Mwigulu adai wananchi ndio walioshauri tuweke tozo

Mwigulu adai wananchi ndio walioshauri tuweke tozo

Viongozi wote serikalini hawa amini uwepo wa Mungu, ingekuwa wana amini wasingekuwa makatili kiasi hicho.
Tozo ni ushauri na matakwa ya wananchi, wameyapokea na kuyafanyia kazi. Tunapigwa tozo kweli kweli. Tuseme sawa serikali yetu ni sikivu na inafanyia kazi maoni na matakwa ya wananchi.

Vipi kuhusu kikokotoo?? Je, wananchi pia wanakitaka?? Je siku zote wamekua wakiwasifia kuwa nacho ni kizuri?? Hamsikii kelele za watumishi juu ya kikokotoo?? Mwigulu acha kulisha wananchi maneno, kumbuka kuna kuulizwa kesho kuhusu uchunga wako mbele ya Mola wako.
 
Kweli sisi wananchi wajinga kama alivyosema kiongozi wa upinzani yaani tumependekeza tozo wenyewe


Halafu tuje tulalamike huu ni ujinga kwekikweli!

Waziri atuambie wananchi wangapi walipendekeza Kati ya wangapi unaweza kuta wananchi wenyewe ni mawaziri na wafuasi tu.

Mambo ya wote tuwe wote, tozo iliyopendekezwa bungeni ni za simu wa siyo za kibenki
sawa lakini hii nchi tumechelewa sana kimaendeleo sasa sijui kulinganisha na nani
Hili kundi la.mchwa linatakiwa kupumzishwa haraka sana kuanzia October na kumalizana nao mwakani!! Wametuchoka sana.
 
Ama hakika yule binti aliimba " wanatuona nyani" wakamtia ganzii wee lakini huu si unyani huu wanatufanyia ajira hakuna,huduma muhimu za kijamii mbaya mno, mashirika ya umma yanakufa, ufisadi na wizi umeshamiri, mmonyoko wa maadili unatisha ( ubakaji na ulawiti) lakini yote hayo hawajayaona ila kwenye kuomba kuongeza tozo chaaaap .WALAAANIWE
 
Waziri wa Fedha Mh Mwigulu akizungumza na Waandishi wa habari amesema kwamba Wananchi wenyewe ndio walioshauri serikali iweke Tozo ili kupanua wigo wa mapato , na kwamba ilichofanya serikali ni kuufanyia kazi ushauri wa Wananchi.
---

Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema wananchi ndio walioshauri Serikali ipanue wigo wa tozo za miamala kwa kujumuisha miamala yote ya kielektroniki, ili wananchi wote wachangie maendeleo. Ameeleza kuwa awali miamala iliyokuwa ikitozwa ni iliyokuwa ikifanyika kwa simu pekee.

Chanzo: SwahiliTimes
Wananchi wa wapi waliokubali hili?

#KataaMachawa
#KataaUozo2025

Mkuu kuna hashtag mpya ya kutembeza JF Erythrocyte Mshana Jr
 
Hao wananchi waliyasema hayo kupitia kura ya maoni au utaatibu gani ulitumika kupata hayo maoni ya watanzania? Viongozi acheni kutulisha maneno.
 
Na je kama walisema wanazitaka mkaweka, basi tukisema hatuzitakitazitoa kesho?
 
Hayo maoni ya wananchi waliyakusanya lini na kwa njia gani?

Aache uongo, hizo tozo zimepitishwa na lile bunge la CCM lisiloweza kuihoji chochote serikali kisha Rais akaweka saini.

Si ndio hapo aache uongo wake kwa kumbukumbu rasmi ilo liwazo alilitoaga mbunge wa ilala hukohuko bungeni naye akalibeba watu wanalilamikia yeye anaongea shudu au anataka na sisi hadi tuandamane kama kenya ndio aliondoe
 
Wananchi gani? huyu jamaa hatufai hata kidogo.
 
Waziri wa Fedha Mh Mwigulu akizungumza na Waandishi wa habari amesema kwamba Wananchi wenyewe ndio walioshauri serikali iweke Tozo ili kupanua wigo wa mapato , na kwamba ilichofanya serikali ni kuufanyia kazi ushauri wa Wananchi.
---

Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema wananchi ndio walioshauri Serikali ipanue wigo wa tozo za miamala kwa kujumuisha miamala yote ya kielektroniki, ili wananchi wote wachangie maendeleo. Ameeleza kuwa awali miamala iliyokuwa ikitozwa ni iliyokuwa ikifanyika kwa simu pekee.

Chanzo: SwahiliTimes
Naibu spika Zungu ndiye aliyekuja na hii idea.

Huyu mjinga asituone mapoyoyo.

Tozo ni ukatili mwingine wa serikali dhidi ya raia. Kampeni zijazo mtalia
 
Back
Top Bottom