Mwenyekiti wa Walimu Wasio Na Ajira (NETO) Joseph Paulo anadaiwa kukamatwa na polisi mkoani Geita

Mwenyekiti wa Walimu Wasio Na Ajira (NETO) Joseph Paulo anadaiwa kukamatwa na polisi mkoani Geita

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,917
Reaction score
11,801
Mwenyekiti wetu wa NETO Joseph Paulo Kaheza amekamatwa na police mkoani Geita. Tumethibitisha hizi taarifa kutoka kwa mjomba wake ambaye alifika katika kituo hicho cha Central Geita Mjini na kutaka kumwekea dhamana kitu ambacho kilishindikana.

Soma Pia: Umoja wa Walimu Wasio Na Ajira (NETO) wakubali wito wa Simbachawene lakini wataka kuwepo na Ulinzi kwenye kikao

IMG_0562.jpeg
Katibu Mkuu wa Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO) Daniel Edigar Mkinga ametangaza kukamatwa kwa Mwenyekiti wa NETO, Joseph Paulo Kaheza akiwa mkoani Geita kwa kile alichodai ni vuguvugu la kupigania ajira kwa walimu wa Tanzania. Ameeleza kuwa alikamatwa na askari hao wakiwa na "silaha kali".

Akizungumza na Jambo TV Jumatatu jioni, Mkinga amesema Joseph amekamatwa mchana wa siku ya Jumatatu mkoani humo katika wakati ambao umoja huo umekubali mwaliko wa kukutana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene, kwa ajili ya majadiliano kuhusu ajira za walimu nchini.

"Askari hao wameahidi kukamata viongozi wote wa NETO nchini jambo ambalo tunalilaani vikali kwani sisi sio waahini, ni watoto wa kimasikini tunaoiomba serikali haki yetu ya ajira kutokana na ugumu wa maisha uliokithiri huku mtaani", ameeleza Katibu Mkuu huyo huku akilaani na kuonesha kusikitishwa kwa Joseph kunyimwa dhamana.

Jambo TV imemtafuta Barnabas Daud, ndugu wa Joseph, mkazi wa kata ya Nyankumbu Geita Mjini ambaye ameeleza kuwa Joseph alikamatwa majira ya saa 9 mchana katika mazingira ya kutatanisha kwani awali alimuacha dukani akiwa na mkewe lakini aliporudi hakumkuta. Hata hivyo baadaye gari lisiloonesha waliomo ndani lilifika dukani hapo na watu ambao hawakujitambulisha kama ni askari kutokana na kutoonesha vitambulisho wala kuvaa sare, wakiwa wamemshikilia Joseph kwa pingu mkononi.

Daud anaeleza kuwa miongoni mwa watu wale kuliwapo aliyemfahamu kuwa ni askari, na alipoulizia kosa la nduguye hakuambiwa zaidi ya kuelezwa kuwa Joseph atapelekwa ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) na kupewa mawasiliano ya mmoja wa wale wati. Baadaye gari hilo liliondoka na Barnabas akachukua hatua ya kwenda ofisi ya RCO ambako huko aliambiwa nduguye hayupo, akafuatilia kituo kingine cha wilaya ambako hakumkuta, ndipo akawasiliana na askari wa namba aliyoichukua ambaye alimsisitizia kuwa nduguye yupo kwa RCO akihojiwa.

Barnabas alifika kwa RCO saa 11 jioni ambapo aliambiwa arudi saa mbili usiku, aliporudi akakutana na ndugu yake ambaye alimwambia sababu ya kukamatwa kwake ni kuwa sehemu ya kundi la NETO.
 
Wakuu,

Mwenyekiti wetu wa NETO Joseph Paulo Kaheza anadaiwa kukamatwa na police mkoani Geita.

Kupitia mtandao wa X taarifa zinasema kuwa kwa mjomba wa Joseph alifika katika kituo hicho cha Central Geita Mjini na kutaka kumwekea dhamana kitu ambacho kilishindikana.


IMG_0562.jpeg




IMG_0563.jpeg
 
Mwenyekiti wetu wa NETO Joseph Paulo Kaheza amekamatwa na police mkoani Geita. Tumethibitisha hizi taarifa kutoka kwa mjomba wake ambaye alifika katika kituo hicho cha Central Geita Mjini na kutaka kumwekea dhamana kitu ambacho kilishindikana.

