Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 577
- 2,595
Waziri wa Fedha na mipango Dr. Mwigulu Nchemba akizungumza na Clouds 360 asubuhi hii kuhusu Deni la Taifa amesema Tanzania ni nchi iliyo na sifa nzuri kimataifa, ikiwemo kuwa na uwezo wa kukopesheka pasipo vikwazo.
Akijibu swali la Mwandishi wa habari aliyetaka kujua kwanini anajisifu kuwa na uwezo wa kukopa huku deni la Taifa likizidi kukua, Dr. Nchemba amesema kuwa kukopesheka ni sifa nzuri tofauti na watu wanavyodhani.
“Kimsingi watu wengi wanadhaniaga siyo sifa, wanadhani labda siyo sifa. Kimsingi, kiuchumi, kiutaalam, kama nchi inaweza kukopesheka ni sifa moja kubwa kuliko nchi isiyoweza kukopesheka”
Amesisitiza kuwa ukiona nchi haikopesheki jua kuwa Nchi hiyo haina Serikali au imekopa hadi imefilisika hivyo haiwezi tena kukopesheka.
Ameongeza, “hata hapa Afrika Mashariki, mwekezaji yeyote sasa hivi, ndio maana mikutano mikubwa ikifanyika nje, Rais mmoja anayesumbuliwa sana duniani kugombewa appointments mpaka zinajaa ni Rais wa Tanzania kwa sababu nchi yake ipo properly maganed kwenye maswala ya uchumi. Mtu anaweza kuwekeza, hata sekta binafsi kukopeshwa kwake ni lazima nchi iwe na hizi sifa”
.............
Kuongezeka kwa deni la taifa kwa kiasi cha Shilingi 21 trilioni ndani ya miezi 6 kumezua tafrani na mijadala mikali kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari nchini Tanzania.
Taarifa ya uchumi ya mwezi Novemba 2022 iliyotolewa hivi karibuni na Benki Kuu ya Tanzania inaonyesha kuwa hadi kufikia mwezi Oktoba 2022 deni la taifa lilikuwa limefikia Shilingi 90.35 trilioni.
Alipokuwa akisoma Bajeti ya Serikali mwezi Juni, Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba alisema hadi mwezi Aprili 2022 deni la taifa lilikuwa limefikia Shilingi 69.4 trilioni
Hii inaonyesha wazi kuwa deni la taifa limeongezeka kwa kiasi cha Shilingi 20.91 trilioni kati ya Mwezi Aprili na Oktoba mwaka huu.
Akijibu swali la Mwandishi wa habari aliyetaka kujua kwanini anajisifu kuwa na uwezo wa kukopa huku deni la Taifa likizidi kukua, Dr. Nchemba amesema kuwa kukopesheka ni sifa nzuri tofauti na watu wanavyodhani.
“Kimsingi watu wengi wanadhaniaga siyo sifa, wanadhani labda siyo sifa. Kimsingi, kiuchumi, kiutaalam, kama nchi inaweza kukopesheka ni sifa moja kubwa kuliko nchi isiyoweza kukopesheka”
Amesisitiza kuwa ukiona nchi haikopesheki jua kuwa Nchi hiyo haina Serikali au imekopa hadi imefilisika hivyo haiwezi tena kukopesheka.
Ameongeza, “hata hapa Afrika Mashariki, mwekezaji yeyote sasa hivi, ndio maana mikutano mikubwa ikifanyika nje, Rais mmoja anayesumbuliwa sana duniani kugombewa appointments mpaka zinajaa ni Rais wa Tanzania kwa sababu nchi yake ipo properly maganed kwenye maswala ya uchumi. Mtu anaweza kuwekeza, hata sekta binafsi kukopeshwa kwake ni lazima nchi iwe na hizi sifa”
.............
Kuongezeka kwa deni la taifa kwa kiasi cha Shilingi 21 trilioni ndani ya miezi 6 kumezua tafrani na mijadala mikali kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari nchini Tanzania.
Taarifa ya uchumi ya mwezi Novemba 2022 iliyotolewa hivi karibuni na Benki Kuu ya Tanzania inaonyesha kuwa hadi kufikia mwezi Oktoba 2022 deni la taifa lilikuwa limefikia Shilingi 90.35 trilioni.
Alipokuwa akisoma Bajeti ya Serikali mwezi Juni, Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba alisema hadi mwezi Aprili 2022 deni la taifa lilikuwa limefikia Shilingi 69.4 trilioni
Hii inaonyesha wazi kuwa deni la taifa limeongezeka kwa kiasi cha Shilingi 20.91 trilioni kati ya Mwezi Aprili na Oktoba mwaka huu.