Uchaguzi 2020 Mwenyekiti CCM MARA: Wasaliti na Watoa Rushwa Hawana nafasi ndani ya CCM

Uchaguzi 2020 Mwenyekiti CCM MARA: Wasaliti na Watoa Rushwa Hawana nafasi ndani ya CCM

Naona safari yake kisiasa ndiyo imeanza kuzama kwenye ziwa Victoria
Yuko right
Huwezi kumuamini ng'ombe alie katwa mkia.. Hata mke asie mwaminifu kwenye ndoa. Hafai kuolewa
 
Kuna siku nilimkuta pale Dodoma hotel siitaji kwa jina Ila alikuwa amelewa chakali hadi anaporomosha kikurya tu pale.
Habari hizi zimfikie yule mkurya anaelewa na kujikojolea huko ukonga dar,mkurya anaekula chips kiepe
 
Hakuna cha kupelekwa alikimbia dsm baada kugundua kwa wapiga kura wake wamebaini tabia zake za ulevi na wakamwambia ukweli kuwa asijisumbue kugombea.
Huyo namba 3 ana ugomvi binafsi na mtia nia. Hana ubavu wa kumkata maana kapelekwa pale kimkakati
 
Wacha kudanganya watu wewe hata aibu huoni? Waitara ajipange kuvuta kokoro hapo mwaroni
Hayupo wa kumshinda Heche zaidi ya Waitara ,pengine Kiboye kachoka kazi ya umwenyekiti na anataka kuhamia upinzani
 
Akiongea leo na UVCCM eneo la Bunda mkoani Mara, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara Ndugu Samwel Kiboye ALMAARUFU kama namba Tatu, amsema kwamba, "Mtu yeyote msaliti hawezi kuaminika. Huyo mtu kuna siku atakusaliti na wewe akipata mwenye dau kubwa, wauza nafsi zao, na watoa rushwa ndani ya CCM hawana nafasi. Tutapitia mchakato mzima, na hapa mkoani Mara tuna taarifa za waliotoa rushwa. Tutawakata. Narudia, TUTAWAKATA. wasijidanganye kwamba wana vyeo. hivyo vyeo ni via chama dola CCM, na CCM imekataa Rushwa"

Nadhani jiwe limerushwa gizani. Kuna watu litawapata
Huyu mwenyekiti kaandaa safu yake pengine ataenda kutengeneza tuhuma feki apate kisingizio cha kuwaengua washindi wa kura za maoni, huo ujinga ndiyo huwafanya wananchi kuichukia CCM
 
Mlevi na no.3 wote hamna uhakika na nani utakuwa mgombea suburini Siku atakavyoamka babu yake bashite!
 
Kiboye ni pandikizi, CCM wamuangalie sana.
Karibu mkoa mzima unashikiliwa na upinzani zaidi ya miaka 10 sasa, alafu badala ya kuleta mikakati yakuurejesha CCM, anaweletea mambo ya kike na wao wanamuangalia tu?
 
Huyo mwenyekiti si ndiyo yule alikataa phd hataki wasomi, nadhani Akili zake zitakuwa finyu sana
 
Kiboye aaache Uadui wa Kikabila kwa Waitara, anafanya biffu la kizamani sana huyu Namba 3 ajiangalie Na.1 asije kumla kichwa yeye
Hakuna cha bifu yeye kama mwenyekiti ana wajibu wa kusimamia maadili ndani ya chama.

Waitara anashutumiwa kutoa takrima hivyo lazima amkate tu
 
Kiboye ni pandikizi, CCM wamuangalie sana.
Karibu mkoa mzima unashikiliwa na upinzani zaidi ya miaka 10 sasa, alafu badala ya kuleta mikakati yakuurejesha CCM, anaweletea mambo ya kike na wao wanamuangalia tu?
Mwenyekiti wa CCM wenu huko mara aweza kuwa ndiyo mwenyekiti wa hovyo kuliko wenyeviti wote wa CCM mkoa ingawa mwenyekiti wa Kinondoni na yeye alitoa kituko kama hicho, huu ujinga wa kutumia uchunguzi kupika tuhuma kutengeneza zengwe ili majina yakatwe CCM Dodoma utaisha lini? mbinu za hovyo kabsa
 
Hakuna cha bifu yeye kama mwenyekiti ana wajibu wa kusimamia maadili ndani ya chama.

Waitara anashutumiwa kutoa takrima hivyo lazima amkate tu
Atende haki kama kweli katoa pesa aweke ushahidi usio na shaka kwani waitara ni mtoa Rushwa hata ukonga aligawa Rushwa akapora ushindi kwa njia haramu, asije kuwaonea wengine kwa mgongo wa waitara ambaye Dodoma anasubiriwa kupewa jimbo kwani mwenyekiti wa CCM Taifa hawezi kusiliza chochote hata wakienda na ushahidi wa video baada ya Bashite chaguo la mtukufu ni waitara sasa
 
Atende haki kama kweli katoa pesa aweke ushahidi usio na shaka kwani waitara ni mtoa Rushwa hata ukonga aligawa Rushwa akapora ushindi kwa njia haramu, asije kuwaonea wengine kwa mgongo wa waitara ambaye Dodoma anasubiriwa kupewa jimbo kwani mwenyekiti wa CCM Taifa hawezi kusiliza chochote hata wakienda na ushahidi wa video baada ya Bashite chaguo la mtukufu ni waitara sasa
Ninavyo mjua Namba tatu lazima atahakikisha Waitara anakatwa tu
 
Chunguzeni sana matokeo ya Jimbo la Rorya hasa walioshika namba 1 na 2 kwenye uchaguzi. Kulikuwa na mchezo mchafu sana.
 
Huyo ndio haswa mlengwa. Kutachimbika. Ila huyo namba tatu hana ubavu wa kukata mtu ni maneno tu yanamtoka baada ya jamaa kupindua meza.
Naona mnaongea kwa mafumbo zaidi wakati hapa Jukwaani kila kitu huwekwa hadharani. Btw huyo mlevi ni nani?
 
Mjumbe
B303D70F-05DE-40CC-88CC-5E8587D27A1A.jpeg
 
Back
Top Bottom