Mwenye nyumba anataka apake rangi kabla mpangaji hajahama, hii ni sawa?

Mwenye nyumba anataka apake rangi kabla mpangaji hajahama, hii ni sawa?

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
Baada ya muda mrefu kuishi kibahili bahili licha ya kuajiriwa taasisi yenye mshahara na posho si haba, Rafiki yangu kaweza kukamilisha nyumba yake.

Hapo majuzi alienda kumuaga mwenye nyumba kwamba nae amejenga na ni muda sasa umefika nae aende kuishi kwenye nyumba yake, Lengo lilikuwa ni kuaga kwa amani, mwenye nyumba alimpokea tu vizuri, akawa anampongeza na hata alipoomba aoneshwe picha za nyumba alimpongeza sana rafiki kwa kujenga nyumba nzuri kuzidi hata pale alipopanga, wakaagana vizuri tu na kumtakia kila la kheri.

Mwenye nyumba akamwambia siku ya kuondoka ikifika amwambie ili aje achukue funguo.

Sasa rafiki alivofika tu nyumbani, mwenye nyumba akamtumia sms kuwa anataka nyumba aipake rangi yote ndio ahame, hio nyumba amekaa miaka 6 na mwenye nyumba ajawah kupaka rangi, alipaka tu wakati anahamia, mkataba ulisema haruhusiwi kufanya chochote bila idhini ya mwenye nyumba hata kama ni kitasa.
 
Baada ya muda mrefu kuishi kibahili bahili licha ya kuajiriwa taasisi yenye mshahara + posho si haba, Rafiki yangu kaweza kukamilisha nyumba yake.


Hapo majuzi alienda kumuaga mwenye nyumba kwamba nae amejemga na ni muda sasa umefika nae aende kuishi kwenye nyumba yake, Lengo lilikuwa ni kuaga kwa amani, mwenye nyumba alimpokea tu vizuri, akawa anampongeza na hata alipoomba aoneshwe picha za nyumba alimpongeza sana rafiki kwa kujenga nyumba nzuri kuzidi hata pale alipopanga, wakaagana vizuri tu na kumtakia kila la kheri,

Mwenye nyumba akamwambia siku ya kuondoka ikifika amwambie ili aje achukue funguo,

sasa rafiki alivofika tu nyumbani, mwenye nyumba akamtumia sms kuwa anataka nyumba aipake rangi yote ndio ahame, hio nyumba amekaa miaka 6 na mwenye nyumba ajawah kupaka rangi, alipaka tu wakati anahamia, mkataba ulisema haruhusiwi kufanya chochote bila idhini ya mwenye nyumba hata kma ni kitass
Kama hawakuandikishiana asipake. but in good spirit apake na amwambie wazi kuwa anapaka kwa kuwa amekuwa baba mwenye nyumba mwema kwake, japo haiko kimkataba
 
Kupaka rangi inakua kwenye mkataba. Mfano mimi kuna nyumba niliingia mwenye nyumba akapaka rangi kila pande ikapendezaa ila jiko la gesi likachakaza sehemu.

Siku ya kuhama nilimwambia kweli nahamia kwangu. Ila ilibidi nipige rangi as per mkataba
 
Baada ya muda mrefu kuishi kibahili bahili licha ya kuajiriwa taasisi yenye mshahara + posho si haba, Rafiki yangu kaweza kukamilisha nyumba yake.


Hapo majuzi alienda kumuaga mwenye nyumba kwamba nae amejemga na ni muda sasa umefika nae aende kuishi kwenye nyumba yake, Lengo lilikuwa ni kuaga kwa amani, mwenye nyumba alimpokea tu vizuri, akawa anampongeza na hata alipoomba aoneshwe picha za nyumba alimpongeza sana rafiki kwa kujenga nyumba nzuri kuzidi hata pale alipopanga, wakaagana vizuri tu na kumtakia kila la kheri,

