Pre GE2025 Mwigulu Nchemba: Upinzani hawafai kabisa watauvunja Muungano

Pre GE2025 Mwigulu Nchemba: Upinzani hawafai kabisa watauvunja Muungano

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Na hili ndilo Tatizo letu watanganyika.

Kama Kuna Zanzibar basi pia Kuna Tanganyika. Wao wana "Serikali ya mapinduzi Zanzibar", iweje sisi tujiite "Tanzania bara"?

Ili kuwe na Tanzania bara ni lazima kuwe na Tanzania visiwani. Sasa Tanzania visiwani haipo kwa nini tuwe na Tanzania bara!!??
Ndiyo ujue Muungano uko upande mmoja. Wairudishe Tanganyika yetu.
 
Ivi haiwezekani Rwanda na Burundi kuwa Mikoa ya Tz, halafu Zanzibar nayo Mikoa ya Tz.Tunakwamaa?!
 
upuuzi mtupu kama wenye PhD wanaongea hivi na kibajaji wasemeje? kuongea ongea tu mradi tonge liende mdomoni kama vile ana hati miliki ya kuwepo madarani kama Ayatollah.
 
"Inawezekana wenzetu hawa kwa tamaa za madaraka hawajatilia maanani suala hili (Muungano) viongozi hao wanafikiri kuwa lugha hizo za kuhatarisha muungano zina mashiko kwa wapiga kura wao na kana kwamba hawajawahi kunufaika na uwepo wa muungano, kuligawa Taifa kwa ajili ya kufanikisha ajenda ya kisiasa ni jambo la hatari sana.

"Ndugu Watanzania, viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani wanaotaka kuligawa Taifa letu kwa maslahi mepesi hawastahili kuaminiwa kupewa uongozi wa nchi, ukiwajaribishia hawa watauvunja muungano wetu, wataiua nchi yetu, hawafai kabisa,"

PIA SOMA
- LIVE - Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025, leo Juni 13, 2024 Bungeni, Dodoma
Yaani huyu jamaa huyu, badala ueleze mikakati ya kuinua uchumi, hotuba robo tatu imejaa mambo ya muungano, ajari na VAR na mawaziri wamuungano, mambo ya ndani na michezo wao hotuba zao ziseme nini??? Kama ni kweli 2030 bora Tulia au SimbaChawene kuliko huyu mbabaishaji.
 
Nimekuwa nasoma maoni ya watanzania wengi kuhusu faida au hasara za muungano nimegundua wengi wanaongelea mambo waliyosikia kuliko uhalisia wake.Kuhusu makazi watanganyika wengi tu wanakaa zanzibar japo sio wengi ukilinganisha na wao kuja kukaa Tanganyika na sababu zipo.Pia kiulinzi kuna d
Faida sana Tanganyika kuungana na zanzibar la sivyo yanayotokea Congo,Msumbiji,Syria,Somalia,Ethiopia,Eritrea, na kote kwenye nchi zenye vita yangeweza kutokea hapa kama kusingekuwa na muungano.Ni kwa bahati mbaya saba watanzania wengi hatusomi siasa za kimataifa tukajua Dunia inavyoendeshwa sababu ya utajiri wa amani waliyotuwekea waasisi wetu.
 
Hata wakiuvunja kwani una faida gani?
 
Akiwasilisha bajeti ya serikali kwa mwaka 24/25 mh mwigulu aliongea sana kuhusu watu wanaotoa maoni tofauti kuhusu muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Aliongea kwa hisia sana kiasi ikanipa kujiuliza kuna uhusiano gani kati ya hicho anacholalamikia na kuwasilisha bajeti?
 
Viongozi wetu wengi kitu wanawezea ni unafiki,kujikomba na Kuvaa tai
 
Namng'ata sikio tu Waziri Mwigullu kwamba Mbowe hawezi kuvunja muungano hata kama Kuna siku Chadema itatwaa DOLA

ACT Wazalendo ndio hawataki kabisa serikali 2 wao wanataka 3

Jumaa Mubarak 😄
 
Namng'ata sikio ti Waziri Mwigullu kwamba Mbowe hawezi kuvunja muungano hata kama Kuna siku Chadema itatwaa DOLA

ACT Wazalendo ndio hawataki kabisa serikali 2 wao wanataka 3

Jumaa Mubarak 😄
[/QUO
Madelu Nchemba ana ugomvi na home boy wake Tundu Lissu,
Muungano utavunjwa na WA Zanzibar,
Wanataka mamlaka kamili,
 
..Othman Masoud na ACT Wazalendo wamekuwa wakitoa kauli kali dhidi ya muungano kuliko Chadema.

..Sielewi kwanini Ccm wanawalaumu zaidi Chadema kuliko ACT kwamba wanatishia muungano na ni wabaguzi.
 
Namng'ata sikio tu Waziri Mwigullu kwamba Mbowe hawezi kuvunja muungano hata kama Kuna siku Chadema itatwaa DOLA

ACT Wazalendo ndio hawataki kabisa serikali 2 wao wanataka 3

Jumaa Mubarak [emoji1]
Kwani ni dhambi muungano huu fake ukivunjika? Wananchi wenye nchi na si viongozi wachache ndo wenye mamlaka ya kuamua hatma ya muungano,wakiukataa unavunjwa fasta,viongoz wajinga watakapopungua,Tanganyika itarudi na Zanzibar itakuwa huru
 
"Inawezekana wenzetu hawa kwa tamaa za madaraka hawajatilia maanani suala hili (Muungano) viongozi hao wanafikiri kuwa lugha hizo za kuhatarisha muungano zina mashiko kwa wapiga kura wao na kana kwamba hawajawahi kunufaika na uwepo wa muungano, kuligawa Taifa kwa ajili ya kufanikisha ajenda ya kisiasa ni jambo la hatari sana.

"Ndugu Watanzania, viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani wanaotaka kuligawa Taifa letu kwa maslahi mepesi hawastahili kuaminiwa kupewa uongozi wa nchi, ukiwajaribishia hawa watauvunja muungano wetu, wataiua nchi yetu, hawafai kabisa,"

PIA SOMA
- LIVE - Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025, leo Juni 13, 2024 Bungeni, Dodoma
Huyo Mwigulu anafaidika nini na huo muungano?Au anaongea tu ili aitwe mzalendo-mjinga?
 
Back
Top Bottom