Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Mnakumbuka yule Mwenyekiti wa CHADEMA mkoani Dodoma ambaye siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa alikimbia na daftari la wapiga kura akidai kuwa kuna hujuma zimefanyika?
Inaonekana sasa "watu wa system wameanza ku-deal nae.
========================================================
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mkoa wa Dodoma, Aisha Madoga leo tarehe 12 Desemba, 2024 ameripoti Makao Makuu ya Polisi mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu masuala yaliyojitokeza siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27 Novemba mwaka huu.
Soma pia: LGE2024 Dodoma: Mwenyekiti CHADEMA akiwasha, apora daftari la wapiga kura baada ya kubaini kuna rafu
Baada ya kuripoti mnamo majira ya saa 4 asubuhi akiwa ameambatana na Mawakili wake, Kiongozi huyo ametumia takribani saa tano ndani ya kituo na baadae kuachiwa kwa dhamana ambapo ametakiwa kuripoti tena hapo siku ya tarehe 17 Desemba, 2024.
Wakizungumza baada ya kutoka nje ya Ofisi za Jeshi hilo wameeleza kuwa hawajaweza kuandika maelezo yoyote hivyo ametumia haki yake kisheria ya kutaka kwenda kutoa maelezo Mahakamani iwapo atakuwa na hatia.
Mnakumbuka yule Mwenyekiti wa CHADEMA mkoani Dodoma ambaye siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa alikimbia na daftari la wapiga kura akidai kuwa kuna hujuma zimefanyika?
Inaonekana sasa "watu wa system wameanza ku-deal nae.
========================================================
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mkoa wa Dodoma, Aisha Madoga leo tarehe 12 Desemba, 2024 ameripoti Makao Makuu ya Polisi mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu masuala yaliyojitokeza siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27 Novemba mwaka huu.
Soma pia: LGE2024 Dodoma: Mwenyekiti CHADEMA akiwasha, apora daftari la wapiga kura baada ya kubaini kuna rafu
Baada ya kuripoti mnamo majira ya saa 4 asubuhi akiwa ameambatana na Mawakili wake, Kiongozi huyo ametumia takribani saa tano ndani ya kituo na baadae kuachiwa kwa dhamana ambapo ametakiwa kuripoti tena hapo siku ya tarehe 17 Desemba, 2024.
Wakizungumza baada ya kutoka nje ya Ofisi za Jeshi hilo wameeleza kuwa hawajaweza kuandika maelezo yoyote hivyo ametumia haki yake kisheria ya kutaka kwenda kutoa maelezo Mahakamani iwapo atakuwa na hatia.