Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM atukana viongozi wa dini nchini, asema washike adabu zao!

Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM atukana viongozi wa dini nchini, asema washike adabu zao!

Status
Not open for further replies.

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Katika hali inayoonekana kulewa madaraka na utovu wa nidhamu nchini, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Kheri James ametoa maneno yasiyo na staha kwa viongozi wetu wa kiroho nchini kwa kuwaambia kuwa washike adabu zao.

Hii inafuatia baada ya viongozi hao akiwemo Sheikh Ponda, Baba Askofu Niwemugizi wa Kanisa Katoliki na Baba Askofu Bagonza, Baba Askofu Mwamakula, Sheikh Katimba na wengineo kutaka Uchaguzi utendeke kwa haki na kwamba tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC itende haki katika Uchaguzi kwa kutoengua wagombea wa upinzani bila sababu za msingi.

Kijana huyo aneyeonekana amevimbiwa madaraka ambapo mara kadhaa amekua akitoa kauli za kuashiria vurugu, kuchochea vurugu nchini hasa pale alipokuwa akihimiza wanachama wa UVCCM kuwa tayari kuwapiga wapinzani.

Majuzi Dr Bashiru alitoa kauli kuwataka vijana wa UVCCM kujibu hoja za wapinzani lakini badala ya kujibu hoja za wapinzani Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM anashambulia na kutukana Mababa Askofu na Masheikh nchini.

Hii inaonyesha ni kwa namna gani Chama Cha Mapinduzi kwa sasa chini ya Mwenyekiti wake ndugu Magufuli na Katibu wake Mkuu ndugu Bashiru Ally kimeshindwa kuthibiti nidhamu ndani ya Chama hicho.

Kimekuwa ni Chama kisichopenda kuambiwa ukweli, bali kusifiwa na kupewa maneno ya kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa

Hapa chini hii ni video ikimuonyesha kijana huyo akitukana na kufokea viongozi wetu wa dini.

 
Mungu atamwadhibu. Wamelewa madaraka na kuwa na kiburi Ila amini nakwambia, wakati wao umefika.
 
Huyu mvulana hana adabu, atatukanaje watu wazima wanaomzidi umri katika jamii kiasi hiki.

Yeye ni msemaji wa NEC?, au kwa sababu NEC inatenda dhulma kuumiza wapinzani na kupendelea CCM kwa hiyo anaumia pale NEC inapoambiwa ukweli?

Kweli hiki chama badala ya kuwa na vijana makini, kina vijana watovu wa nidhamu wasio na adabu. Utatukanaje mababa askofu na Masheikh kiasi hiki kisa tu wewe ni mwenyekiti wa uoja wa vijana wa CCM je ukibahatika kuwa hata mkuu wa wilaya si utanyea watu kichwani?
 
Hivi hawa jamaa huwa wanatetea nn haswa mpaka wanakuwa wakali wakiambiwa inatakikana tume huru au watanzania wanataka uchaguzi huru na wa haki?
Kwani wao hawapendi haki?
Huu ni upumbavu na ujinga wa kiwango cha PhD mtu unakuwa mkali unafoka ukiambiwa haki inatakiwa itendeke!

Takataka kabisa hawa watu!
 
Huyo na asubiri promosheni yake tu mara baada ya uchaguzi. Kwani bashite alipomtwanga warioba si alikula promo za kufamtu
 
Katika hali inayoonekana kulewa madaraka na utovu wa nidhamu nchini, Mwenyekiti wa umoja wa vijana Kheri James ametoa maneno yasiyo na staha kwa viongozi wetu wa kiroho nchini kwa kuwaambia kuwa washike adabu zao.

Hii inafuatia baada ya viongozi hao akiwemo Sheikh Ponda, baba Askofu Niwemugizi wa Kanisa Katoliki na Baba Askofu Bagonza, Baba Askofu Mwamakula, Sheikh Katimba na wengineo kutaka uchaguzi utendeke kwa haki na kwamba tume ya Taifa ya uchaguzi NEC itende haki katika uchaguzi kwa kutoengua wagombea wa upinzani bila sababu za msingi.

Kijana huyo aneyeonekana amevimbiwa madaraka ambapo mara kadhaa amekua akitoa kauli za kuashiria vurugu, kuchochea vurugu nchini hasa pale alipokuwa akihimiza wanachama wa UVCCM kuwa tayari kuwapiga wapinzani.

Majuzi Dr Bashiriu alitoa kauli kuwataka vijana wa UVCCM kujibu hoja za wapinzani lakini badala ya kujibu hoja za wapinzani Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM anashambulia na kutukana Mababa Askofu na Masheikh nchini.

Hii inaonyesha ni kwa namna gani chama cha mapinduzi kwa sasa chini ya Mwenyekiti wake ndugu Magufuli na Katibu wake Mkuu ndugu Bashiru Ally kimeshindwa kuthibiti nidhamu ndani ya Chama hicho.

Kimekuwa ni chama kisichopenda kuambiwa ukweli, bali kusifiwa na kupewa maneno ya kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa

Hapa chini hii ni video ikimuonyesha kijana huyo akitukana na kufokea viongozi wetu wa dini.


Hekima ni kitu cha muhimu kwa kiongozi.Ukiwa na hekima utachuja maneno,hutazungumza ilimradi tu uonekane una kauli.
 
Katika hali inayoonekana kulewa madaraka na utovu wa nidhamu nchini, Mwenyekiti wa umoja wa vijana Kheri James ametoa maneno yasiyo na staha kwa viongozi wetu wa kiroho nchini kwa kuwaambia kuwa washike adabu zao.

Hii inafuatia baada ya viongozi hao akiwemo Sheikh Ponda, baba Askofu Niwemugizi wa Kanisa Katoliki na Baba Askofu Bagonza, Baba Askofu Mwamakula, Sheikh Katimba na wengineo kutaka uchaguzi utendeke kwa haki na kwamba tume ya Taifa ya uchaguzi NEC itende haki katika uchaguzi kwa kutoengua wagombea wa upinzani bila sababu za msingi.

Kijana huyo aneyeonekana amevimbiwa madaraka ambapo mara kadhaa amekua akitoa kauli za kuashiria vurugu, kuchochea vurugu nchini hasa pale alipokuwa akihimiza wanachama wa UVCCM kuwa tayari kuwapiga wapinzani.

Majuzi Dr Bashiriu alitoa kauli kuwataka vijana wa UVCCM kujibu hoja za wapinzani lakini badala ya kujibu hoja za wapinzani Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM anashambulia na kutukana Mababa Askofu na Masheikh nchini.

Hii inaonyesha ni kwa namna gani chama cha mapinduzi kwa sasa chini ya Mwenyekiti wake ndugu Magufuli na Katibu wake Mkuu ndugu Bashiru Ally kimeshindwa kuthibiti nidhamu ndani ya Chama hicho.

Kimekuwa ni chama kisichopenda kuambiwa ukweli, bali kusifiwa na kupewa maneno ya kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa

Hapa chini hii ni video ikimuonyesha kijana huyo akitukana na kufokea viongozi wetu wa dini.


Hivi nani anapaswa kujibu hizo hoja ni tume au huyo jamaa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom