Mwenyekiti CCM Moshi Mjini atumia msiba kuwashambulia waliobwagwa kura za maoni 2020

Mwenyekiti CCM Moshi Mjini atumia msiba kuwashambulia waliobwagwa kura za maoni 2020

Fred Mwakitundu

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2018
Posts
227
Reaction score
382
Msiba wa kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Shambe Sagafu aliyefariki mwanzoni mwa wiki ,uligeuka kuwa uwanja wa siasa baada ya mwenyekiti wa chama hicho Moshi Mjini, Alhaj Omar Amin Shamba kuwashambulia kwa maneno makali baadhi ya makada wa Chama hicho waliojitosa kuomba kuteuliwa na chama hicho kuwania nafasi ya ubunge Jimbo la Moshi Mjini mwaka 2020.

Tukio hilo lilitokea muda mfupi baada ya mazishi ya Shambe wakati mwenyekiti huyo akitoa salama za chama nyumbani kwa marehemu eneo la majengo tukio ambalo liliugeuza msiba huo kama uwanja wa siasa huku baadhi ya waombolezaji wakikosoa maneno hayo wakidai hayakuwa pahala pake .

Lakini habari kutoka kwenye msiba huo zinadai kuwa,Mzee Shamba kabla ya kuwashambulia makada hoa alianza kueleza uhusiano wake na marehemu akidai hakuwa na uhusiano naye mzuri na walifikia hatua ya kutokusalimiana lakini akasema miezi mitatu kabla ya kifo cha marehemu wawili hao waliombana msamaha na maisha yakaendelea japo hata hilo halikuwafurahisha waombolezaji.

Inaelezwa baada ya kutamka maneno hayo akawageukia makada hao na kudai baada ya majina yao kukatwa na ngazi za juu za uamuzi za chama baadhi yao walimnunia wakiamini amehusika kuyakata majina hayo na kuhitimisha kwa kuwambia siasa siyo uhasama maneno ambayo yalimwamsha mmoja wa makada waliokuwa sehemu ya watia nia Ibrahim Shayo maarufu kama Ibra Line .

Ibra line kwa upande wake akapiga kijembe na kuwataka baadhi ya wazee kujitathimini na kuchagua maneno na sehemu ya kuyasemea akiamini kuwa mzee Shamba alikosea kutamka maneno yale kwenye mkusanyiko wa watu waliojawa na majonzi kauli ambayo iliwaibua watu wengi na kuanza kushangilia.

Shayo alisema Mzee Shamba hakuwa na sababu yoyote kusema kuhusu msuguano wake na maheremu kwani yalikuwa ni maneno ya kuendelea kuitia simanzi familia yake na ndugu na jamaa walioshiriki tukio la kumstiri ndugu yao.

Pamoja na hayo,Ibra Line kama anavyofahamika na wengi aliipa faraja familia ya marehemu Shambe baada ya kubeba jukumu la kuwasomesha watoto wawili wa marehemu kwenye moja ya shule anazozimiliki.


Kazi iendeleee
 
Siasa za Moshi zinafanana sana na siasa za Kenya!

Kwenye msiba wa Mengi walimtaka Makonda amuombe msamaha Mbowe.

Baba Keegan akagoma!
 
Msiba wa kada wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Shambe Sagafu aliyefariki mwanzoni mwa wiki ,uligeuka kuwa uwanja wa siasa baada ya mwenyekiti wa Chama hicho Moshi Mjini,Alhaj Omar Amin Shamba kuwashambulia kwa maneno makali baadhi ya makada wa Chama hicho waliojitosa kuomba kuteuliwa na chama hicho kuwania nafasi ya ubunge jimbo la Moshi Mjini mwaka 2020.

