Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohammedi Kawaida akiwa amebeba Jeneza lenye Mwili wa Michael Kalinga

Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohammedi Kawaida akiwa amebeba Jeneza lenye Mwili wa Michael Kalinga

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Mohammedi Kawaida .Kwa uchungu,maumivu,simanzi ,majonzi na huzuni isiyopimika wala kuelezeka.

Ameshiriki na kuhusika katika shughuli zote za kuaga na kuupumzisha Mwili wa Mwenyekiti wa UVCCM Tawi la Machinjioni Makongorosi wilayani Chunya Mkoani Mbeya, Marehemu Michael Kalinga katika Nyumba yake ya Milele.alipoteza Maisha kutokana na kuuwawa kikatili na baadaye Mwili wake kutelekezwa.

Ambapo Mwenyekiti huyo wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa Ameweza kubeba Mabegani pake Jeneza Lenye Mwili wa Marehemu Michael Kalinga ambaye kwa sasa Ametangulia Mbele za Haki.

Kwa hakika kifo kinaumiza sana na wala hakizoeleki hata kidogo,hasa pale ambapo kifo hicho kimetokana na kukatishwa uhai na watu wenye roho za kishetani na waliojaa ushetani ndani yao. Kwa hakika Watanzania wote hatuna budi kukemea vikali sana matukio ya namna hii bila kujali itikadi zetu za kisiasa.. Ni lazima tukatae kabisa kumwagilia ardhi yetu kwa Damu zisizo na hatia.

Kwa sababu Damu ya mtu inazungumza hata kama mdomo na kinywa chake kimefumba.Kwa hiyo Damu zisizo na Hatia zikianza kuzungumza na kulia kwa wingi kutoka Mavumbini zilipomwagwa kuelekeza kilio chake machoni, usoni na masikioni pa Mwenyezi Mungu .Basi inaweza kuleta dhahama kutoka kwa Mungu Mwenyewe pale atakapoamua kusikiliza Madai na kilio cha Damu hizo zilizomwagwa Bila Hatia.

Vilio hivyo vinaweza kuwa vingi masikioni pa Mungu pale ambapo Damu zitaanza kuzungumza kutokea Mavumbini, huku pia vilio vikali vikitokea kutoka kwenye vinywa vya wajane na yatima walioachwa na kunyimwa haki ya kuwa na wazazi wao ambao wanajua wamekatishwa uhai wao kikatili na kwa maonezi. Mungu anaweza kujibu Mapigo na ikawa balaa kwelikweli kwa wahusika wote.

Watanzania Tujizuie kumwaga Damu zisizo na hatia kwa kila njia na kila mbinu iwezekanavyo.Tusiue mtu yeyote yule asiye na hatia.iwe ni kwa imani za kishirikina au chuki binafsi au kutumiwa na watu au kwa malipo ya pesa au kwa kutafuta utajiri au kwa kulipa kisasi au visasi au kukomeshana au wivu tu na mengine mengi ya aina hiyo.

Michael Kalinga Amepigana vita vilivyo vizuri, Mwendo Ameumaliza na Imani Ameilinda.

Screenshot_20241204-230618_1.jpg
 
well done uvccm & chairman,
R.I.P comrade Michael Kalinga
Ndugu zangu Watanzania,

Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Mohammedi Kawaida .Kwa uchungu,maumivu,simanzi ,majonzi na huzuni isiyopimika wala kuelezeka .

Ameshiriki na kuhusika katika shughuli zote za kuaga na kuupumzisha Mwili wa Mwenyekiti wa UVCCM Tawi la Machinjioni Makongorosi wilayani Chunya Mkoani Mbeya, Marehemu Michael Kalinga katika Nyumba yake ya Milele.alipoteza Maisha kutokana na kuuwawa kikatili na baadaye Mwili wake kutelekezwa.

Ambapo Mwenyekiti huyo wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa Ameweza kubeba Mabegani pake Jeneza Lenye Mwili wa Marehemu Michael Kalinga ambaye kwa sasa Ametangulia Mbele za Haki.

Kwa hakika kifo kinaumiza sana na wala hakizoeleki hata kidogo,hasa pale ambapo kifo hicho kimetokana na kukatishwa uhai na watu wenye roho za kishetani na waliojaa ushetani ndani yao. Kwa hakika Watanzania wote hatuna budi kukemea vikali sana matukio ya namna hii bila kujali itikadi zetu za kisiasa.. Ni lazima tukatae kabisa kumwagilia ardhi yetu kwa Damu zisizo na hatia.

