Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wangu Dkt. Magufuli kuna kitu ambacho haukukifanya kitakuangusha tu kwenye Uchaguzi huu

Uchaguzi 2020 Mwenyekiti wangu Dkt. Magufuli kuna kitu ambacho haukukifanya kitakuangusha tu kwenye Uchaguzi huu

U
Ndugu Mahanju, ni kweli unayoyasema; Lakini, nawaomba Watanzania tutangulize uzalendo kwanza. Uzalendo ambao ndani mwake mna kujitoa (mhanga) kwa hali na mali kwa ajili ya Nchi; kuna kujikana nafsi na kutengeneza kwa ajili ya watoto wetu, watoto wa watoto wetu, watoto wa watoto wa watoto wetu, na kuendelea.

Hebu jiulize, lipi bora, kujinyima (kwa muda) ili kile tunachokusanya tukitumie kujenga kwanza miundombinu mbalimbali (SGR, Stiglers HEP, Barabara nzuri, hospitali na vifaa tiba, eropleni, mifumo ya maji, mashule na vyuo, n.k.); Au, tukitumie kuongeza mishahara ya watumishi, na kadhalika?

Ni wazi huwezi fanya mambo yote kwa wakati mmoja. Hakutokuwa na efficiency. Lazima uwe na priority and options.
"Roma haikujengwa kwa siku moja"; hali kadhalika Ulaya magharibi au Asia. Watu walijifunga vibwebwe na leo hii vitukuu wa vitukuu ndio wanafaidi jasho la babu zao
Kwa hiyo, JPM yuko sawa. Watumishi wa Serikali na Watanzania kwa jumla, tunapaswa kujifunga mkanda na kuridhika na hiki kidogo tunachopata sasa.

Ni dhiki ya muda tu kwani tukiisha kamilisha kutengeneza miundombinu hii, Pesa inayokusanywa kutoka vyanzo mbalimbali itatumika sasa kuboresha maisha ya watu.

Tena kwa ulaiini kabisa. Serikali itakuwa na uwezo wa hata kufanya KCCCM kuwa zaidi ya 2,000/= kwa mwezi!
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki JPM.

Unachosema ni sahihi lakini huwezi kujenga ghorofa wanaowanakufa njaa
 
Kama ambavyo siku zote nimekua nikisema kua mimi ni mkweli daima na fitina kwangu mwiko. Ni MwanaCCM hai niliyekitumikia muda mrefu na bado naendelea. Rais wangu ulikosea mambo machache sana pamoja na mengine mengi makubwa uliyofanya.

MAISHA MAGUMU KWA WATANZANIA
Mwenyekiti wangu, maisha ni magumu sana kwa watanzania wote hata mtu kupata milo miwili kwa siku ni shida. Kama wasaidizi hawasemi ukweli mkuu huko mitaani watu taabani kuliko awamu iliyopita. Watu walioko vijijini hawataki kujua Dar es salaam kuna marababara za juu au kuna Airport, hawajui kama kama kuna makubwa yamefanyika. Wao wanataka maisha mazuri.
Kiukweli akitokea mgombea atakayewaambia vizuri walalahoi hawa kura zote atapewa.

BIASHARA KUWA NGUMU
Kwa sasa maisha ya wafanyabishara yamekua magumu kabisa kila mahali kuliko awamu iliyopita, lipo tatizo kubwa ambalo kama tusiposema ukweli CCM hakuna mfanyabiashara atakayetupatia kura.

MAISHA MAGUMU KWA WAFANYAKAZI WA UMMA
Ni muda sasa wafanyakazi wa umma wanalia na maslahi duni, wengi hawana amani.
Hapa kura hatupati kabisa katika kundi hili tupende tusipende. Akitokea mgombea atakayeongea vizuri na kundi hili anaweza kuvuna kura nyingi sana na atapewa ushirikiano mkubwa .Wao wanaangalia mtu atakayewajali vizuri.

