Mwenye majibu kuhusu jambo hili anisaidie nami nipate uelewa

Mwenye majibu kuhusu jambo hili anisaidie nami nipate uelewa

Joined
Jan 3, 2024
Posts
26
Reaction score
25
Mfumo wa demokrasia hapa nchini ulianzishwa rasmi mwaka 1992 chini ya Rais Mwinyi akiwa ndiye mwenyekiti wa chama mapinduzi CCM, na ndio kilikuwa chama pekee cha siasa kabla ya hapo kutokana na mfumo wa siasa wa wakati huo.
Najua suala la maamuzi ya kuruhusu mfumo wa mabadiliko ya kisiasa kutoka ujamaa hadi demokrasia haukufanywa na Mwinyi pekee kama Rais bali ni maamuzi ya chama kizima cha CCM ambacho kwa wakati ule kilikuwa ndio serikali yenyewe ukiondoa suala la chama. Najua waliwaza mengi na kujiridhisha kuwa ni sahihi nchi kubadili mfumo wake wa kisiasa huku CCM ikijua wazi inaruhisu wapinzani dhidi yake,hilo lilikuwa ni jambo jema sana kwa nchi kupata watu wenye mitazamo tofauti ili kupata mwenye mawazo bora kwa wakati husika kuongoza nchi pamoja na chama chake.
Sasa swali langu ni hili; kama ccm ilijua wasi kwamba inaruhusu upinzani dhidi yake kama chama tawala na ikaruhusu, sasa kwanini leo inatumia nguvu nyingi kukandamiza upinzani tena bila hata sababu? Au ilitegemea licha ya kuruhusu upinzani ya kwamba wasingetokea watu wa kuwapinga kihija na mitazamo? Au walikurupuka bila kujua athari zake kwa upande wao? Kama walijua ni kwanini sasa watu wenye mawazo tofauti na wao wanatendewa mambo mabaya ili hali wako sahihi kufanya hivyo na hawajavunja sheria? Leo tunasikia habari za watu wengi kutekwa na ukifiatilia wengi wao ni watu wa vyama vya upinzani haijawahi kutokea katekwa mtu wa CCM. Kumeshuhudiwa mara nyingi shughuli za vyama vya upinzani zikizuiwa na vyombo vya dola na shughuli hizo ziko kihalali na hawavunji sheria yoyote, mambo kama hayo hawajawahi fanyiwa watu wa CCM, je hii ni halali?
Mawazo yangu; kama CCM inaona iliruhusu mfumo wa demokrasia hapa nchini kimakosa basi ni vizuri wakae tena chini waamue upya kuufuta mfumo huo kama hauwafai kulikoni kuwanyanyasa watu ambao wanafanya shughuli zao kihalali. Ikifuta demokrasia sisi tusio kuwa na vyama ikitokea mtu anaikosoa serikali na akakamatwa tutajua wazi kavunja sheria kwasababu sheria za nchi haziruhusu mtu kuikosoa serikali kwa namna yoyote ile na tutajua ni stahili yake. Na kama watu watajitolea kudai haki zao kwa nguvu punde serikali inakuwa haiwajibiki vema kwa wananchi basi iwe wazi wanaamua kwa kujitoa muhanga kwa maana sheria hairuhusu watu kufanya hivyo, hapo inakuwa inaeleweka wazi ni kufa au kupona kuliko ilivyo sasa kwamba mtu anaruhusiwa halafu anaviziwa.
Mwenye uelewa sababu za CCM kuruhusu mfumo wa vyama vingi huku yenyewe inauchukia mfumo aniambie waliruhusu ili iweje?
 
