Uchaguzi 2020 Mwenye ushahidi wa Dkt. Magufuli akimtaja Tundu Lissu kwenye kampeni zake tangu zilipoanza atuwekee hapa

Dam55

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2015
Posts
5,641
Reaction score
11,958
Tunashuhudia kampeni za mgombea urais kupitia CHADEMA ndugu Tundu Lissu kila anapopanda jukwaani lazima atamtaja Magufuli kwa jambo lolote lile kwa kifupi kipaumbele cha kwanza kwenye hotuba za Tundu Lissu ni Dkt. Magufuli.

Sasa tunaomba mwenye ushahidi wa JPM akimtaja Tundu Lissu mahala popote pale kwenye kampeni zake basi atuwekee hapa.

Naamini humu JF kuna watu wenye akili kubwa wanaweza kuwa na ushahidi watusaidie hapa.
 
Magufuli ni Rais anayetetea kiti lazima atajwe si dhambi hata kidogo.

Pili mgombea wa CCM anaposema kuna mtu ametumwa kutoka kwa mabeberu na kibaraka kwa maoni yake, huwa anammaanisha nani?!
 
Lissu anasema kuwa maendeleo yapatikane kwa watu wote bila ubaguzi wala kutisha watu eti wasipomletea wagombea wa chama chake hawatapata maendeleo. Sasa kwa muktadha huu unataka aache kumtaja huyo mbaguzi?
Aliyetaifisha mali za watu ni nani? Sasa asitajwe?

Magufuli anaposema kuwa wapo wenye uraia wa nchi nyingine huwa anamtaja nani?
 
Mama Samia anavyosema askari wao hawawezi kumkosa mtu kwa risasi tatu anamaanisha nani?
 

ukimkemea shetani lazima umtaje wazi wazi
 
Nitajie mgombea Urais anayetokea Singida maeneo ya Ikungi nami nitakutajia unachotaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…