johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 97,869
- 171,716
Kichwa Cha thread ndio utashi wa Mwenyekiti wa UVCCM Nyamagana kupitia ukurasa wake wa X
Yaani anatangaza Kufungia X kupitia ukurasa wake wa X 😂😂
Ila nimemwelewa ukishafungia X hutaacha itaendelea Kufungia Mitandao mingine yaani ni Sawa na kula Nyama ya mtu 🐼
======
Mwenyekiti wa CCM (Chama cha Mapinduzi) wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza Peter Begga amesema endapo yeye angekuwa Mkuu wa idara ya TEHAMA (Teknolojia ya Habari na Mawasiliano) hapa nchini miongoni mwa kazi ambayo angeifanya kwa haraka ni kuhakikisha anaifuta mitandao ya kijamii ya 'X' zamani ikijulikana kama 'twitter' na Instagram kwa kuwa hapendezwi na mijadala inayoendeshwa kwenye mitandao hiyo
Akizungumza kwenye kongamano la shirikisho la Walimu ambao ni wanachama wa CCM wilayani humo Begga amedai kuwa kupitia mitandao hiyo kumękuwa kukiendeshwa mijadala hasi dhidi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo wengi wanaoendesha mijadala hiyo ya kumchafua ni wenye chuki binafsi dhidi yake na baadhi yao wakiwa na lengo la kuwania nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia uchaguzi mkuu ujao (2025)
Katika kongamano hilo lililofanyika jijini Mwanza Juni 09.2024 Begga amewashukia baadhi ya wanasiasa kutoka ndani ya nje ya CCM ambao wamekuwa wakieneza propaganda za kubeza uwajibikaji wa serikali ya awamu ya sita (6) chini ya Rais Dkt. Samia, jambo ambalo amedai kuwa linalenga kumuharibia taswira njema aliyoijenga kwa wananchi
Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo wa CCM wilaya ya Nyamagana amedai kuwa wengi wanaoendesha mijadala hasi kwenye mitandao ya kijamii dhidi ya Rais Dkt. Samia wamekuwa wakiishi nje ya nchi na kwamba hata wale walioko hapa nchini wengi wao familia zao zinaishi nje ya Tanzania ikiwemo mataifa ya Ulaya, Marekani na kwingineko.
Jambo
Pia, soma=> UVCCM waitaka Serikali kuifungia X (zamani Tittwer)
Yaani anatangaza Kufungia X kupitia ukurasa wake wa X 😂😂
Ila nimemwelewa ukishafungia X hutaacha itaendelea Kufungia Mitandao mingine yaani ni Sawa na kula Nyama ya mtu 🐼
======
Mwenyekiti wa CCM (Chama cha Mapinduzi) wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza Peter Begga amesema endapo yeye angekuwa Mkuu wa idara ya TEHAMA (Teknolojia ya Habari na Mawasiliano) hapa nchini miongoni mwa kazi ambayo angeifanya kwa haraka ni kuhakikisha anaifuta mitandao ya kijamii ya 'X' zamani ikijulikana kama 'twitter' na Instagram kwa kuwa hapendezwi na mijadala inayoendeshwa kwenye mitandao hiyo
Akizungumza kwenye kongamano la shirikisho la Walimu ambao ni wanachama wa CCM wilayani humo Begga amedai kuwa kupitia mitandao hiyo kumękuwa kukiendeshwa mijadala hasi dhidi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo wengi wanaoendesha mijadala hiyo ya kumchafua ni wenye chuki binafsi dhidi yake na baadhi yao wakiwa na lengo la kuwania nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia uchaguzi mkuu ujao (2025)
Katika kongamano hilo lililofanyika jijini Mwanza Juni 09.2024 Begga amewashukia baadhi ya wanasiasa kutoka ndani ya nje ya CCM ambao wamekuwa wakieneza propaganda za kubeza uwajibikaji wa serikali ya awamu ya sita (6) chini ya Rais Dkt. Samia, jambo ambalo amedai kuwa linalenga kumuharibia taswira njema aliyoijenga kwa wananchi
Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo wa CCM wilaya ya Nyamagana amedai kuwa wengi wanaoendesha mijadala hasi kwenye mitandao ya kijamii dhidi ya Rais Dkt. Samia wamekuwa wakiishi nje ya nchi na kwamba hata wale walioko hapa nchini wengi wao familia zao zinaishi nje ya Tanzania ikiwemo mataifa ya Ulaya, Marekani na kwingineko.
Jambo
Pia, soma=> UVCCM waitaka Serikali kuifungia X (zamani Tittwer)