Mfumo wa demokrasia hapa nchini ulianzishwa rasmi mwaka 1992 chini ya Rais Mwinyi akiwa ndiye mwenyekiti wa chama mapinduzi CCM, na ndio kilikuwa chama pekee cha siasa kabla ya hapo kutokana na mfumo wa siasa wa wakati huo.
Najua suala la maamuzi ya kuruhusu mfumo wa mabadiliko ya kisiasa kutoka ujamaa hadi demokrasia haukufanywa na Mwinyi pekee kama Rais bali ni maamuzi ya chama kizima cha CCM ambacho kwa wakati ule kilikuwa ndio serikali yenyewe ukiondoa suala la chama. Najua waliwaza mengi na kujiridhisha kuwa ni sahihi nchi kubadili mfumo wake wa kisiasa huku CCM ikijua wazi inaruhisu wapinzani dhidi yake,hilo lilikuwa ni jambo jema sana kwa nchi kupata watu wenye mitazamo tofauti ili kupata mwenye mawazo bora kwa wakati husika kuongoza nchi pamoja na chama chake.
Sasa swali langu ni hili; kama ccm ilijua wasi kwamba inaruhusu upinzani dhidi yake kama chama tawala na ikaruhusu, sasa kwanini leo inatumia nguvu nyingi kukandamiza upinzani tena bila hata sababu? Au ilitegemea licha ya kuruhusu upinzani ya kwamba wasingetokea watu wa kuwapinga kihija na mitazamo? Au walikurupuka bila kujua athari zake kwa upande wao? Kama walijua ni kwanini sasa watu wenye mawazo tofauti na wao wanatendewa mambo mabaya ili hali wako sahihi kufanya hivyo na hawajavunja sheria? Leo tunasikia habari za watu wengi kutekwa na ukifiatilia wengi wao ni watu wa vyama vya upinzani haijawahi kutokea katekwa mtu wa CCM. Kumeshuhudiwa mara nyingi shughuli za vyama vya upinzani zikizuiwa na vyombo vya dola na shughuli hizo ziko kihalali na hawavunji sheria yoyote, mambo kama hayo hawajawahi fanyiwa watu wa CCM, je hii ni halali?
Mawazo yangu; kama CCM inaona iliruhusu mfumo wa demokrasia hapa nchini kimakosa basi ni vizuri wakae tena chini waamue upya kuufuta mfumo huo kama hauwafai kulikoni kuwanyanyasa watu ambao wanafanya shughuli zao kihalali. Ikifuta demokrasia sisi tusio kuwa na vyama ikitokea mtu anaikosoa serikali na akakamatwa tutajua wazi kavunja sheria kwasababu sheria za nchi haziruhusu mtu kuikosoa serikali kwa namna yoyote ile na tutajua ni stahili yake. Na kama watu watajitolea kudai haki zao kwa nguvu punde serikali inakuwa haiwajibiki vema kwa wananchi basi iwe wazi wanaamua kwa kujitoa muhanga kwa maana sheria hairuhusu watu kufanya hivyo, hapo inakuwa inaeleweka wazi ni kufa au kupona kuliko ilivyo sasa kwamba mtu anaruhusiwa halafu anaviziwa.
Mwenye uelewa sababu za CCM kuruhusu mfumo wa vyama vingi huku yenyewe inauchukia mfumo aniambie waliruhusu ili iweje?
Usahihi ni kwamba mfumo wa vyama vingi ulirudishwa rasmi mwaka 1992 na siyo kuanzishwa, vyama vingi vilikuwepo kabla ya ccm kuzaliwa.

Sababu za mfumo kurudishwa ni mbinyo wa mabeberu na si vinginevyo, hutaki mfumo huo sahau kuhusu pesa za world bank na ÍMF.

Ccm waliitisha maoni fake yalioonyesha waliotowa maoni wengi walitaka chama kimoja lakini ulaghai wao haukufuwa dafu kwa mabeberu, condition yao ni vyama vingi na utawala bora ndio mtaelewana hapo ccm hawakuwa na jinsi na Nyerere ndio akashinikiza mfumo wa vyama vingi urudi rasmi.

Kwahiyo jibu lako kwa kifupi wazungu ndio waliorudisha huu mfumo siyo ccm hawajawahi kuukubali mfumo huu.
 
Usahihi ni kwamba mfumo wa vyama vingi ulirudishwa rasmi mwaka 1992 na siyo kuanzishwa, vyama vingi vilikuwepo kabla ya ccm kuzaliwa.

