DOKEZO Mwenyekiti wa CCM Mkoa: Miili ya Watu inaokotwa kwenye Mifuko ya Rambo, Simiyu si salama

DOKEZO Mwenyekiti wa CCM Mkoa: Miili ya Watu inaokotwa kwenye Mifuko ya Rambo, Simiyu si salama

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Ipo hivi Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika ziara zake anazofanya hivi karibuni, alifika Mkoani Simiyu na katika moja ya mikutano yake na Watumishi wa Umma kuna mambo mazito yalizungumzwa.

Katika Mkutano huo pia wadau wengine walikaribishwa ikiwemo viongozi wa dini na viongozi wa CCM, lakini aliyeteka shoo na kutibua hali ya hewa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa, huyu mama anaitwa Shemsa Mohamed.

Alielezea mambo mengi ambayo najua viongozi wa Serikali hawakutaka jamii iyajue au kuyasikia ikiwemo masuala ya mauaji uonevu na uvunjwaji wa haki za binadamu unavyoendelea huku mamlaka za usalama ikiwemo Jeshi la Polisi vikiwa kimya na kutaka mambo yasifike kwenye jamii.

Sikiliza sehemu hii ya hotuba ya kiongozi huyo wa CCM alivyoelezea mambo mazito ambayo hata waandishi wa habari waliokuwepo hawakuripoti.

Waandishi wa Habari waliziwa na kupigwa mkwara na watu wa Usalama kuwa 'ole wao watoe hiyo taarifa.'

Natamani ningekuwa mwandishi wa habari nione huyo ambaye anaweza kuzuia habari yenye faida kwa jamii isitoke. Waliowatishia waandishi majina na sura zao niliziona, nawahifadhi kwa sasa, Inakera sana

Baadhi ya mambo ambayo Mwenyekiti huyo wa Chama Mkoa ameyasema ni:

1. Watu wamekuwa wakipotea kwenye mkoani hapo

2. Wizi umezidi, nyumba zinavamiwa usiku na hakuna hatua kutoka kwa vyombo vya usalama

3. Miili ya watu imekuwa wakiokotwa kwenye mifuko ya Rambo

4. Taarifa zinazoandikwa na Jeshi la Polisi sizo ambazo watu wameenda kuripoti

5. Lamadi kuna mtu amepigwa na Polisi akafa kituoni lakini taarifa ikaandikwa tofauti

Kwa ufupi hali ya usalama si nzuri Mkoani Simiyu, RPC wa Simiyu hajatoa tamko wala kuchukua hatua zozote licha ya mambo hayo kuzungumzwa mbele ya hadhara

Jiulize kwa maneno kama hayo ambayo yalitamkwa tarehe 25 mwezi wa tatu mwaka 2023, mamlaka zinakaa kimya kabisa kama vile hakuna kitu kilichozungumzwa cha msingi? Kuna shida mahala
 
Wale wa kusema magufuri alikuwa anauwa watu halafu anawatupa baharini kwenye viroba hebu waje basi hapa kutuambia hawa wa simiyu magufuri anawauwaje?

Ama kweli watanzania laana ya MUNGU kwa kumdharau na kumsingizia madhambi yule mzee itawatafuna. SUBIRIENI TU.
 
Wale wa kusema magufuri alikuwa anauwa watu halafu anawatupa baharini kwenye viroba hebu waje basi hapa kutuambia hawa wa simiyu magufuri anawauwaje?

Ama kweli watanzania laana ya MUNGU kwa kumdharau na kumsingizia madhambi yule mzee itawatafuna. SUBIRIENI TU.

Umekimbilia kwa Magufuli kwa Nini? Baadala ujadili kilichopo umekimbilia kwa Magufuli. Hakuna laana kwa muuaji..kila anayeua naye damu yake nayo itadaiwa.
 
Wale wa kusema magufuri alikuwa anauwa watu halafu anawatupa baharini kwenye viroba hebu waje basi hapa kutuambia hawa wa simiyu magufuri anawauwaje?