Mimi najaribu kusema msije mkasema hatukurlshauri.
Sisi wakulima wa Korosho Pamba na mbaazi pia tuongeze hapo kwenye list
 
Wanasiasa wanasema " You win the people through their stomach"
Yesu Kristo aligeuza mikate mitano na samaki wawili na kuwa mikate mingi na samaki wengi wa kutosha watu 5000. Chakula kilibaki kikakusanywa na kupata vikapu 12.
Yusufu , aliyekuwa Wazari mkuu wa Misri wakati wa Mfalme Farao, alikusanya chakula kwa miaka saba ili aje awalishe watu kwa miaka mingine saba ya njaa.
Kwa hiyo hapa Duniani wanaokumbukwa kwa muda mrefu ni wale wanaowapatia watu chakula.
Ukimpatia mtu ajira, umempatia chakula.
Ukiongeza pesa kwenye mzunguko unawapatia watu chakula.
Watu wa Fedha wanasema " Money works" kwa hiyo kama hakuna pesa watu hawafanyi kazi.
Sasa hivi Mabank mengi hayatoi tena mikopo mikubwa ya kibiashara kwa sababu Benki nyingi hazina pesa na watu wengi wanashindwa kufanya biashara kwa hiyo hawahitaji kukopa.
Ardhi, nyumba nk vimeshuka bei kwa asilimia zaidi ya 75. Ardhi kubwa hapa Inchini inashikiliwa na masikini kwa hiyo waathirika wakubwa katika hili ni masikini.
Mwalimu Nyerere alihakikisha kuwa kila anayemaliza shule hata darasa la saba anapata ajira kama atapenda.
Mwalimu Nyerere alianzisha mashirika ya umma mengi ili kumsaidia mkulima na kuongeza ajira.
Uchumi wa Tanzania haukuharibiwa na Mashirika ya UMMA ila uliyumba sana kwa sababu ya Vita ya Uganda na ukame ulioikumba Inchi kwa kipindi kirefu.
 
Wenye akili wanamuheshimu Walter Rodney, mburula kama wewe lazima wawe na mawazo ya kipunguani yanayoshabihiana na muhanga wa risasi 16, kama mnavyodai
mliosoma sllybus za zamani milifundishwa ujinga eti matatizo ya mwafrika chanzo ni mzungu.Kutawaliwa sio kikwazo cha maendeleo kama alivowapoteza walter rodney,fungua ubongo
 
Kama ambavyo siku zote nimekua nikisema kua mimi ni mkweli daima na fitina kwangu mwiko. Ni MwanaCCM hai niliyekitumikia muda mrefu na bado naendelea. Rais wangu ulikosea mambo machache sana pamoja na mengine mengi makubwa uliyofanya.

MAISHA MAGUMU KWA WATANZANIA
Mwenyekiti wangu, maisha ni magumu sana kwa watanzania wote hata mtu kupata milo miwili kwa siku ni shida. Kama wasaidizi hawasemi ukweli mkuu huko mitaani watu taabani kuliko awamu iliyopita. Watu walioko vijijini hawataki kujua Dar es salaam kuna marababara za juu au kuna Airport, hawajui kama kama kuna makubwa yamefanyika. Wao wanataka maisha mazuri.
Kiukweli akitokea mgombea atakayewaambia vizuri walalahoi hawa kura zote atapewa.

BIASHARA KUWA NGUMU
Kwa sasa maisha ya wafanyabishara yamekua magumu kabisa kila mahali kuliko awamu iliyopita, lipo tatizo kubwa ambalo kama tusiposema ukweli CCM hakuna mfanyabiashara atakayetupatia kura.

MAISHA MAGUMU KWA WAFANYAKAZI WA UMMA
Ni muda sasa wafanyakazi wa umma wanalia na maslahi duni, wengi hawana amani.
Hapa kura hatupati kabisa katika kundi hili tupende tusipende. Akitokea mgombea atakayeongea vizuri na kundi hili anaweza kuvuna kura nyingi sana na atapewa ushirikiano mkubwa .Wao wanaangalia mtu atakayewajali vizuri.