Sababu za mfumo kurudishwa ni mbinyo wa mabeberu na si vinginevyo, hutaki mfumo huo sahau kuhusu pesa za world bank na ÍMF.

Ccm waliitisha maoni fake yalioonyesha waliotowa maoni wengi walitaka chama kimoja lakini ulaghai wao haukufuwa dafu kwa mabeberu, condition yao ni vyama vingi na utawala bora ndio mtaelewana hapo ccm hawakuwa na jinsi na Nyerere ndio akashinikiza mfumo wa vyama vingi urudi rasmi.

Kwahiyo jibu lako kwa kifupi wazungu ndio waliorudisha huu mfumo siyo ccm hawajawahi kuukubali mfumo huu.
Upo Sahihi sana, Mwl Nyerere alipoona upepo wa mabadiliko ulikuwa unavuma kwa namna ya kuuondoa ujamaa haswa baada ya vita baridi kuibua ubepari na democracy kuwa washindi akaona bora ajing'atue na kupisha mfumo mpya ambao yeye hakuupenda wala kuuamini. Kwenye hotuba yake 1996 aliyoitoa Ottawa Canada alilalamika kwamba nchi za Africa zimelazimishwa kukopi demokrasia ya nchi za Magharibi na kwamba zikikataa basi zinanyimwa misaada, na kwamba inch yake ipo kwenye jaribio la mfumo mpya wa kibepari na demokrasia ya magharibi. Utaona kwamba Nyerere hakupenda ubepari wala demokrasia ya vyama vingi.

Kinachoendelea Tanzania kinafuata historia ya nchi nyingi za Africa ambazo hazikuwa na mpango wa kuikumbatia demokrasia tangu zipate Uhuru. Tena zikajitengenezea mfumo wa PAN AFRICANISM ambao kamwe haukuwa na maana ya kukuza demokrasia badala yake kujenga himaya za watawala wachache wa milele. Watawala ambao hawakupenda kukosolewa, kupingwa wala kutoka madarakani labda kwa mtutu wa bunduki. Fikiria akina Nyerere, Mobutu, Nkurumah, Sankara, Biya, Kaunda, Kenyatta, Obote, Bongo, Banda nk nk. Hao wote hapo hawakuwa na mpango wa demokrasia wala mpango wa kutoka madarakani kwa njia ya amani.

Sasa tunachokiona Tanzania na nchi za Afrika ni kuisigina demokrasia ya Magharibi ili iwe na sura ya kuwaweka viongozi madarakani kadri watakavyo. Ili viongozi waendelee kutawala lazima wakiuke misingi ya demokrasia ya Magharibi. Chaguzi lazima zifanyike kwa namna ya kuwaweka wao madarakani kwa kutumia njia haramu alizozitaja Mbunge wangu. Haki za binadamu zinazotiliwa mkazo kwenye demokrasia ya Magharibi hazina nafasi kwenye nchi za Africa, na ndio maana kwenye viwango vya kimataifa za kusimamia haki za binadamu ni nchi 10 tu za Africa ndio zimeonyesha kusimamia angalau nusu kwa mujibu wa UN. Vile vile mgawanyo wa madaraka kati ya mihimili ya nchi, yaani bunge, serikali na mahakama Tanzania na Africa haupo katika vitendo. Jaji mkuu anateuliwa na rais, waziri ni sehemu ya bunge, na bunge linaweza kutunga sheria za kutengua maamuzi ya mahakama. Haya yote maana yake demokrasia ya vyama vingi haina nafasi Tanzania na Africa. Badala yake imetengenezwa demokrasia ya kuhakikisha na kulinda utawala uliopo kwa gharama za matarajio ya umma.

Pasipo katiba mpya tusahau demokrasia ya vyama vingi.
 
Usahihi ni kwamba mfumo wa vyama vingi ulirudishwa rasmi mwaka 1992 na siyo kuanzishwa, vyama vingi vilikuwepo kabla ya ccm kuzaliwa.