View attachment 3248480

Nchini Zaire (DRC)! ilikuwa ni Kosa kubwa sana kwa kufanya Kitendo cha Kumkosoa mtawala wa nchi hiyo Dikteta Mobutu Sese Seko au kuukosoa Utawala wake. Hali ipo hivyo pia nchini Urusi kwa Putin na nchini China.

Kuwakosoa Madikteta ni sawa sawa na kujikatia tiketi ya kifo.
 
Kwahiyo wanataka kumuua??? Huyo mwl itakuwa ajabu sana mwlimu kuuwawa na serikali ya JMT chini ya uongozi wa samia kwa kukulalamika kukosa ajira na mwenendo mbaya wa ajira zinatolewa na serikali kwa usimamizi wa taasisi iliyojaa upendeleo undugu na rushwa, ucheleweshwaji wa mchakato bila sababu wala maelezo ya hali juu secretariat
 
Kitu vijana tunakosa kwenye mambo yetu mengi ni mifumo. Hapo unaweza ukakuta hawa NETO kwenye safu zao wote ni waalimu wasio na ajira. Hii inafanya mara nyingi sana harakati na vuguvugu za vijana wengi kuangukia pua na kuonekana ni vikundi vya wahun waleta vurugu.

Ila siku tukiona ipo sababu ya kuwa na safu zenye fani tofauti tofauti hapo tutaweza kushauri na kushinikiza mambo mengi chanya. Ushauri na kushauriwa ni jambo muhimu sana
 
Kitu vijana tunakosa kwenye mambo yetu mengi ni mifumo. Hapo unaweza ukakuta hawa NETO kwenye safu zao wote ni waalimu wasio na ajira. Hii inafanya mara nyongi sana harakati na vuguvugu za vijana wengi kuangukia pua na kuonekana ni vikundi vya wahun waleta vurugu.

Ila siku tukiona ipo sababu ya kuwa na safu zenye fani tofauti tofauti hapo tutaweza kushauri na kushinikiza mambo mengi chanya. Ushauri na kushauriwa ni jambo muhimu sana
Hawapendi kushauliwa sasa ukiuliza walicho mkamatia nini??
 
Hawapendi kushauliwa sasa ukiuliza walicho mkamatia nini??
Labda kuzua taharuki na kusambaza taarifa za uongo mtandaoni. Unajua ukitamka jambo la kitakwimu inabidi uwe makini sana.

Hawa walitakiwa hizo hotuba na maelezo yao yote wapitishe kwenye jopo la mawakili, ili kuangalia madhara na matokeo yake. Hivyo ndio mambo yanapaswa kwenda na sio hivi kwenda kiholela, lazima uzingue tu na unajua Jamhuri haina time na raia mwema (mfuata sheria) tatizo lipo ukijichanganya pahali tu wana wewe.

Huyu jamaa nilimsikiliza kidogo ila nikajua hapa na hapa kazingua na wameruka naye tayari.

Vijana tunataki tujue kuwa tufanye yote ila kamwe tusijaribu kusababisha kitisho kwenye usalama wa hili taifa, utapotea na hakuna atakayejutia. Sasa kutaka kuinua hasira za graduates ni big move inayoitaji akili sana, sio jambo la mchezo au masihara.
 
Sasa polisi kwa kosa gani? Tena kunyimwa dhamana mbona polisi wanafanya mambo ya ajabu hivi?
Kunyimwa dhamans kuna sababu nyingi ila za moja kwa moja huwa ni ama hajakamatwa kwa kosa lolote, hapo hawezi kupewa dhamana sababu hana kosa alilokamatwa nalo.

Sababu nyingine inaweza ikawa kwa ajili ya kuulinda usalama wake yeye mwenyewe. Baada ya intelijensia ya polisi kuona ipo hiyo sababu.

Sasa usiniulize mtu anakamatwaje bila kosa, hilo linawezekana na limeruhusiwa na sheria zetu wenyewe. Kukamatwa sio kosa kosa ni lile lililofanyika tu.
 
Labda kuzua taharuki na kusambaza taarifa za uongo mtandaoni. Unajua ukitamka jambo la kitakwimu inabidi uwe makini sana.

Hawa walitakiwa hizo hotuba na maelezo yao yote wapitishe kwenye jopo la mawakili, ili kuangalia madhara na matokeo yake. Hivyo ndio mambo yanapaswa kwenda na sio hivi kwenda kiholela, lazima uzingue tu na unajua Jamhuri haina time na raia mwema (mfuata sheria) tatizo lipo ukijichanganya pahali tu wana wewe.

Huyu jamaa nilimsikiliza kidogo ila nikajua hapa na hapa kazingua na wameruka naye tayari.

