Mwigulu Nchemba: Tanzania haikutuma maombi wala kulipia kuingia uchumi wa kati. Agusia deni la Taifa

Mwigulu Nchemba: Tanzania haikutuma maombi wala kulipia kuingia uchumi wa kati. Agusia deni la Taifa

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Leo Dkt. Mwigilu Nchemba alisamama kuhitimisha hoja ya mapendekezo ya mpango wa tatu wa maendeleo ya Taifa wa miaka mitano kwa mwaka 2021/22 hadi 2025/26 kwa niaba ya wizara ya fedha na wabunge kujadili kwa takribani siku tano. Pamoja na mambo mengine amefafanua hoja chache ikiwemo mjadala wa tafsiri ya uchumi wa kati, maana yake na kwa mwananchi mmoja mmoja.

Mwigulu Nchemba: Utaratibu wa kuingia uchumi wa kati ni utaratibu ambao unazingatia vigezo, Tanzania kuingia uchumi wa kati haikutuma maombi kwamba tunaomba na sisi tuwe nchi ya kipato cha kati, hatukufanya application na wala Tanzania haikulipia.

Ni jambo linalozingatia vigezo tena vigezo vyenyewe vimezingatiwa na taasisi kubwa zinazoheshimika duniani, World Bank, IMF na wachumi wote ambao wameitangaza Tanzania ni ya uchumi wa kati wala sio washabiki wa CCM, ni taasisi za wasomi waliobobea na hawajaanza kwa kuitangaza Tanzania, zipo nchi ambazo zimewahi kufika kule na zimefika kule kwa kuzingatia vigezo.

Angalia nchi inayoweza kulipia takribani bilioni 700 kulipia watoto kwenye elimu ya juu, tunaita mikopo lakini kimsingi ni bajeti ya serikali kwasababu hawakopi benki hawa, ni bajeti ya serikali. Mambo mengi yamebadilika hata jana tu Simba kushinda kule ni uchumi wa kati ndio maana hawakuwahi kushinda siku zilizopita, viwango vyao vilikuwa vya kiuchumi wa kati.

Wale wapiga ramli wanaosema hatutaweza, niwaambieni tunasonga mbele haturudi nyuma, tunakwenda Kaanani.

======

Kuhusu deni la Taifa, Mwigulu amesema viashiria vyote vinaonesha deni ni himilivu akitoa mfano deni la nje kwa pato la Taifa ukomo wake huwa ni aslimia 55 ilhali Tanzania ipo asilimia 17.3
 
Kwanini ni Mwigulu Nchemba ndiye kawa msemaji wa Wizara hii nyeti? Waziri husika na Naibu wake hawapo?
Unaweza kukuta anakabidhiwa wizara sidhani kama mitishamba ya Kigoma ina nguvu kuizidi ya Singida.

Ngoja tuone kale kawizara ka KS ni kadogo na mabosi wako wengi mara JM mara AG yaani waziri huwezi kujimwambafy!
 
Unaweza kukuta anakabidhiwa wizara sidhani kama mitishamba ya Kigoma ina nguvu kuizidi ya Singida.

Ngoja tuone kale kawizara ka KS ni kadogo na mabosi wako wengi mara JM mara AG yaani waziri huwezi kujimwambafy!
Kwa maana hiyo wapo mle mle Mjengoni halafu Jamaa anafanyia zoezi Wizara yao ili akabidhiwe?
 
Hivi Bado kuna watu wanataka tujadili hili jambo?

Nadhani maswala ya msingi ya kujadili ni namna gani tutaongeza maviwanda na wananchi wapate ajira.

Swala la uchumi wa Kati nadhani tumeshafika na tunahitaji kufanya mengine mengi zaidi ili kufikia hatua nyingine.
 
Ni jambo linalozingatia vigezo tena vigezo vyenyewe vimezingatiwa na taasisi kubwa zinazoheshimika duniani, World Bank, IMF na wachumi wote ambao wameitangaza Tanzania ni ya uchumi wa kati wala sio washabiki wa CCM, ni taasisi za wasomi waliobobea na hawajaanza kwa kuitangaza Tanzania, zipo nchi ambazo zimewahi kufika kule na zimefika kule kwa kuzingatia vigezo.
"Vigezo" na "Taasisi kubwa zinazoheshimika duniani" ni kwa maswala ya kiuchumi tu?

WHO na wasomi wabobezi kuhusu mambo ya magonjwa ambukizi wao hatuwasikilizi kwa kuwa huko CCM mashabiki wake ni wataalam zaidi kuwashinda hao wa dunia nzima?

Unafiki wa hali ya juu sana huu!
 
Mwigulu kabobea katika maswala hayo huenda anaitaka hiyo wizara kuliko hii aliyonayo.
 
Huyu uchumi hajui, ni kosa sana kumpa nafasi ya kuongelea swala kama hili, akae na wafanya biashara akajifunze namna anaweza saidia nchi iwe na uchumi imara, nashindwa kuelewa hawa watu wanashindwaje kujifunza kutoka China,Singapore nk. Mbona rahisi sana hili somo.
 
Uchumi wa kati ni vyema kufika huko n tumefika ila kuna mambo mengi bado hayapo sawa.

Kuna mambo hayako sawa kwakuwa kila waziri anadhamanaya kuzungumzia wizara yake ila naona kwa huyu iko tofauti.

Kuna mambo yalekebishwe kuhusu huyu mtu au kwake yamemshinda?
 
Waziri wa Sheria haya mambo yanakuhusu vipi? Kesi zinachelewa mahakamani!. Elimu yake ya kupewa na kuandikiwa pale mlimani 😂😂 muachie Dr Mipango wizara yake.
 
Back
Top Bottom