Pre GE2025 Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akamatwa uwanja wa Ndege Songwe

Pre GE2025 Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akamatwa uwanja wa Ndege Songwe

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
JPM alisingiziwa mabaya mengi sana
mpaka Leo anasingiziwa sana lkn ukisikia sgr,stiglers gorge power project,MAGU city na project nyingine nyingi yeye ndo mwasisi na bila kifo zingeshakamilika kitambo.na nchi ingekuwa mbali sana kimaendeleo kifo kiliidhulumu hii nchi kiongozi madhubuti kabisa.
 
Hao chadema watuache na amani yetu. Kama wanaotaka kuandamana waende Kenya ndio nchi ya maandamano. Hapa TANZANIA MTU MZIMA HATISHIWI NYAU. Waziri mkuu pinda alishasema :" Wapigwe tuu" hamna namna.
Mpuuzi
 
Kosa la Samia ni nini hapo? Sio yeye aliyeifuta Tanganyika wala aliyelazimisha Muungano. Mnamuonea tu, makosa wafanye wengine lawama apewe yeye. Samia kwa mujibu wa Nyerere na Karume na Katiba yetu ni mtanzania halisi kama watanzania wengine. Acha ubaguzi wa kike. Ni Rais yupi ambae hajakamata watu kwenye uongozi wake?
Samia anamtumia Abdul kuifilisi nchi na amenogewa hataki kuachia kwa gharama yoyote ile
 
Tushukuru Mungu hatuna visasi nchi hii. Vinginevyo kuna watu wangekuwa hawana familia ama ukoo mzima unaishi makambini.

Hii ni tunu kubwa kwa taifa, ilindwe kwa gharama yeyote ile. Rais ametupa 4Rs, hebu aoneshe kwa vitendo kwa viongozi wahuni huni wanaoleta taharuki kipindi ambacho taifa linapata maendeleo.

Waachwe wasemezane nao ni watanzania kama ambavyo wengine wapo. Hakuna mtu anayejiona yeye ni Mtanzaniw zaidi ya mwingine.
 
Polisi wajitathimini.wazalendo tukiamua kuingia barabarani hataweza kuzuia mafuriko.hamuoni kule Bangladesh?
Wazalendo?! au PANYA road tu mnataka mkaibe ubwabwa wa wabunge huko bungeni kama walivyofanya PANYA ROAD wenzenu wa huko Kenya?!
 
Sana , yaani wahuni walete mambo ya kuiga huko eti ya Gen Z? Washughulikiwe kama M7 alivyowafa ya wale wa Uganda Hadi wamekomaa.

Watuvurugie Nchi kisa? Wangekuwa wanaungwa mkono na Umma watu si wangeenda?
Polisi wa Kenya wanacheka na PANYA ROAD wanaojiita Gen Z, hapa kwetu TZ polisi hawajui kucheka na nyani wanaotaka kuvuruga amani ya nchi. Hapa ni Rungu kwenda mbele.
 
Kama ni la kawaida basi wasilalamike washangilie si ni kawaida kwao? 😁😁
Hata Afrika kusini wakati wa ubaguzi wa Rangi ilikuwa kawaida watu weusi kuuwawa na kufungwa wala hawakurudi nyuma. Binadamu wapo kama nyuki unapozidi kuwakandamiza ndivyo wanavyo zidi kuja na kupambana. CCM wasidhani wataweza kuishi na siasa za hila miaka yote Zanzibar leo tayari kumewashinda siku nyingi na sasaTanzania Bara wanakwenda kuchemsha mda si mrefu.
 
Back
Top Bottom