Mimi najaribu kusema msije mkasema hatukurlshauri.
Nakushukuru kwa mawazo yako, siku zote lazima tuanzie uchumi wa Nchi (macro economy) kisha uchumi wa mtu mmoja mmoja (micro economy). Mhe.Rais JPM kaanza na Uchumi wa Nchi na miundombinu ,sasa 2020 -2025 yatafuata hayo. Ndivyo ilivyokuwa awamu zote. Watumishi wa umma tulipata increment moja, tumelipwa malimbikizo ya madeni (salary Arreas), likizo, kupanda madaraja baada ya uhakiki nk, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Wazazi tunasomeshewa darasa la 1 -12, mzigo michango mbalimbali ya elimu imepungua sana, maana ulikuwa unaambiwa ada 10,000/= michango 380,000/=! Ila misheni town, udalali na vitu vya namna hiyo kwa kweli vimepungua sana. Acha tufanye kazi rasmi.
 
mliosoma sllybus za zamani milifundishwa ujinga eti matatizo ya mwafrika chanzo ni mzungu.Kutawaliwa sio kikwazo cha maendeleo kama alivowapoteza walter rodney,fungua ubongo
Mjinga ni ambae hajui kuwa yeye ni mjinga. Kwa sababu hujijui kuwa wewe ni mjinga baki na ujinga wako. Kama ulisoma syllabus moja na wazazi wako, well and good. But kama wazazi wako walikutangulia, basi kwa maneno yako mwenyewe WAZAZI WAKO NA KIZAZI CHAKO KILICHOSOMA ZAMANI NI KIZAZI CHA WAJINGA. Mjinga huzaa mjinga, so wewe ni mjinga kama walivyo wazazi wako
 
Huelewi unajadiliana na nani. Hata raisi awe lisu hawezi kutoa ajira kwa watanzania wote ambao hawana ajira. Kama qewe ungekuwa na upeo wa mfu

Ndugu, mm siwezi kuajiriwa. Porojo unazo wewe na wenzako ambao mlipata elimu ya kusubiri ajira serikali. Mtasubiri sanaaaa
Dogo
Akili yako ni ndogo Kama avatar yako! Siyo kila anayetoa maoni humu mwajiriwa na serikali! Tambua Hilo kwanza kabla hujawashambulia wengine waliojiajiri wenyewe!
Usichokijua kitakusumbua daima. Soma Tena nilichoandika juu ya Sera mbili zilizonadiwa na ccm na kukosa usimamizi na mitaji ambazo zingepewa kipaumbele Kama hiki Cha flyover, sgr na bwawa Basi ajira zingekuwa za kumwaga na ingekuwa historia!
Sera za kilimo na viwanda zilihitaji msukumo mkubwa mno kuliko Ile wa she, flyover na bwawa kwani zingeajiri kuanzia wakulima na wewe unayezurura na bahasha ya kaki kwenye ofisi zetu ukisaka kuajiriwa! Usijifariji hapa Bali iambie ccm yako iache Sanaa na kuwatumia wapigakura wake mafukara na maskioni ili uendelee kuwatawala na kinyume chake itekeleze Sera inazoombea kura ili kuleta maendeleo ya kweli! Hutaki, Baki na ujinga wako na elimu yako iliyoshindwa kukusaidia!
 
Mjinga ni ambae hajui kuwa yeye ni mjinga. Kwa sababu hujijui kuwa wewe ni mjinga baki na ujinga wako. Kama ulisoma syllabus moja na wazazi wako, well and good. But kama wazazi wako walikutangulia, basi kwa maneno yako mwenyewe WAZAZI WAKO NA KIZAZI CHAKO KILICHOSOMA ZAMANI NI KIZAZI CHA WAJINGA. Mjinga huzaa mjinga, so wewe ni mjinga kama walivyo wazazi wako
Kuwa na lugha ya staha Basi eeh! Wazazi wa wenzako waweke kando na jadili hoja itapendeza kwani hata wewe unao wazazi na usingependa wawe sehemu ya mjadala Tena kwa kuitwa wajinga! Behave yourself please!
 