Sababu za mfumo kurudishwa ni mbinyo wa mabeberu na si vinginevyo, hutaki mfumo huo sahau kuhusu pesa za world bank na ÍMF.

Ccm waliitisha maoni fake yalioonyesha waliotowa maoni wengi walitaka chama kimoja lakini ulaghai wao haukufuwa dafu kwa mabeberu, condition yao ni vyama vingi na utawala bora ndio mtaelewana hapo ccm hawakuwa na jinsi na Nyerere ndio akashinikiza mfumo wa vyama vingi urudi rasmi.

Kwahiyo jibu lako kwa kifupi wazungu ndio waliorudisha huu mfumo siyo ccm hawajawahi kuukubali mfumo huu.
Sasa kama suala ni kuogopa kunyimwa misaada si warudishe mfumo wa chama kimoja halafu wajenge uchumi wao kwa nchi yao kuliko kukubali mambo kishingoupande halafu wanaanza kunyanyasa watu na uhai wao? Wanakuwaje na jeuri ya kukandamiza haki za watu na wakati suala la kujenga uchumi imara hawawezi? Hii nguvu si wangewekeza kwenye mambo ya msingi kutwa kupenda kukopa tu, na watu unanyanyasa kuna faida gani?
 
Mfumo wa demokrasia hapa nchini ulianzishwa rasmi mwaka 1992 chini ya Rais Mwinyi akiwa ndiye mwenyekiti wa chama mapinduzi CCM, na ndio kilikuwa chama pekee cha siasa kabla ya hapo kutokana na mfumo wa siasa wa wakati huo.
Najua suala la maamuzi ya kuruhusu mfumo wa mabadiliko ya kisiasa kutoka ujamaa hadi demokrasia haukufanywa na Mwinyi pekee kama Rais bali ni maamuzi ya chama kizima cha CCM ambacho kwa wakati ule kilikuwa ndio serikali yenyewe ukiondoa suala la chama. Najua waliwaza mengi na kujiridhisha kuwa ni sahihi nchi kubadili mfumo wake wa kisiasa huku CCM ikijua wazi inaruhisu wapinzani dhidi yake,hilo lilikuwa ni jambo jema sana kwa nchi kupata watu wenye mitazamo tofauti ili kupata mwenye mawazo bora kwa wakati husika kuongoza nchi pamoja na chama chake.
Sasa swali langu ni hili; kama ccm ilijua wasi kwamba inaruhusu upinzani dhidi yake kama chama tawala na ikaruhusu, sasa kwanini leo inatumia nguvu nyingi kukandamiza upinzani tena bila hata sababu? Au ilitegemea licha ya kuruhusu upinzani ya kwamba wasingetokea watu wa kuwapinga kihija na mitazamo? Au walikurupuka bila kujua athari zake kwa upande wao? Kama walijua ni kwanini sasa watu wenye mawazo tofauti na wao wanatendewa mambo mabaya ili hali wako sahihi kufanya hivyo na hawajavunja sheria? Leo tunasikia habari za watu wengi kutekwa na ukifiatilia wengi wao ni watu wa vyama vya upinzani haijawahi kutokea katekwa mtu wa CCM. Kumeshuhudiwa mara nyingi shughuli za vyama vya upinzani zikizuiwa na vyombo vya dola na shughuli hizo ziko kihalali na hawavunji sheria yoyote, mambo kama hayo hawajawahi fanyiwa watu wa CCM, je hii ni halali?
Mawazo yangu; kama CCM inaona iliruhusu mfumo wa demokrasia hapa nchini kimakosa basi ni vizuri wakae tena chini waamue upya kuufuta mfumo huo kama hauwafai kulikoni kuwanyanyasa watu ambao wanafanya shughuli zao kihalali. Ikifuta demokrasia sisi tusio kuwa na vyama ikitokea mtu anaikosoa serikali na akakamatwa tutajua wazi kavunja sheria kwasababu sheria za nchi haziruhusu mtu kuikosoa serikali kwa namna yoyote ile na tutajua ni stahili yake. Na kama watu watajitolea kudai haki zao kwa nguvu punde serikali inakuwa haiwajibiki vema kwa wananchi basi iwe wazi wanaamua kwa kujitoa muhanga kwa maana sheria hairuhusu watu kufanya hivyo, hapo inakuwa inaeleweka wazi ni kufa au kupona kuliko ilivyo sasa kwamba mtu anaruhusiwa halafu anaviziwa.
Mwenye uelewa sababu za CCM kuruhusu mfumo wa vyama vingi huku yenyewe inauchukia mfumo aniambie waliruhusu ili iweje?
Kwanza kabisa, CCM haikuruhusu upinzani kwa kutaka.