Tukio hilo lilitokea muda mfupi baada ya mazishi ya Shambe wakati mwenyekiti huyo akitoa salama za chama nyumbani kwa marehemu eneo la majengo tukio ambalo liliugeuza msiba huo kama uwanja wa siasa huku baadhi ya waombolezaji wakikosoa maneno hayo wakidai hayakuwa pahala pake .

Lakini habari kutoka kwenye msiba huo zinadai kuwa,Mzee Shamba kabla ya kuwashambulia makada hoa alianza kueleza uhusiano wake na marehemu akidai hakuwa na uhusiano naye mzuri na walifikia hatua ya kutokusalimiana lakini akasema miezi mitatu kabla ya kifo cha marehemu wawili hao waliombana msamaha na maisha yakaendelea japo hata hilo halikuwafurahisha waombolezaji.

Inaelezwa baada ya kutamka maneno hayo akawageukia makada hao na kudai baada ya majina yao kukatwa na ngazi za juu za uamuzi za chama baadhi yao walimnunia wakiamini amehusika kuyakata majina hayo na kuhitimisha kwa kuwambia siasa siyo uhasama maneno ambayo yalimwamsha mmoja wa makada waliokuwa sehemu ya watia nia Ibrahim Shayo maarufu kama Ibra Line .

Ibra line kwa upande wake akapiga kijembe na kuwataka baadhi ya wazee kujitathimini na kuchagua maneno na sehemu ya kuyasemea akiamini kuwa mzee Shamba alikosea kutamka maneno yale kwenye mkusanyiko wa watu waliojawa na majonzi kauli ambayo iliwaibua watu wengi na kuanza kushangilia.

Shayo alisema Mzee Shamba hakuwa na sababu yoyote kusema kuhusu msuguano wake na maheremu kwani yalikuwa ni maneno ya kuendelea kuitia simanzi familia yake na ndugu na jamaa walioshiriki tukio la kumstiri ndugu yao.

Pamoja na hayo,Ibra Line kama anavyofahamika na wengi aliipa faraja familia ya marehemu Shambe baada ya kubeba jukumu la kuwasomesha watoto wawili wa marehemu kwenye moja ya shule anazozimiliki.


Kazi iendeleee
[emoji871]Wewe umeripoti habari ki-Chawa zaidi.

[emoji871]Msibani pia ni sehemu sahihi ya kukosoana na kuombana misamaha kwa wanajamii pale inapobidi.

[emoji871]Na ndio maana jamii huwa inaulizwa kama kuna mtu alikuwa Mdai au Mdaiwa wa marehemu,ili kuwekana sawa.

[emoji871]Jifunzeni kwa Wakenya hapo jirani.

[emoji871]Huyo Ibra Line ni kama vile alipatwa na jiwe la gizani.ndio maana alitumia ukwasi wake kwa taharuki.
Anaendekeza makundi bado.
 
Hakuna "Mwenyekiti wa CCM wa Moshi Mjini" bali kuna "Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi".

Wilaya ya Moshi ina DC mmoja, Halmashauri 3:

1.Halmashauri ya Wilaya ya Moshi,

2. Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na;

3. Halmashauri ya Mji Mdogo wa Himo.
 
Hakuna "Mwenyekiti wa CCM wa Moshi Mjini" bali kuna "Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi".

Wilaya ya Moshi ina DC mmoja, Halmashauri 3:

1.Halmashauri ya Wilaya ya Moshi,

2. Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na;

3. Halmashauri ya Mji Mdogo wa Himo.
Asante sana
 
Hivi kuna Moshi Mjini na Moshi Vijijini?
Hakuna "Mwenyekiti wa CCM wa Moshi Mjini" bali kuna "Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi".

Wilaya ya Moshi ina DC mmoja, Halmashauri 3:

1.Halmashauri ya Wilaya ya Moshi,

2. Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na;

3. Halmashauri ya Mji Mdogo wa Himo.
 
Hakuna "Mwenyekiti wa CCM wa Moshi Mjini" bali kuna "Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi".

