Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga, Rajabu Abdulrahman Abdallah, amesema wanasiasa wa vyama vya upinzani hawana cha kuwaeleza wananchi juu ya kile walichokifanya, na kwamba wanafaa kupuuzwa.
Badala yake, amewataka wananchi wamuunge mkono Rais Samia Suluhu Hassan.
Rajabu ameyasema hayo akiwa wilayani Lushoto, mkoani Tanga, katika ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo, sambamba na kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 48 ya CCM yanayotarajiwa kufanyika siku chache zijazo.
Soma Pia: Tanga: Matukio Yanayojiri Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Amesema kila mtu ameshuhudia jinsi Chadema walivyotukanana na kuvuana nguo kwenye uchaguzi wao, na kwamba huo ni uthibitisho kuwa hawafai kupewa nafasi ya kuongoza nchi.
Badala yake, amewataka wananchi wamuunge mkono Rais Samia Suluhu Hassan.
Rajabu ameyasema hayo akiwa wilayani Lushoto, mkoani Tanga, katika ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo, sambamba na kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 48 ya CCM yanayotarajiwa kufanyika siku chache zijazo.
Soma Pia: Tanga: Matukio Yanayojiri Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Amesema kila mtu ameshuhudia jinsi Chadema walivyotukanana na kuvuana nguo kwenye uchaguzi wao, na kwamba huo ni uthibitisho kuwa hawafai kupewa nafasi ya kuongoza nchi.