Nyerere aliogopa sana kuona jinsi rafiki yake Nicolae Ceaucescu wa Romania alivyouawa na wananchi wake, akaogopa kilichotokea Romania kisitokee Tanzania.

Nyerere akawaambia CCM ni bora waanze kufanya mabadiliko wao wenyewe wasije kuyaacha mabadiliko yatokee bila kupangwa na CCM.

Tume ya Nyalali ikasema Watanzania asilimia 80 wanataka chama kimoja na asilimia 20 tu ndio wanaotaka vyama vingi, Nyerere akasema hata kama asilimia 20 wametaka vyama vingi, ni busara kuwasikiliza hao asilimia 20.

Kwa hiyo, kuweka muktadha vizuri tu, CCM hawakuruhusu kwa hiyari yao upinzani, walilazimika kuruhusu upinzani kutokana na geopolitics, muenendo wa siasa za dunia.
 
Ccm ni kama mwanamke alielazimishwa kuolewa na mtu tajiri ilhali yeye kuna kapuku anampenda.
Sawa atakua na huyo tajili ili jamii ione kaolewa na kaolewa na tajiri ila mapenzi yake yote yapo kwa kapuku.

Atamzubaisha mumewe tajiri kwa maneno na bashasha feki ila penzi analifaidi kapuku asie na uwezo wa kufika nae popote.
 
Kwanza kabisa, CCM haikuruhusu upinzani kwa kutaka.

Nyerere aliogopa sana kuona jinsi rafiki yake Nicolae Ceaucescu wa Romania alivyouawa na wananchi wake, akaogopa kilichotokea Romania kisitokee Tanzania.

Nyerere akawaambia CCM ni bora waanze kufanya mabadiliko wao wenyewe wasije kuyaacha mabadiliko yatokee bila kupangwa na CCM.

Tume ya Nyalali ikasema Watanzania asilimia 80 wanataka chama kimoja na asilimia 20 tu ndio wanaotaka vyama vingi, Nyerere akasema hata kama asilimia 20 wametaka vyama vingi, ni busara kuwasikiliza hao asilimia 20.

Kwa hiyo, kuweka muktadha vizuri tu, CCM hawakuruhusu kwa hiyari yao upinzani, walilazimika kuruhusu upinzani kutokana na geopolitics, muenendo wa siasa za dunia.
Ndio maana Nyerere analaumiwa kwa maamuzi yake ya kibinafsi.

Huu mfumo ni wake na hawezi kukwepa lawama kwa namna yoyote.
 
Kwanza kabisa, CCM haikuruhusu upinzani kwa kutaka.

Nyerere aliogopa sana kuona jinsi rafiki yake Nicolae Ceaucescu wa Romania alivyouawa na wananchi wake, akaogopa kilichotokea Romania kisitokee Tanzania.

Nyerere akawaambia CCM ni bora waanze kufanya mabadiliko wao wenyewe wasije kuyaacha mabadiliko yatokee bila kupangwa na CCM.

Tume ya Nyalali ikasema Watanzania asilimia 80 wanataka chama kimoja na asilimia 20 tu ndio wanaotaka vyama vingi, Nyerere akasema hata kama asilimia 20 wametaka vyama vingi, ni busara kuwasikiliza hao asilimia 20.

