Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 9,258
- 10,014
Kumbuka Jairo, alienda kwa Yesu akaomba Yesu aende nyumbani kwake, aweke mkono wake juu ya kichwa cha mtoto wake apone. Yesu akasema tunakwenda, ila wakachelewa njiani.Mimi sio bora kuliko wengine ila napambana kwa namna ilio haki, kwa namna ilio ya juhudi huku namtanguliza alioiumba dunia hii.
Kila nachogusa ni kama kiko allergic na mikono yangu, hakiwi ridhiki, hakikaii, watoto watakula nini, nimtamtunza vp huyu mrembo ambae Mungu alinijalia.
Mimi ni mpumbavu kuliko wote? Mimi ni mdhambi kuzidi wadhambi wengine?
Je, natwanga maji kwenye kuni? Je nasukuma ukuta? Maana baba jitihada yangu kukufikia hailingani na muelekeo nilio nao.
Mama anataabika, mimi nitaabika, mdogo wangu anataabika,
Nimemuona mama yangu akikuliliia miaka nenda miaka rudi ila bado amekuwa rafiki wa tabu na mateso,.
Je, baba yangu ni laana umeiruhusu katika nzao yake, je ni basi tu hatupo katika mipango ya baraka zako?
Nashuhudia tu makuu ya hii dunia, hata walio na dhambi wakifurahia kiasi, ila mimi nimekuwa cas study ya tabu
Mbona saul alikuwa muuaji ila ulimpa ukuu wa milele, mimi ni wa aina gani hadi niwe mtumwa wa dhiki kiasi hiki
Baba, nimekufanyia makubwa, nimekulilia, hata kama nilikosea ila ilikuwa ni kwa jina lako.
Kwanini utake kuruhusu nifanye maamuzi utafikiri mlugha mlugha ambae hajawi kukutumainia?
Mara wasaidizi wa Jairo wakafika toka nyumbani na kilio wakimwambia Jairo, wala usimsimbue Yesu, mtoto amekufa. Jairo hakulalamika kwa Yesu kwanini amechelewa kusikia na kutekeleza ombi lake. Na Yesu alimwambia Amini tu. Yaani AAMINI mtoto atapona. Jairo aliamini.
Ndugu, mwamini Mungu usimtilie mashaka kuwa hajibu. Ukiacha kuamini na kuweka mashaka anakupa kulingana na mashaka yako, yaani picha inayoiona kwenye mashaka yako ndiyo utaiona kwenye maisha yako. Ukiamini, unakuwa na picha ya kile kizuri unachokitarajia na utakipata. Anza kuamini