Na kama kuna mtanzania wa aina yako anaetegemea Lisu ndio atabadilisha maisha yake, nakubaliana na wewe kua mna shida kwenye mifumo yenu ya fahamu. Maisha yako utayabadilisha mwenyewe kwa kuonyesha uthubutu katika kupambana na maisha badala ya kusubiri mwanasiasa akufanyie hivyo. Utasubiri sana kijana.
Akili yako iko uchi.bila Sera madhubuti hayo yote ni hewa.ccm oyeee
 
Mjinga ni ambae hajui kuwa yeye ni mjinga. Kwa sababu hujijui kuwa wewe ni mjinga baki na ujinga wako. Kama ulisoma syllabus moja na wazazi wako, well and good. But kama wazazi wako walikutangulia, basi kwa maneno yako mwenyewe WAZAZI WAKO NA KIZAZI CHAKO KILICHOSOMA ZAMANI NI KIZAZI CHA WAJINGA. Mjinga huzaa mjinga, so wewe ni mjinga kama walivyo wazazi wako
Mimi ni dotcom thus Sina mawazo ya kijima Kama yako
 
Na kama kuna mtanzania wa aina yako anaetegemea Lisu ndio atabadilisha maisha yake, nakubaliana na wewe kua mna shida kwenye mifumo yenu ya fahamu. Maisha yako utayabadilisha mwenyewe kwa kuonyesha uthubutu katika kupambana na maisha badala ya kusubiri mwanasiasa akufanyie hivyo. Utasubiri sana kijana.
Sasa hao viongozi tunaowachagua wanakazi gani kama si kubadilisha maisha ya mtanzania?
 
Ndugu Mahanju, ni kweli unayoyasema; Lakini, nawaomba Watanzania tutangulize uzalendo kwanza. Uzalendo ambao ndani mwake mna kujitoa (mhanga) kwa hali na mali kwa ajili ya Nchi; kuna kujikana nafsi na kutengeneza kwa ajili ya watoto wetu, watoto wa watoto wetu, watoto wa watoto wa watoto wetu, na kuendelea.

Hebu jiulize, lipi bora, kujinyima (kwa muda) ili kile tunachokusanya tukitumie kujenga kwanza miundombinu mbalimbali (SGR, Stiglers HEP, Barabara nzuri, hospitali na vifaa tiba, eropleni, mifumo ya maji, mashule na vyuo, n.k.); Au, tukitumie kuongeza mishahara ya watumishi, na kadhalika?

Ni wazi huwezi fanya mambo yote kwa wakati mmoja. Hakutokuwa na efficiency. Lazima uwe na priority and options.
"Roma haikujengwa kwa siku moja"; hali kadhalika Ulaya magharibi au Asia. Watu walijifunga vibwebwe na leo hii vitukuu wa vitukuu ndio wanafaidi jasho la babu zao
Kwa hiyo, JPM yuko sawa. Watumishi wa Serikali na Watanzania kwa jumla, tunapaswa kujifunga mkanda na kuridhika na hiki kidogo tunachopata sasa.

Ni dhiki ya muda tu kwani tukiisha kamilisha kutengeneza miundombinu hii, Pesa inayokusanywa kutoka vyanzo mbalimbali itatumika sasa kuboresha maisha ya watu.

Tena kwa ulaiini kabisa. Serikali itakuwa na uwezo wa hata kufanya KCCCM kuwa zaidi ya 2,000/= kwa mwezi!
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki JPM.
From neutral perspective mkuu acha kufananisha ulaya magharibi na Asia (sio yote) na vitu vya ajabu.
Tatizo la serekali yetu inakosa framework ya mipango. Mtu anaweza tu akaamka akasema toa pesa fanya hiki. Chukua bilioni 2 hakikisha hili linaisha in two weeks. Kweli inatakiwa iwe hivyo kikawaida? Kwani hakuna mipango imewekwa mpk tu publisize or rather politicise mambo namna hiyo?
Naamini kinachofanywa kwenye orders kama hizo ni kitu kizuri lakini dah kwani jambo zuri hilo si lilitakiwa liwe na mikakati kabla na fedha zilizotengwa kabla.
Just saying
 
Maisha yako utayabadilisha mwenyewe kwa kuonyesha uthubutu katika kupambana na maisha badala ya kusubiri mwanasiasa akufanyie hivyo. Utasubiri sana kijana.