Kwa hiyo, kuweka muktadha vizuri tu, CCM hawakuruhusu kwa hiyari yao upinzani, walilazimika kuruhusu upinzani kutokana na geopolitics, muenendo wa siasa za dunia.
Ahsante sana ndugu yangu, kama ni hivyo wasiwe waoga wasimamie wanachokiamini na wanachokitaka sio kuruhusu au kukubali mambo kimtego ili wanyanyase watu. Kama wanauwezo wa kutuongoza milele waamue moja tu kusiwe na vyama vingi mimi binafsi nitawaelewa kuliko hali ilivyo sasa. Kama ni mabadiliko wasubiri raia wenyewe na sio vyama wataamua kwa gharama watakauoiona ni sawa, hapo ndipo CCM watujua madhara ya kukandamiza watu. Kwa sasa watu wakidai haki vinanyoshewa vidole vyama, kwahiyo hata kama madai ya raia wote ccm wanasimamia kuwa ni chama fulani kumbe ni shida ya watanzania wote bila kujali vyama.
 
Ndio maana Nyerere analaumiwa kwa maamuzi yake ya kibinafsi.

Huu mfumo ni wake na hawezi kukwepa lawama kwa namna yoyote.
Si maamuzi yake binafsi. Alielewa kuwa haya mabadiliko ni ya dunia nzima na ni bora kuyakubali na kuya control, vinginevyo, yangekuja machafuko.
 
Si maamuzi yake binafsi. Alielewa juwa haya mabadiliko ni ya dunia nzima na ni bora kuyakubali na kuya control, vinginevyo, yangekuja machafuko.
Hiyo kuyacontrol ndo shida inapoanzia hapo, wanayacontrol kwa hizi kutekana hovyo, kuuana na kutokubali kupingwa.
 
Ndio maana Nyerere analaumiwa kwa maamuzi yake ya kibinafsi.

Huu mfumo ni wake na hawezi kukwepa lawama kwa namna yoyote.
Alifanya kitu kimoja kibaya sana, leo hii raia wanaamini midomo yao iko kwenye vyama jambo ambalo linapelekea wachache wanukuliwe badala ya umma. Watu wanapotea kwasababu ya kusimama na raia kama watetezi wao. Wafute vyama vingi ili raia wajue namna ya kuzungumza na serikali na sio kuonea wachache
 