Vijana tunataki tujue kuwa tufanye yote ila kamwe tusijaribu kusababisha kitisho kwenye usalama wa hili taifa, utapotea na hakuna atakayejutia. Sasa kutaka kuinua hasira za graduates ni big move inayoitaji akili sana, sio jambo la mchezo au masihara.
Mkuu wacha wainuke watawala hawana uchungu na mali za TANGANYIKA wanajinufaisga wao. Kuhusu takwimu huenda kazingua kweli lakin

CWT sijui kama walitoa taarifa za uongo juu ya uhitaji wa watalaam na watu wa private kuwalipa 150k hio no doubt serikali hata leo ikiwaita wanaofanya kazi private waulizzwe watajibiwa wengine hawapat hata hio 150k
 
Kitu vijana tunakosa kwenye mambo yetu mengi ni mifumo. Hapo unaweza ukakuta hawa NETO kwenye safu zao wote ni waalimu wasio na ajira. Hii inafanya mara nyongi sana harakati na vuguvugu za vijana wengi kuangukia pua na kuonekana ni vikundi vya wahun waleta vurugu.

Ila siku tukiona ipo sababu ya kuwa na safu zenye fani tofauti tofauti hapo tutaweza kushauri na kushinikiza mambo mengi chanya. Ushauri na kushauriwa ni jambo muhimu sana
Kingine hawa wame iga chama Cha ma jobless pro max, hawa kuelewa mfumo na mipango thabiti.

shida wali ona kuji ita ma jobless ita wapa airtime, bila kujua ni shida kwa watawala wetu hawa.
 
Labda kuzua taharuki na kusambaza taarifa za uongo mtandaoni. Unajua ukitamka jambo la kitakwimu inabidi uwe makini sana.

Hawa walitakiwa hizo hotuba na maelezo yao yote wapitishe kwenye jopo la mawakili, ili kuangalia madhara na matokeo yake. Hivyo ndio mambo yanapaswa kwenda na sio hivi kwenda kiholela, lazima uzingue tu na unajua Jamhuri haina time na raia mwema (mfuata sheria) tatizo lipo ukijichanganya pahali tu wana wewe.

Huyu jamaa nilimsikiliza kidogo ila nikajua hapa na hapa kazingua na wameruka naye tayari.

Vijana tunataki tujue kuwa tufanye yote ila kamwe tusijaribu kusababisha kitisho kwenye usalama wa hili taifa, utapotea na hakuna atakayejutia. Sasa kutaka kuinua hasira za graduates ni big move inayoitaji akili sana, sio jambo la mchezo au masihara.
Hata tshekedi aliamini hivyo hivyo kama unavyo amini wewe kwamba serikali ni lidude likuuubwa halitishwi wala kutishika lakini mwisho wa siku akajua kumbe kuna serikali kikundi chake na kuna wananchi wenye nchi na ndiko tunako pelekwa sasa hivi
 
Naomba mfahamu mimi raisi wa chama Cha ma jobless pro max niko salama kabisa.

hao neto sijui neto ni wezi wa sera na jina letu la ma jobless pro max,

Raisi wa chama Cha ma jobless pro max ni Intelligent businessman.
makamu wake ni Bolotoba.

katibu wa ma jobless ni min -me, mratibu wa mipango ni Edo kissy.

Wakili wa ma jobless ni Selikavu
waziri wa mambo ya ndani ni Thecoder, na msemaji wa chama Cha ma jobless pro max ni makutupora.

Kidumu chama Cha ma jobless pro max.
OIG2.uG.jpeg
 
Kingine hawa wame iga chama Cha ma jobless pro max, hawa kuelewa mfumo na mipango thabiti.

shida wali ona kuji ita ma jobless ita wapa airtime, bila kujua ni shida kwa watawala wetu hawa.
Sure, haya mambo ni hatari sema tu vijana wengi wanachukulia simple sababu wao wanaona kama hawapo upande wa kupoteza, japo wanaweza poteza pia.
 
Sure, haya mambo ni hatari sema tu vijana wengi wanachukulia simple sababu wao wanaona kama hawapo upande wa kupoteza, japo wanaweza poteza pia.
Kuna bro mmoja ni mkandarasi, wali wahi pata tuhuma za kuchekewesha mradi kwa makusudi.

nika muuliza mbona hamja zungumza msikike, aka sema vingine waachie viongozi wa chama.

maisha yako ni bora kuliko kushindana na kutunisha msuli, kisa uonekane ume ongea!.
 
Back
Top Bottom