Mwenye nyumba akamwambia siku ya kuondoka ikifika amwambie ili aje achukue funguo,

sasa rafiki alivofika tu nyumbani, mwenye nyumba akamtumia sms kuwa anataka nyumba aipake rangi yote ndio ahame, hio nyumba amekaa miaka 6 na mwenye nyumba ajawah kupaka rangi, alipaka tu wakati anahamia, mkataba ulisema haruhusiwi kufanya chochote bila idhini ya mwenye nyumba hata kma ni kitass
Hup ujinga mm nilikataa,angekuwa amevunja milango au kuharibu structure ya nyumba ndo unahaki ya kumwambia arekebishe ila siyo rangi au choo kujaa,maana hivo ni vitu perishable ndani ya nyumba na ndo maana tunalipia kodi hatukai bure,hizo ni service za mwenyenyumba na anazicover kwnye kodi hususan atakapokuja mpangaji mpya atamchaji hela ya kupaka rangi,mm mwnye nyumba wakati nahama alitaka kuniletea hivo nilimtoa baru,mm nikipaka rangi yy arafanya kazi gani sasa au anadhan kodi anayopokea ni ya vikoba,lazime aendelee kufanya uboreshaji ktk nyumba yake ili iendelee kuvutia wapangaji wengine,siyo mm nimpakie rangi?? Kumwambia mpangaji apake rangi ni sawa na kukodi tax au uber halafu mwisho wa safari dereva akwambie upite sheli uweke na mafuta uliyotumia wakati umeshamlipa nauli yake!!
 
Baada ya muda mrefu kuishi kibahili bahili licha ya kuajiriwa taasisi yenye mshahara + posho si haba, Rafiki yangu kaweza kukamilisha nyumba yake.


Hapo majuzi alienda kumuaga mwenye nyumba kwamba nae amejemga na ni muda sasa umefika nae aende kuishi kwenye nyumba yake, Lengo lilikuwa ni kuaga kwa amani, mwenye nyumba alimpokea tu vizuri, akawa anampongeza na hata alipoomba aoneshwe picha za nyumba alimpongeza sana rafiki kwa kujenga nyumba nzuri kuzidi hata pale alipopanga, wakaagana vizuri tu na kumtakia kila la kheri,

Mwenye nyumba akamwambia siku ya kuondoka ikifika amwambie ili aje achukue funguo,

sasa rafiki alivofika tu nyumbani, mwenye nyumba akamtumia sms kuwa anataka nyumba aipake rangi yote ndio ahame, hio nyumba amekaa miaka 6 na mwenye nyumba ajawah kupaka rangi, alipaka tu wakati anahamia, mkataba ulisema haruhusiwi kufanya chochote bila idhini ya mwenye nyumba hata kma ni kitass
Aoneshwe mkataba, kama mwenye nyumba amepoteza nakala yake. Walikubaliana nini?
 
maybe kuepuka ugomvi paka tu kadiria gharama ukiona unazimudu basi paka ila mwambie siyo kazi yako kuifanyia maboresho nyumba yake ndo maana unalipa kodi
Alafu mwanaume unakosaje kifua?kwani lazima useme nahama kwasababu nimejenga?
 
Ni sawa mimi kwangu nakagua hadi vitasa, switch za Umeme, koki za maji , shower. Ukuta umetoboatoboa utarekebisha. Rangi ya ukutani nakagua kuna jamaa nilimpangisha walikuwa na mtoto alifanya ukuta kama ubao wake wa kujifunzia

Mimi nyumbani yangu ikiwa kama nilivyomkabidhi alivyoingia.

Kujenga ni gharama sana na ni biashara inayolipa kidogokidogo kwa hizi nyumbani za kuishi.

Umepanga kwenye nyumbani ili kuishi na sio kufanya uharibifu na uchafuzi wa rangi
 
Ni sawa mimi kwangu nakagua hadi vitasa, switch za Umeme, koki za maji , shower. Ukuta umetoboatoboa utarekebisha. Rangi ya ukutani nakagua kuna jamaa nilimpangisha walikuwa na mtoto alifanya ukuta kama ubao wake wa kujifunzia

Mimi nyumbani yangu ikiwa kama nilivyomkabidhi alivyoingia.

Kujenga ni gharama sana na ni biashara inayolipa kidogokidogo kwa hizi nyumbani za kuishi.