Kwa sababu Damu ya mtu inazungumza hata kama mdomo na kinywa chake kimefumba.Kwa hiyo Damu zisizo na Hatia zikianza kuzungumza na kulia kwa wingi kutoka Mavumbini zilipomwagwa kuelekeza kilio chake machoni, usoni na masikioni pa Mwenyezi Mungu .Basi inaweza kuleta dhahama kutoka kwa Mungu Mwenyewe pale atakapoamua kusikiliza Madai na kilio cha Damu hizo zilizomwagwa Bila Hatia.

Vilio hivyo vinaweza kuwa vingi masikioni pa Mungu pale ambapo Damu zitaanza kuzungumza kutokea Mavumbini, huku pia vilio vikali vikitokea kutoka kwenye vinywa vya wajane na yatima walioachwa na kunyimwa haki ya kuwa na wazazi wao ambao wanajua wamekatishwa uhai wao kikatili na kwa maonezi. Mungu anaweza kujibu Mapigo na ikawa balaa kwelikweli kwa wahusika wote.

Watanzania Tujizuie kumwaga Damu zisizo na hatia kwa kila njia na kila mbinu iwezekanavyo.Tusiue mtu yeyote yule asiye na hatia.iwe ni kwa imani za kishirikina au chuki binafsi au kutumiwa na watu au kwa malipo ya pesa au kwa kutafuta utajiri au kwa kulipa kisasi au visasi au kukomeshana au wivu tu na mengine mengi ya aina hiyo .

Michael Kalinga Amepigana vita vilivyo vizuri ,Mwendo Ameumaliza na Imani Ameilinda.View attachment 3169192
 
Pumbavu kabisa uchungu huo unausikia kwa kuwa aliyekufa ni mkwapua kura mwenzeko?,angekufa mwanaChadema bila shaka ungeandika maneno ya makufuru
Ningependa tuondoe hisia na kuweka itikadi zetu za kisiasa katika mambo yanayogusa uhai wa mtu. Uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu Mwenyewe ambayo tunapaswa kujivunia na kutohusika kwa namna yoyote ile kukatisha uhai wa mtu asiye na hatia kwa sababu ya aina yoyote ile.
 
ufe na wewe ili makala aje abebe jeneza lako Kwa uchungu,maumivu,simanzi ,majonzi na huzuni isiyopimika wala kuelezeka huku akibubujikwa na kamasi,mate na machozi
Hivi wewe utakua na kukomaa lini akili yako? Hivi kwanini hujitambui kabisa kiasi hicho? Wewe ni mgonjwa? Una matatizo ya akili?
 
Ningependa tuondoe hisia na kuweka itikadi zetu za kisiasa katika mambo yanayogusa uhai wa mtu. Uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu Mwenyewe ambayo tunapaswa kujivunia na kutohusika kwa namna yoyote ile kukatisha uhai wa mtu asiye na hatia kwa sababu ya aina yoyote ile.
Angekufa mwanachadema ungekuwa na lugha ya staha kweli kama uliyokuwa nayo kwa huyu mfu wa CCM
 
Hivi wewe utakua na kukomaa lini akili yako? Hivi kwanini hujitambui kabisa kiasi hicho? Wewe ni mgonjwa? Una matatizo ya akili?
Akili ikomae kwani imekuwa maembe?,mawe na vichunguu ndio huwa havijitambui mimi ni mwanadamu hivyo najitambua na kutambua takataka unazoandikaga,unaniuliza mimi kama mgonjwa kwani wewe ni daktari?,unauliza nina matatizo ya akili unataka kugharamia matibabu yangu mirembe
 
Ningependa tuondoe hisia na kuweka itikadi zetu za kisiasa katika mambo yanayogusa uhai wa mtu. Uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu Mwenyewe ambayo tunapaswa kujivunia na kutohusika kwa namna yoyote ile kukatisha uhai wa mtu asiye na hatia kwa sababu ya aina yoyote ile.
Muosha huoshwa
 
Ok natoa pole kwa familia yake najua wao ndo Wana majonzi ya kweli kwani wamepoteza mpendendwa wao upande wapili wa shilingi haya mambo wanayaendekeza haohao ccm kwani tumeshapoteza wapendwa wetu wengi kutoka vyama pinzani ni haohao ccm wanatoaga na maneno ya kejeri na kufurahia matatizo ya upinzani so kama mtanania sipendi na nachukia kutoka uai wa mtanzania mwenzetu lkn mpaka hapo uyo jamaa anayetoa machozi ajue yeye ni chanzo Cha haya matatizo
 
Back
Top Bottom