupunguza kero. Hivi inshindikana nini :-
-Wasimamizi hao hao wahakikishe kuwa mabasi yanapakia abiria kwa kiwango fulani kiasi abiria waweze kupumua vizuri na mama/dada/binti zetu wasiwe wanadhalilishwa na dunga dunga ndani ya mabasi.
- Kuwa angalau na ofisa mmoja kila kituo ambao watakuwa na mawasiliano ya redio call wakawa na mawasiliano na incharge mabasi yanapoanzia yaani gerezani, kivukoni, kimara, moroco na mbezi. Wawe wanasiliana muda wote kujua kila wakati wapi kuna abairia wengi ili mabasi mengi yaelekezwe huko kwa muda husika.
- Kila kituo kuwe angalau na wasimamizi wa kutosha kuhakikisha abiria wanapanada kwa foleni badala ya kusukumana, kukanyagana na kuibiana.
- Wasimamizi hao hao waweze kuhakikisha kuwa wajawazito, watoto, wazee, wagonjwa na wasijiweza wanapanda bila bugudha na wanakaa kwenye viti vyao husika ndani ya basi tofauti na sasa amabao viti hivyo vinakaliwa na watu wasistahili.
Mwisho ni ombi kwa serikali kwanini wasiruhusu wawekezaji wengine wenye uwezo katika sekta ya usafiri kama Azam waingie wapewe baadhi ya ruti na waruhusiwe walete idadi fulani ya mabasi ambayo itakuwa luxury na nauli waruhusiwe kuongeza kidogo. Kwa mfano unampa Azam ruti ya Mbezi - Kivukoni au Abood unampa ruti ya Gerezani Kimara. Naamini siku serikali ikifanya hivi ndio utakuwa mwisho wa foleni mjini kwani hawa jamaa lazima wataleta mabasi yenye viyoyozi na kuboresha usafiri kwa ujumla kiasi watu wengi watapaki magari yao majumbani na kuanza kutumia usafiri wa umma.