Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na mbunge Esther Matiko waachiwa kwa dhamana baada ya kushinda rufaa ya dhamana

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na mbunge Esther Matiko waachiwa kwa dhamana baada ya kushinda rufaa ya dhamana

Francis12

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2016
Posts
7,533
Reaction score
22,281
Mahakama Kuu Masijala ya Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 7, 2019 inatarajiwa kutoa hukumu kwenye maombi ya rufaa yaliyowasilishwa mahakamani hapo na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa (Mb) na Esther Matiko (Mb) wakipinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia dhamana kwenye kesi na. 112/2018 inayowakabili baadhi ya voingozi wakuu wa Chama na wabunge 7 wa CHADEMA.
========

UPDATE:



Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na mbunge Esther Matiko wameachiwa kwa dhamana baada ya kushinda rufaa ya dhamana katika Mahakama Kuu jijini Dar‬


Maneno ya Jaji Rumanyika akisoma hukumu

Mahakama ya Kisutu ilikabidhi jukumu lake kwa Polisi. Hakuna mahala popote warufani wamezuiwa kusafiri lakini wakati huo huo wanatakiwa kuripoti Polisi kila Juma. Hii maana yake wamenyimwa Uhuru wa kusafiri na haki ya kufanya kazi

Ni hatari sana kunyima dhamana mtu bila sababu za Msingi.

Hii ni rufaa mojawapo sijawahi kuiona Katika kazi yangu ya Ujaji. Maofisa wa mahakama kama mahakimu wanapaswa kutumia utashi wao kuamua haki za watu kwa kuzingatia Haki.

=====


Mahakama kuu ya Tanzania masijala ya Dar es Salaam chini ya Jaji Rumanyika yatengua uamuzi wa mahakama ya hakimu mkazi kisutu wa kufuta dhamana za Mhe Freeman Mbowe na Mhe Esther Matiko. Mahakama hiyo imeeleza kusikitishwa na ufutaji wa dhamana hizo na kuzitaka mahakama za chini zijionye kabla ya kufikia maamuzi yasio ya haki na kikatiba. Mahakama yaagiza warufani waachiwe mara moja.

Jaji Sam Rumanyika Katika kufuta uamuzi wa mahakama ya Kisutu kuwafutia dhamana Freeman Mbowe na Esther Matiko ametaja misingi 9 ya Mahakimu kuzingatia Katika Maombi ya dhamana.
1. Kesi inadhaminika

2. Kutoa dhamana ni tafsiri dhahiri ya mahakama ya dhana ya katiba ya kuwa mtu hana hatia mpaka mahakama itakapomhukumu vinginevyo.

3. Kufuta dhamana kunahitaji sababu kubwa kuliko sababu za kumpa mtu dhamana

4. Mahakama izingatie Ukubwa wa kosa Kutoa masharti ya dhamana

5. Masharti ya dhamana yawekwe bila kuleta hisia kuwa mpango ni kunyima mtu dhamana.

6. Mahakama izingatie adhabu kwa makosa yaliyopo mbele yake ili Pale ambapo mshatikiwa akitiwa hatiani asiwe amedhibiwa mara 2.

7. Sababu ziwe zinakubalika mahakama yeyote duniani

8. Mahakama izingatie Msongamano uliopo gerezani na je kutoa dhamana au kufuta dhamana kunachangia au kupunguza msongamano gerezani

9. Mahakama izingatie kuwa Uhuru ya mshatakiwa hauna mbadala.

Jaji Rumanyika sio tu amewaachia huru Mbowe na Matiko bali pia amefuta masharti ya dhamana ya kuripoti Polisi kila wiki.

Akisoma uamuzi huo leo, Jaji Sam Rumanyika amesema ushahidi uliowasilishwa mahakamani unaonesha Mbowe na Matiko hawakuruka masharti ya dhamana kama ilivyoelezwa na upande wa Jamhuri. Mahakama kuu imejiridhisha kwa nyaraka kuwa Mbowe alikwenda Afrika kusini kwa matibabu na akatumia kipindi chake cha mapumziko ya matibabu kwenda Ubelgiji jambo ambalo si kosa kisheria.

Pia Ester Matiko hakufika mahakamani siku ya kesi yake kwa sababu alitumwa na Spika kwenda Burundi kwa ajili ya maandalizi ya michezo ya mabunge ya Afrika mashariki. Ester aliwasilisha mahakamani barua ya Spika lakini ilikataliwa na kufutiwa dhamana.
 

Attachments

Wakionekana wanapaswa kuwa nje kwa dhamana, Je watalipwa fidia ya kuwekwa ndani muda wote huo!?