Ama kweli watanzania laana ya MUNGU kwa kumdharau na kumsingizia madhambi yule mzee itawatafuna. SUBIRIENI TU.
Inauma sana
 
Mkuu 'Anonymous, umetimiza wajibu wako kwa kuleta taarifa hii hapa jukwaani.

Ni wazi, huyu mama Rais wa nchi hii hana uwezo wa kuongoza nchi kama hii. Yeye ndiye Mwenyekiti wa hicho chama, lakini inaonekana hata wenyeviti wa chama huko mikoani hawana njia yoyote ya kumfikishia taarifa Mwenyekiti.

Hii aliyowasilisha Mwenyekiti wa Mkoa ni taarifa ya kutisha sana, ambayo serikali ingeshindwa kupata taarifa juu yake. Huyu mama Mwenyekiti wa Mkoa, pamoja na kutoa taarifa hii kwa Waziri Mkuu, lakini inaonyesha wazi hata yeye anayo hofu kubwa sana juu ya usalama wake. Ni kama ndani ya mkoa huo wa Simiyu, kuna genge la watu wenye madaraka wanaowatendea watu uhalifu, na kuwatia hofu kubwa

Watu hawajui wakimbilie wapi ili wasidhurike, kwa sababu waliopewa dhamana ya kulinda usalama wa wananchi ndio hao hao wanaoshiriki kwenye uovu.
 
Polisi SIMIYU ni majambazi yale, wanazo project zao za kuibia watu, mtuhumiwa kukaa mahabusu miezi 6 ni kawaida, kuwaficha maabusu kupisha ukaguzi wa nje ni kawaida, kubambikia raia wema makosa ni kawaida sana ilimradi watoe pesa tu kujikomboa, wametengeneza ka umoja na taasisi zinazotoa haki ili kufanikisha wahanga hawachomoki.
 
Acha uongo, mifuko ya Rambo ilipigwa marufuki zamani sana, na hakuna binadamu mtu mzima anayetosha katika mfuko wa rambo.

Huyu ana fursa ya kuongea na mkuu wa Mkoa moja kwa moja, anaongoza kamati ya Siasa ya mkoa, huko kote ameshindwa kusema? Asitafute umaarufu ambao haupo, atimize wajibu wake.
 
Acha uongo, mifuko ya Rambo ilipigwa marufuki zamani sana, na hakuna binadamu mtu mzima anayetosha katika mfuko wa rambo.

Huyu ana fursa ya kuongea na mkuu wa Mkoa moja kwa moja, anaongoza kamati ya Siasa ya mkoa, huko kote ameshindwa kusema? Asitafute umaarufu ambao haupo, atimize wajibu wake.
chiembe una akili kama za johnthebaptist .. Huyu mwandishi ameripoti tu kilichoongelewa na mwenyekiti wa ccm mkoa na video ipo hapo sasa uongo wake ninini hapa
 
Hawa viongozi wa aina hii ni wanafiki wakubwa. Wakiambiwa tunatakiwa tuwe na katiba mpya wanapiga danadana halafu mambo yanapoenda visivyo wanapiga kelele za uongo ili kujikomba. Uchaguzi unakuja ndiyo maana anajifanya kusikitika.
 
Hawa viongozi wa aina hii ni wanafiki wakubwa. Wakiambiwa tunatakiwa tuwe na katiba mpya wanapiga danadana halafu mambo yanapoenda visivyo wanapiga kelele za uongo ili kujikomba. Uchaguzi unakuja ndiyo maana anajifanya kusikitika
Katiba mpya itazuia watu kuuwawa?
 
Retired, hivi JPM bado ni mtawala huko simiyu? Mlimshupalia na marambo ati Beni sanane. Umesikia?
 
Huyu mama ana Hoja lakini naona njia aliyotumia kuwasilisha sio nzuri, Naamini ana access na Ofisi ya RC Muda wote
 
Mkuu 'Anonymous, umetimiza wajibu wako kwa kuleta taarifa hii hapa jukwaani.

Ni wazi, huyu mama Rais wa nchi hii hana uwezo wa kuongoza nchi kama hii. Yeye ndiye Mwenyekiti wa hicho chama, lakini inaonekana hata wenyeviti wa chama huko mikoani hawana njia yoyote ya kumfikishia taarifa Mwenyekiti.

Hii aliyowasilisha Mwenyekiti wa Mkoa ni taarifa ya kutisha sana, ambayo serikali ingeshindwa kupata taarifa juu yake. Huyu mama Mwenyekiti wa Mkoa, pamoja na kutoa taarifa hii kwa Waziri Mkuu, lakini inaonyesha wazi hata yeye anayo hofu kubwa sana juu ya usalama wake. Ni kama ndani ya mkoa huo wa Simiyu, kuna genge la watu wenye madaraka wanaowatendea watu uhalifu, na kuwatia hofu kubwa

Watu hawajui wakimbilie wapi ili wasidhurike, kwa sababu waliopewa dhamana ya kulinda usalama wa wananchi ndio hao hao wanaoshiriki kwenye uovu.
Mbona mnambebesha Sana mizigo huyu mama kwa chuki zenu za kipumbavu simiyu Kuna mkuu wa mkoa,rpc,rco,rso nk kwanini msianze kuhoji huko!? au mnafikiri mtu akiwa raisi anavikwa uMungu kwamba atajua Kila kinachotokea? muda mwingine muwe mnaficha chuki na upumbavu wenu.
 
Kulea Lea wahalifu ndio kunatufikisha huku, yani kuna wapumbavu wanajikuta hawagusiki kisa tuu kuna viongozi Fulani washenzi wanapata chochote kutoka kwao
 
Ipo hivi Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika ziara zake anazofanya hivi karibuni, alifika Mkoani Simiyu na katika moja ya mikutano yake na Watumishi wa Umma kuna mambo mazito yalizungumzwa.

Katika Mkutano huo pia wadau wengine walikaribishwa ikiwemo viongozi wa dini na viongozi wa CCM, lakini aliyeteka shoo na kutibua hali ya hewa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa, huyu mama anaitwa Shemsa Mohamed.

Alielezea mambo mengi ambayo najua viongozi wa Serikali hawakutaka jamii iyajue au kuyasikia ikiwemo masuala ya mauaji uonevu na uvunjwaji wa haki za binadamu unavyoendelea huku mamlaka za usalama ikiwemo Jeshi la Polisi vikiwa kimya na kutaka mambo yasifike kwenye jamii.

Sikiliza sehemu hii ya hotuba ya kiongozi huyo wa CCM alivyoelezea mambo mazito ambayo hata waandishi wa habari waliokuwepo hawakuripoti.

Waandishi wa Habari waliziwa na kupigwa mkwara na watu wa Usalama kuwa 'ole wao watoe hiyo taarifa.'

Natamani ningekuwa mwandishi wa habari nione huyo ambaye anaweza kuzuia habari yenye faida kwa jamii isitoke. Waliowatishia waandishi majina na sura zao niliziona, nawahifadhi kwa sasa, Inakera sana

Baadhi ya mambo ambayo Mwenyekiti huyo wa Chama Mkoa ameyasema ni:

1. Watu wamekuwa wakipotea kwenye mkoani hapo

2. Wizi umezidi, nyumba zinavamiwa usiku na hakuna hatua kutoka kwa vyombo vya usalama

3. Miili ya watu imekuwa wakiokotwa kwenye mifuko ya Rambo

4. Taarifa zinazoandikwa na Jeshi la Polisi sizo ambazo watu wameenda kuripoti

5. Lamadi kuna mtu amepigwa na Polisi akafa kituoni lakini taarifa ikaandikwa tofauti

Kwa ufupi hali ya usalama si nzuri Mkoani Simiyu, RPC wa Simiyu hajatoa tamko wala kuchukua hatua zozote licha ya mambo hayo kuzungumzwa mbele ya hadhara

Jiulize kwa maneno kama hayo ambayo yalitamkwa tarehe 25 mwezi wa tatu mwaka 2023, mamlaka zinakaa kimya kabisa kama vile hakuna kitu kilichozungumzwa cha msingi? Kuna shida mahala
Wasiojulikana wanatoka wapi tena ili hali jiwe alishtangulia? Tuliambiwa walikuwa wanatumwa na jiwe?
 
Back
Top Bottom