Si kosa lako, waliokunyima elimu ya Uraia ili usijue umuhimu wa serikali ndio hao wa kuwalahumu. Unapozungumzia Rais unauzungumzia muhimili serikali, serikali ni mwamuzi sawa na refa uwanjani, jukumu lake kubwa ni kuweka sawa mazingira ya ushindani uwanjani pasipo uonevu. Kama ulishawahi lalamika refa Fulani alikuwa mbaya, basi ndio sawa na ukipata Rais mbaya.

Timu inaweza kuwa na uthubutu wa kutosha ila kwa refa mbaya kazi bure.
 
Alichoamua kukifanya JPM na anachoendelea kukifanya sasa, cha kuijenga nchi Kwa miundombinu ndicho kilipaswa kifanywe na awamu ya Kwanza ya pili na tatu,

Kwa kuwa viongozi awamu hizo hawakujikita ktk ujenzi huo, ndio huu ugumu wa maisha tunaouona leo

Kivyovyote ndugu zangu, ili maisha yawe na uahuweni ni lazima mtu awe na kwake, Kwa maana ya kuwa na nyumba aliyoijenga mwenyewe, Kwa kuwa uko tofauti kubwa Kati ya kuishi maisha ya kuanga na maisha yakukaa ktk nyumba unayoimiliki wewe

Lakini, Wakati mtu anajenga nyumba yake! Ni lazima waksti huo awe na maisha magumu,Kwa kuwa itambidi abane matumizi, kama alikuwa na bajeti ya kila wiki ale kuku mara mbili, itamlazimu ale mara moja ikiwezekana Kwa mwezi

Lakini baada ya ujenzi kukamilika, pesa zote za alizokuwa akilia nyumba ya kupanga, nazo atazimiliki yeye

Mf mzuri, Muumbaji wetu, alituwekea miundo Mbinu yote Kwanza, ndipo akatuumba, hii inamana gani

Bila miundo Mbinu, maendeleo hakuna, usafirishaji wa mazao utafanyikaje? Umeme bei nafuu nao utapatikanaje? Usafiri wa anga nao ni mhimu mno Kwa kuwa watu watataka kuja ili nchi ipate pesa za kigeni, mahali pa kutibiwa pakuwa ni karibu vifo visivyo vya lazima vitapungua, mashule yakijenfwa, watoto wengi watapata mahali pa kusoma

Miundo Mbinu ndio Uchumi wenyewee

Ni kweli maisha ni magumu leo, lakini baada ya kuwa tumeimarisha miundo Mbinu yetu, Hali itakuwa Bora zaidi,

Chaguo sahihi la watu wanaoona mbali, Si mwingine, ni JpM pekee,

Anajua kusimamia pesa zetu, hacheki na mzungu Wala nyani
 
Wapo walio graduate mwaka huo huo wakaanzisha ufugaji wa kuku kwa msingi wa TZS 2,000,000 sasa hivi they are talking of 3 - 4mil a month. Msubiri Lisu, wengi wenu mnaamini nyumbani kwake amefunga bomba la ajira ambalo anasubiri achaguliwe ili alifunguwe ambao hamna ajira mpate ajira.

We akili hauna hiyo milion mbili inatoka wap🤔

We ni bunju
 
Ndugu Mahanju, ni kweli unayoyasema; Lakini, nawaomba Watanzania tutangulize uzalendo kwanza. Uzalendo ambao ndani mwake mna kujitoa (mhanga) kwa hali na mali kwa ajili ya Nchi; kuna kujikana nafsi na kutengeneza kwa ajili ya watoto wetu, watoto wa watoto wetu, watoto wa watoto wa watoto wetu, na kuendelea.

Hebu jiulize, lipi bora, kujinyima (kwa muda) ili kile tunachokusanya tukitumie kujenga kwanza miundombinu mbalimbali (SGR, Stiglers HEP, Barabara nzuri, hospitali na vifaa tiba, eropleni, mifumo ya maji, mashule na vyuo, n.k.); Au, tukitumie kuongeza mishahara ya watumishi, na kadhalika?