Sent using Jamii Forums mobile app

umeongea upuuzi, maana hakunaga kitu kama hicho

ebu tupekue vifungu vya sheriw vya kumtetea MBOWE ATOKE NDANI

msaidie mwanasheria kutafuta vifungu na omba atoke

umeongea kama mtanzania halisi na may be std 3 ambaye anauliza maswali badala ya ku focus kwenye KUFANYA jambo litokee
 
Mahakama Kuu Masijala ya Dar es Salaam leo Alhamis Machi 7, 2019 inatarajiwa kutoa hukumu kwenye maombi ya rufaa yaliyowasilishwa mahakamani hapo na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa (Mb) na Esther Matiko (Mb) wakipinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia dhamana kwenye kesi na. 112/2018 inayowakabili baadhi ya voingozi wakuu wa Chama na wabunge 7 wa CHADEMA.
______________________
Update..
Tunatumaini leo watapewa dhamana maana dhamana ni haki ya watuhumiwa
 
Mahakama Kuu Masijala ya Dar es Salaam leo Alhamis Machi 7, 2019 inatarajiwa kutoa hukumu kwenye maombi ya rufaa yaliyowasilishwa mahakamani hapo na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa (Mb) na Esther Matiko (Mb) wakipinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia dhamana kwenye kesi na. 112/2018 inayowakabili baadhi ya voingozi wakuu wa Chama na wabunge 7 wa CHADEMA.
______________________
Update..
wanaachiwa leo
 
Wakionekana wanapaswa kuwa nje kwa dhamana, Je watalipwa fidia ya kuwekwa ndani muda wote huo!?

Sent using Jamii Forums mobile app
Na wakionekana wanapaswa kuendelea kuwa ndani kwa kukiuka masharti ya dhamana ikiwemo kutoonekana mahakamani na kuvunja sharti la kutosafiri nje ya nchi mtaridhia waendelee tu kukaa ndani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mahakama Kuu Masijala ya Dar es Salaam leo Alhamis Machi 7, 2019 inatarajiwa kutoa hukumu kwenye maombi ya rufaa yaliyowasilishwa mahakamani hapo na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa (Mb) na Esther Matiko (Mb) wakipinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia dhamana kwenye kesi na. 112/2018 inayowakabili baadhi ya voingozi wakuu wa Chama na wabunge 7 wa CHADEMA.
______________________
Update..
YALIYOJIRI MAHAKAMANI TAREHE 7! Naona unausongo na hii kesi.
 
Haya mambo yatakuja kuandikwa baadae kwenye vitabu na masimulizi siku magufuri akifa.. tumeona viongozi wengi wakisimuliwa huko YouTube mabaya yao...

Story yako Pombe itasumiliwa na ananiasi Edgar..na kuandaliwa na denis mbagaza...

Pombe uliingia madarakani madaraka yaka kulevya.. ukazaaa,
ukafukuza,
ukatesa,
ukateka,
ukaporomosha uchumi,
ukaminya ajira,
ukabana mishahara na kupandisha madaraja ya watumishi,
ukawafunga wapinzani,
ukauwa,
ukafanya kila njama kuuwa upinzani, UKATEUWA wanao kusujudia tuu,
NCHI ukaiendesha utakavyo sio katiba itakavyo n.k

POMBE STORY YAKO ITAKUJA KUANDIKWA SIKU UKIFA.. UTAZIDIWA ATA NA RUGE MTAHABA..HUNA WEMA WOWOTE WA KUKUMBUKWA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya mambo yatakuja kuandikwa baadae kwenye vitabu na masimulizi siku magufuri akifa.. tumeona viongozi wengi wakisimuliwa huko YouTube mabaya yao...

Story yako Pombe itasumiliwa na ananiasi Edgar..na kuandaliwa na denis mbagaza...

Pombe uliingia madarakani madaraka yaka kulevya.. ukazaaa,
ukafukuza,
ukatesa,
ukateka,
ukaporomosha uchumi,
ukaminya ajira,
ukabana mishahara na kupandisha madaraja ya watumishi,
ukawafunga wapinzani,
ukauwa,
ukafanya kila njama kuuwa upinzani, UKATEUWA wanao kusujudia tuu,
NCHI ukaiendesha utakavyo sio katiba itakavyo n.k

POMBE STORY YAKO ITAKUJA KUANDIKWA SIKU UKIFA.. UTAZIDIWA ATA NA RUGE MTAHABA..HUNA WEMA WOWOTE WA KUKUMBUKWA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Jiwe ana laana haya mabaya anayofanya kuna siku naye atahukumiwa sijawahi kuona kiongozi mkatili kaka jiwe unafurahi kuona kiongozi wa upinzani kukaa mahabusu kwa muda wa miezi mitatu bila kuwa na hatia
 
Mbowe na Esther Matiko wakikaa ndani wewe unapata faida gani ?Chuki nyingine za kipuuzi kabisa unashindwa kuwa na utu kwa sababu ya buku 7
Na wakionekana wanapaswa kuendelea kuwa ndani kwa kukiuka masharti ya dhamana ikiwemo kutoonekana mahakamani na kuvunja sharti la kutosafiri nje ya nchi mtaridhia waendelee tu kukaa ndani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa umemwaga omo bila kumjibu alichouliza nikweli wadanganyika wengi hawaelewi mambo mfano mzuri wanaotukuza jiwe! Sasa kwa vile ww umzidi ufahamu alieuliza upuuzi unakila sababu yakumsaidia kuelewa
umeongea upuuzi, maana hakunaga kitu kama hicho

ebu tupekue vifungu vya sheriw vya kumtetea MBOWE ATOKE NDANI

msaidie mwanasheria kutafuta vifungu na omba atoke

umeongea kama mtanzania halisi na may be std 3 ambaye anauliza maswali badala ya ku focus kwenye KUFANYA jambo litokee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom