Mwigulu aliacha lini kuutaka Urais?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mwigulu Lameck Nchemba Madelu alijitokeza kwenye kinyang'anyiro cha 2015.



Kwa kweli siyo siri kuwa huyu ndugu alikuwa na kiu kubwa ya kuitumia haki yake hiyo ya kikatiba. Basi tu wajumbe hawakuzithamini potentials zake nyingi anazozijua mwenyewe.

"Pana maswali ya kujiuliza kwa yeyote anayeikodolea macho fursa ya 2025."

Je, kiu ya ndugu Madelu kama ilikwisha, ilimalizwa na nini?

Je ni uchochoro upi wa kupitia angali nao Madelu kuweza kuipata nafasi hiyo adhimu japo hata kwa kuwa candidate tu?

Vipi hii Singida United imechipuka chipuka kama uyoga tu?

Vipi haya mabango kuendelea kuwepo wakati wagombea wengine walisha vunja makundi?

Penye Tozo pana njia.
 
Japo mimi namsuport Mwingulu kwenye urais kwa sababu hii Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President!-Nimeguswa! lakini 2025 ni awamu ya pili ya Samia ambayo ataitoa zawadi kwa Zanzibar for one term kumalizia term yake, hivyo 2030 ni zamu ya mgombea mwanamke Mkristu probably Dr. Tulia!. 2040 ni zamu ya Muislamu. Sasa Mwigulu atapitia wapi?.
P
 

Uyasemayo mkuu yamfanye vipi Madelu kuacha kufurukuta? Mfa maji aliacha lini kutapa tapa?
 
Naona, basi wewe ni Mwanamalundi wa zama zetu, umekuja katika umbo la Mwanamayalla.
 
 
Mungu atatuamulia
 
Acha ujinga wewe jamaa! Hatujawahi kuwa na zamu eti this time muisiramu au this time ni mkristo! Au this time Tanzania bara au this time Tanzania visiwani! Jakaya alitoka bara,akaja Magu alitoka bara! Nilikua nakuheshimu sana humu jukwaani, kumbe na wewe ni hovyo kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…