Ni wazi huwezi fanya mambo yote kwa wakati mmoja. Hakutokuwa na efficiency. Lazima uwe na priority and options.
"Roma haikujengwa kwa siku moja"; hali kadhalika Ulaya magharibi au Asia. Watu walijifunga vibwebwe na leo hii vitukuu wa vitukuu ndio wanafaidi jasho la babu zao
Kwa hiyo, JPM yuko sawa. Watumishi wa Serikali na Watanzania kwa jumla, tunapaswa kujifunga mkanda na kuridhika na hiki kidogo tunachopata sasa.

Ni dhiki ya muda tu kwani tukiisha kamilisha kutengeneza miundombinu hii, Pesa inayokusanywa kutoka vyanzo mbalimbali itatumika sasa kuboresha maisha ya watu.

Tena kwa ulaiini kabisa. Serikali itakuwa na uwezo wa hata kufanya KCCCM kuwa zaidi ya 2,000/= kwa mwezi!
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki JPM.

Hongera sana kwa mchango wako, binafsi naachana na mahaba kwa Magufuli hafai kabisa kabisa anatembea anagawa fedha halafu haoni umuhimu wa watu wengine, ngoja ajifunze kulimia meno, upepo wa kisulisuli atauona atalii ahuuu ahuuu,!!!
 
2020 watanzania tutamchagua JPM kwa kura za kutosha.
Mazuri ya JPM ni mengi sana,changamoto huwa zipo tu.hata U.S kuna raia wanalalamikia changamoto za taifa lao.
ilhali tunaambiwa U.S ni kinara wa kila jambo la kimaendeleo.
Wasiojulikana buana!
 
Alichoamua kukifanya JPM na anachoendelea kukifanya sasa, cha kuijenga nchi Kwa miundombinu ndicho kilipaswa kifanywe na awamu ya Kwanza ya pili na tatu,

Kwa kuwa viongozi awamu hizo hawakujikita ktk ujenzi huo, ndio huu ugumu wa maisha tunaouona leo

Kivyovyote ndugu zangu, ili maisha yawe na uahuweni ni lazima mtu awe na kwake, Kwa maana ya kuwa na nyumba aliyoijenga mwenyewe, Kwa kuwa uko tofauti kubwa Kati ya kuishi maisha ya kuanga na maisha yakukaa ktk nyumba unayoimiliki wewe

Lakini, Wakati mtu anajenga nyumba yake! Ni lazima waksti huo awe na maisha magumu,Kwa kuwa itambidi abane matumizi, kama alikuwa na bajeti ya kila wiki ale kuku mara mbili, itamlazimu ale mara moja ikiwezekana Kwa mwezi

Lakini baada ya ujenzi kukamilika, pesa zote za alizokuwa akilia nyumba ya kupanga, nazo atazimiliki yeye

Mf mzuri, Muumbaji wetu, alituwekea miundo Mbinu yote Kwanza, ndipo akatuumba, hii inamana gani

Bila miundo Mbinu, maendeleo hakuna, usafirishaji wa mazao utafanyikaje? Umeme bei nafuu nao utapatikanaje? Usafiri wa anga nao ni mhimu mno Kwa kuwa watu watataka kuja ili nchi ipate pesa za kigeni, mahali pa kutibiwa pakuwa ni karibu vifo visivyo vya lazima vitapungua, mashule yakijenfwa, watoto wengi watapata mahali pa kusoma

Miundo Mbinu ndio Uchumi wenyewee

Ni kweli maisha ni magumu leo, lakini baada ya kuwa tumeimarisha miundo Mbinu yetu, Hali itakuwa Bora zaidi,

Chaguo sahihi la watu wanaoona mbali, Si mwingine, ni JpM pekee,

Anajua kusimamia pesa zetu, hacheki na mzungu Wala nyani

Mtaisoma namba na ngonjera zenu, fyuuu......na mtajamba sana mgombea wenu
 
Back
Top Bottom