Wilaya ya Moshi ina DC mmoja, Halmashauri 3:

1.Halmashauri ya Wilaya ya Moshi,

2. Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na;

3. Halmashauri ya Mji Mdogo wa Himo.
nani boss wa halmashauri mji mdogo himo?
 
Hakuna "Mwenyekiti wa CCM wa Moshi Mjini" bali kuna "Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Moshi".

Wilaya ya Moshi ina DC mmoja, Halmashauri 3:

1.Halmashauri ya Wilaya ya Moshi,

2. Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na;

3. Halmashauri ya Mji Mdogo wa Himo.
Mji wa Himo una halmshauri yake?
 
Hivi kuna Moshi Mjini na Moshi Vijijini?
Kuna Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini na ina Mkurugenzi wake na madiwani wake. Hii ina majimbo ya Moshi Vijijini na Vunjo. Na ndani yake kuna Mamlaka ya Mji Mdogo wa Himo.

Kuna Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na ina Mkurugenzi wake na madiwani.Hii ina jimbo moja la Moshi Mjini

Ila Wilaya ni Moshi. Wilaya ya Moshi ni eneo lote la Halmashauri ya Wilaya ya Moshi na Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, na mkuu wa Wilaya ni mmoja, ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Moshi.
 
Swali zuri maana huduma kubwa za Serikali utaambiwa hadi Moshi mjini iwe za kiwilaya au mahakama Himo ipo ipo tu.
Kwa mujibu wa sheria, Mamlaka za Miji midogo zipo chini ya Halmashauri ya Wilaya husika. Kwa hiyo, mambo mengi hufanyika wilayani na hata pia kwa yale maamuzi ambayo yatafanywa na Mamlaka za Miji Midogo ni sharti yapate ruhusa ya Halmashauri ya Wilaya husika.

Mfano, Mamlaka za Miji Midogo ikipitisha sheria ndogo ni sharti rasimu ya sheria hizo ziende Halmashauri ya Wilaya, zipitiwe na kutolewa maamuzi kama zinafaa au laa.
 
Kwa mujibu wa sheria, Mamlaka za Miji midogo zipo chini ya Halmashauri ya Wilaya husika. Kwa hiyo, mambo mengi hufanyika wilayani na hata pia kwa yale maamuzi ambayo yatafanywa na Mamlaka za Miji Midogo ni sharti yapate ruhusa ya Halmashauri ya Wilaya husika.

Mfano, Mamlaka za Miji Midogo ikipitisha sheria ndogo ni sharti rasimu ya sheria hizo ziende Halmashauri ya Wilaya, zipitiwe na kutolewa maamuzi kama zinafaa au laa.
Sawa vizuri sasa kama mamlaka ya miji midogo ni lazima ziende Wilayani na Himo ipo w/moshi vijijini kwa nini mambo yake yote yapo Moshi mjini na wakati ni Wilaya mbili tofauti? Ofisi ya mkuu wa wilaya ya moshi vijijini ipo wapi?
 
Sawa vizuri sasa kama mamlaka ya miji midogo ni lazima ziende Wilayani na Himo ipo w/moshi vijijini kwa nini mambo yake yote yapo Moshi mjini na wakati ni Wilaya mbili tofauti? Ofisi ya mkuu wa wilaya ya moshi vijijini ipo wapi?
Ofisi zote za Halmashauri zote ikiwemo ofisi za vyama zipo Moshi Mjini.

Moshi Mjini siyo Wilaya bali ni Halmashauri.
 
Tofautisha mamlaka ya Mji Mdogo wa Himo

Tofautisha Halmashauri ya Wilaya ya Moshi(MDC)

Tofautisha Halmashauri ya Manispaa ya Moshi(MMC)

Kiutawala Mkuu wa wilaya ni Mmoja ila wakurugenzi ni wawili kwa maana na Manispaa ya Moshi na Moshi DC
 
Back
Top Bottom