Mfumo wa demokrasia hapa nchini ulianzishwa rasmi mwaka 1992 chini ya Rais Mwinyi akiwa ndiye mwenyekiti wa chama mapinduzi CCM, na ndio kilikuwa chama pekee cha siasa kabla ya hapo kutokana na mfumo wa siasa wa wakati huo.
Najua suala la maamuzi ya kuruhusu mfumo wa mabadiliko ya kisiasa kutoka ujamaa hadi demokrasia haukufanywa na Mwinyi pekee kama Rais bali ni maamuzi ya chama kizima cha CCM ambacho kwa wakati ule kilikuwa ndio serikali yenyewe ukiondoa suala la chama. Najua waliwaza mengi na kujiridhisha kuwa ni sahihi nchi kubadili mfumo wake wa kisiasa huku CCM ikijua wazi inaruhisu wapinzani dhidi yake,hilo lilikuwa ni jambo jema sana kwa nchi kupata watu wenye mitazamo tofauti ili kupata mwenye mawazo bora kwa wakati husika kuongoza nchi pamoja na chama chake.
Sasa swali langu ni hili; kama ccm ilijua wasi kwamba inaruhusu upinzani dhidi yake kama chama tawala na ikaruhusu, sasa kwanini leo inatumia nguvu nyingi kukandamiza upinzani tena bila hata sababu? Au ilitegemea licha ya kuruhusu upinzani ya kwamba wasingetokea watu wa kuwapinga kihija na mitazamo? Au walikurupuka bila kujua athari zake kwa upande wao? Kama walijua ni kwanini sasa watu wenye mawazo tofauti na wao wanatendewa mambo mabaya ili hali wako sahihi kufanya hivyo na hawajavunja sheria? Leo tunasikia habari za watu wengi kutekwa na ukifiatilia wengi wao ni watu wa vyama vya upinzani haijawahi kutokea katekwa mtu wa CCM. Kumeshuhudiwa mara nyingi shughuli za vyama vya upinzani zikizuiwa na vyombo vya dola na shughuli hizo ziko kihalali na hawavunji sheria yoyote, mambo kama hayo hawajawahi fanyiwa watu wa CCM, je hii ni halali?
Mawazo yangu; kama CCM inaona iliruhusu mfumo wa demokrasia hapa nchini kimakosa basi ni vizuri wakae tena chini waamue upya kuufuta mfumo huo kama hauwafai kulikoni kuwanyanyasa watu ambao wanafanya shughuli zao kihalali. Ikifuta demokrasia sisi tusio kuwa na vyama ikitokea mtu anaikosoa serikali na akakamatwa tutajua wazi kavunja sheria kwasababu sheria za nchi haziruhusu mtu kuikosoa serikali kwa namna yoyote ile na tutajua ni stahili yake. Na kama watu watajitolea kudai haki zao kwa nguvu punde serikali inakuwa haiwajibiki vema kwa wananchi basi iwe wazi wanaamua kwa kujitoa muhanga kwa maana sheria hairuhusu watu kufanya hivyo, hapo inakuwa inaeleweka wazi ni kufa au kupona kuliko ilivyo sasa kwamba mtu anaruhusiwa halafu anaviziwa.
Mwenye uelewa sababu za CCM kuruhusu mfumo wa vyama vingi huku yenyewe inauchukia mfumo aniambie waliruhusu ili iweje?
Kwa uelewa wangu mdogo juu ya swala hili ni kwamba Ccm haijawahi kuamua kuanzisha mfumo wa vyama vingi kwenye hii nchi ila huu mfumo ulianza kwa lazima baada ya Russia kuanguka sisi kama nchi tukakosa option na sehemu ya kukimbilia na badala yake tukaangukia kwenye mikono ya nchi ambazo zinaapply mfumo wa democracy na masharti ndio yakawa hayo ili uweze kupata misaada kwenye hizo nchi lazima kuwe na democracy nchini kwako na ndio hapo kupelekea hiyo mifumo kuanza.

Kwahiyo Ccm haijawahi kuhutaji hayo mambo ya vyama vingi na pengine hata sisi kama nchi kwa wakati ule hatukua tayari kwa sehemu kubwa.

Ndio maana mimi kati ya vitu ambavyo sijawahi kuviamini kwenye hii nchi ni upinzani wa kweli coz vyama vyote ambavyo vilianzishwa huwa nahisi vilianzishwaga kimchongo ili kuwafanyia danganyia toto mabeberu so ili upinzani wa kweli utokee ni lazima damu changa ziingie kwenye system kwasababu zinakua hazina historia yoyote kuhusiana na mambo haya ila hawa wazee sijui kwakweli.
 
Alifanya kitu kimoja kibaya sana, leo hii raia wanaamini midomo yao iko kwenye vyama jambo ambalo linapelekea wachache wanukuliwe badala ya umma. Watu wanapotea kwasababu ya kusimama na raia kama watetezi wao. Wafute vyama vingi ili raia wajue namna ya kuzungumza na serikali na sio kuonea wachache
Ukiikosoa serikali utaonekana chadema, ukiisifia ni ccm na wapambe wa hivyo vyama watakuzonga ati uonekane ni mwanachama wao.
 
Huu mfumo wa demokrasia uliopo Tanzania ni hatari sana kwa maendeleo ya nchi hatuwezi kuendelea kama mfumo huu utaendelea kubaki hivi vinginevyo ni lazima wananchi waviweke pembeni vyama vyao wadai haki kama raia na sio vyama. CCM wanasimamia kuwa mambo yoyote yakisemwa kupitia viongozi wa vyama wanachukulia ni agenda za vyama ni sio madai au maoni ya wananchi. Ili ionekane wazi kuwa ni maoni au madai ya wananchi ni lazima wananchi wajifunze kuanzia sasa namna ya kujiwakilisha kwa serikali yao.
 
Back
Top Bottom