Umepanga kwenye nyumbani ili kuishi na sio kufanya uharibifu na uchafuzi wa rangi
Unataka rangi ibaki mpyaa bhasi usipangisheee hiyo nyumbaa...!!
 
Hakuna kulipwa iyo ndio hasara ya biashara yake lazima apake rangi mwenyewe maana ile nyumba sio mali yako.
 
Unataka rangi ibaki mpyaa bhasi usipangisheee hiyo nyumbaa...!!
Kwa taarifa yako rangi za nyumba za siku hizi hazichakai, ni uchafuzi tu unafanyika either makusudi au watoto.
Kuna jamaa nilimpangisha zaidi ya miaka 4 akaja kuhama kanikabidhi nyumba Safi kama nilivyomkabidhi sana sana sebuleni walikuwa ametoboa sehemu ya kuweka TV akaniambia nitafute Fundi azibe nikamwambia aachane napo.
Rangi za nyumba Kwa ndani zinaharibiwa na watu wenyewe au maji ndio maana sehemu zenye maji hususani jikoni na chooni tunaweka tiles.
Unapanga nyumba ya mtu mwaka tu unaichakaza utadhani umeishi miaka 10.
Kwangu Mpangaji labda atoroke ila kama amefanya uharibifu wa rangi na vitu lazima alipe kabla ya kuhama
 
Hup ujinga mm nilikataa,angekuwa amevunja milango au kuharibu structure ya nyumba ndo unahaki ya kumwambia arekebishe ila siyo rangi au choo kujaa,maana hivo ni vitu perishable ndani ya nyumba na ndo maana tunalipia kodi hatukai bure,hizo ni service za mwenyenyumba na anazicover kwnye kodi hususan atakapokuja mpangaji mpya atamchaji hela ya kupaka rangi,mm mwnye nyumba wakati nahama alitaka kuniletea hivo nilimtoa baru,mm nikipaka rangi yy arafanya kazi gani sasa au anadhan kodi anayopokea ni ya vikoba,lazime aendelee kufanya uboreshaji ktk nyumba yake ili iendelee kuvutia wapangaji wengine,siyo mm nimpakie rangi?? Kumwambia mpangaji apake rangi ni sawa na kukodi tax au uber halafu mwisho wa safari dereva akwambie upite sheli uweke na mafuta uliyotumia wakati umeshamlipa nauli yake!!
Hii ni sawa kabisa lazima mwenye nyumba afanye marekebisho bila hivyo itakuwa kama ni gari la abiria mnasafiri afu likiharibila eti abiria ndo atoe hela ya kutengeneza gari haiingii akilini kabisa
 
Ni sawa mimi kwangu nakagua hadi vitasa, switch za Umeme, koki za maji , shower. Ukuta umetoboatoboa utarekebisha. Rangi ya ukutani nakagua kuna jamaa nilimpangisha walikuwa na mtoto alifanya ukuta kama ubao wake wa kujifunzia

Mimi nyumbani yangu ikiwa kama nilivyomkabidhi alivyoingia.

Kujenga ni gharama sana na ni biashara inayolipa kidogokidogo kwa hizi nyumbani za kuishi.

Umepanga kwenye nyumbani ili kuishi na sio kufanya uharibifu na uchafuzi wa rangi
Hivyo ndiyo inapaswa kuwa. Siasa za ujamaa na kufanya umiliki wa nyumba ni uovu vimefanya tuone ni haki yetu kuharibu nyumba tunazopanga. Kuna wanaong'oa bulb kwa mayai waliweka wao baada ya waliyoikuta kuungua.
Kutaifisha majumba ilihalalishwa kwa maelezo kuwa si haki kuingiza kipato bila ya kufanya kazi. Ni matamko ya Mwalimu haya.
 
Unapaka tuu Rangi kama nyumba uliikuta amepaka rangi unawezaje kumuachia huku ikiwa imechorwa chorwa na watoto muda mwingine msiangalie sana mkataba mnaenda kupata mikosi bure kwa kupaka rangi ya maji na fundi ni wako shida ipo wapi ...
 
Back
Top Bottom