Je huyu mtu mwenye kinga imara ya mwili na tayari ameambukizwa akipima atapatikana na maambukizi? (Pamoja na kwamba hana dalili yoyote)
HAYA MAELEZO NILIKUWA SIJAELEWA VIZURI SWALI,LAKINI KWA KUWA NAYO NI MAELEZO MAZURI YA KUTOA ELIMU SITAYAFUTA,ILA NILIKUWA NAMUONGELEA MTU ASIYEWEZA KUAMBUKIZWA UKIMWI KUTOKANA NA KINGA YAKE IMARA YA KUWEZA KUZUIA MAAMBUKIZI,NA UTAFITI ULIOFANYIKA NA UNAOFANYIKA KUJARIBU KUTUMIA CELL ZA WATU WASIOAMBUKIZWA UKIMWI NA KUZIPANDIKIZA KWA WENGINE ILI IWE KAMA CHANJO YA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA UKIMWI
MAJIBU YA SWALI HUSIKA NIMEYAWEKA CHINI,SAMAHANI KWA USUMBUFU WASOMAJI
hao wenye kinga dhidi ya maambukizi ya UKIMWI kamwe hawezi kuambukizwa kabisa, na wanasayansi walitaka kufanya upandikizaji wa cell za watu hawa kwa watu wengine ili nao wajikinge na maambukizi ya ukimwi,
tatizo likawa hivi, mfano mimi upandikizaji wa stem cell,T cell za hao watu wasioweza kuambukizwa inaleta shida kwa kuwa cell zangu mimi zinaona cell nilizopandikiziwa ni adui na zinaanza kuzishambulia na kuziua, na hapo ndipo walishindwa,
lakini kwa mfano yule mtu aliyepandikiziwa seli za bon marrow wa huko marekani MISSISSIP wakati wakimtibu na kansa, iliwezekana tu kwa sababu yeye ugonjwa wake ulikuwa umeua mfumo wake wote wa ulinzi(hakuwa na immune system) na hivyo hakukuwa na kizuizi ndani ya mwili wake cha kushambulia upandikizaji wa seli kutoka kwa mtu mwigine na watu wanaopandikizwa seli za wengine asilimia 20% wanakufa baada ya muda mfupi kati ya miezi na miaka 3 na ndio maana wanasayansi wakaona hii njia haifai,
hata hivyo utafiti unao-onekana kuondoa tatizo hili la mfumo wa ulinzi wa ndani kushambulia upandikizaji wa seli toka kwa mtu mwingine ni kwamba kwa sasa wanachokifanyia nikuchukua cell za mtu huyohuyo aneugua ukimwi wanazitoa na kuzifanyia mabadiliko ya kuhimili na kuzuia maambukizi,wakishazipandikiza kwa mtu yuleyule hazishambuliwi na mfumo wa ndani wa ulinzi kwa kuwa seli hizo zinafanana na za ndani japo kidogo zimebadilishwa,
lakini wakati huohuo mtu anatakiwa kuendelea kutumia ARV wakati hizi cell zinajijenga kwenye mfumo ili kuzuia zisiambukizwe wakati hazijajiimarisha na baadae hizi seli zina uwezo wa kuua vurusi vyenyewe na cell zenye virusi
lakini na hapa pia tatizo limekuwa ni kwamba hizi seli zinazopandikizwa haziwezi kuua virusi vyote na kuua cell zote zilizoambukizwa,lakini ni hatua nzuri zaidi iliyoikiwa.
NADHANI KWA MAELEZO HAYA MAFUPI UMENIELEWA.