Mwijaku acha kushika mikono wake za watu unapoendesha kipindi chako

Mwijaku acha kushika mikono wake za watu unapoendesha kipindi chako

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Wakuu Kwema!

Vijana katika utafutaji ni vizuri kuelekezana ili kufanya kazi zetu zizidi kuwa na manufaa. Katika hilo, nimeona nimshauri na kumuelekeza Ndugu Mwijaku kuwa aache Kushika Mikono wake za watu anapoendesha kipindi chake yeye na Ndugu Soudy.

Hii tabia anaweza akaiona ni yakawaida lakini Kwa upande mwingine inaathiri kazi yake hasa Kwa Watazamaji, pia hata Kwa Wale anaowahoji.

Mwijaku unapomhoji mtu hasa mwenye jinsia ya kike, haupaswi kumshika Mkono, labda iwe ni salamu tu.

Lakini wewe, unawang'ang'ania Wadada wa watu licha ya wao kujaribu kujinasua kwenye mikono yako.

Haipendezi, na kisaikolojia mtu anayeongea huku anamshika mtu mwingine ni kwamba anatumia nguvu kumshawishi.

Lakini pia, Kisaikolojia, Mtu anapoongea huku akipendelea kutumia mikono yake kumshika mtu wa jinsia nyingine wakati wa mazungumzo inaashiria anaongozwa na hisia za mapenzi zaidi.

Kwa mwanaume, ni kwamba mtu huyo anapenda wanawake, na msukumo wake wa kihisia umezidi kupitiliza mpaka anashindwa kujizuia ndio maana anaongea huku akitumia mikono kumshika mwanamke.

Mwijaku, kipindi chako kinaweza kikawa ni kizuri kwani Kwa jamii yetu ya kitanzania kipo relevant kutokana na kuwa Watanzania wengi wanapenda kujua habari za watu wengine. Lakini embu fanyia marekebisho kidogo kwenye suala la uendeshaji wa kipindi, usimshike mtu hasa WA jinsia nyingine iwe aliyeolewa au asiyeolewa.

Soudybrown yeye anajitahidi Kwa nafasi yake. Wewe unachoharibu ni kipengele kimoja nilichokitaja, usishike shike wanawake za watu Mikono.

Ni ushauri tuu!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Morogoro
 
Mkuu alimuhoji mkeo nini? Af hii habari bila ushahidi ni “wei chai” ama chai ya kichina

Ukiwa na akili limited ni rahisi kuuliza maswali Kama ulilouliza.

Kuhusu ushahidi, Kwa wanaofuatilia vipindi vya Wazee wa mbanga wanajua nazungumzia nini.

Kama wewe sio mfuatiliaji, nafikiri hii imekupita
 
kumbe unamwongelea mwijaku .....mi nilidhani mw&ig*ulu
 
Kipindi chake kinaitwaje na saa ngap kinarushwa taicon wa fasihi.
 
Acha hizo mleta mada mbona Wanawake wenyewe hawalalamiki? Au nawe ni mmojawapo ulioshikwa mkono na Mwijaku?

Angeshika kiuno au kalio ingekuwaje si ungemfungulia kesi ya ugaidi?

Watanzania tuna utamaduni wa kushikana mikono wakati wa kusalimiana,kucheka,kuagana,kupeana pole nk
 
Acha hizo mleta mada mbona Wanawake wenyewe hawalalamiki? Au nawe ni mmojawapo ulioshikwa mkono na Mwijaku?

Angeshika kiuno au kalio ingekuwaje si ungemfungulia kesi ya ugaidi?

Watanzania tuna utamaduni wa kushikana mikono wakati wa kusalimiana,kucheka,kuagana,kupeana pole nk

Karibu.
 
Mi mwenyewe nilikuwa nachukulia poa , sababu ya maisha ya chuo ya extremely socialization kat ya jinsia mbili tofaut bila kuhusisha Hsia za mapenzi, hata hvyo nimekuja kugundua sio tabia nzur Kwa upande wa mke wa mtu , ni vigumu mwanamke kureact Ila Inaleta picha mbaya Sana kwenye jamii hasa kwa Mme wake ....!!! Ushauri mzuri Ila anajifanya mjuaji na ana kiburi na tabia zake za kibwax
 
Mi mwenyewe nilikuwa nachukulia poa , sababu ya maisha ya chuo ya extremely socialization kat ya jinsia mbili tofaut bila kuhusisha Hsia za mapenzi, hata hvyo nimekuja kugundua sio tabia nzur Kwa upande wa mke wa mtu , ni vigumu mwanamke kureact Ila Inaleta picha mbaya Sana kwenye jamii hasa kwa Mme wake ....!!! Ushauri mzuri Ila anajifanya mjuaji na ana kiburi na tabia zake za kibwax


Mdada anamtoa Mkono, yeye anang'ang'ania, mume anamtoa Mkono kidizaini ili kipindi kisiharibike, bado Mwijaku hajiongezi.

Siku akipigwa makofi asijesema hakuambiwa
 
Wakuu Kwema!

Vijana katika utafutaji ni vizuri kuelekezana ili kufanya kazi zetu zizidi kuwa na manufaa. Katika hilo, nimeona nimshauri na kumuelekeza Ndugu Mwijaku kuwa aache Kushika Mikono wake za watu anapoendesha kipindi chake yeye na Ndugu Soudy.

Hii tabia anaweza akaiona ni yakawaida lakini Kwa upande mwingine inaathiri kazi yake hasa Kwa Watazamaji, pia hata Kwa Wale anaowahoji.

Mwijaku unapomhoji mtu hasa mwenye jinsia ya kike, haupaswi kumshika Mkono, labda iwe ni salamu tu.

Lakini wewe, unawang'ang'ania Wadada wa watu licha ya wao kujaribu kujinasua kwenye mikono yako.

Haipendezi, na kisaikolojia mtu anayeongea huku anamshika mtu mwingine ni kwamba anatumia nguvu kumshawishi.

Lakini pia, Kisaikolojia, Mtu anapoongea huku akipendelea kutumia mikono yake kumshika mtu wa jinsia nyingine wakati wa mazungumzo inaashiria anaongozwa na hisia za mapenzi zaidi.

Kwa mwanaume, ni kwamba mtu huyo anapenda wanawake, na msukumo wake wa kihisia umezidi kupitiliza mpaka anashindwa kujizuia ndio maana anaongea huku akitumia mikono kumshika mwanamke.

Mwijaku, kipindi chako kinaweza kikawa ni kizuri kwani Kwa jamii yetu ya kitanzania kipo relevant kutokana na kuwa Watanzania wengi wanapenda kujua habari za watu wengine. Lakini embu fanyia marekebisho kidogo kwenye suala la uendeshaji wa kipindi, usimshike mtu hasa WA jinsia nyingine iwe aliyeolewa au asiyeolewa.

Soudybrown yeye anajitahidi Kwa nafasi yake. Wewe unachoharibu ni kipengele kimoja nilichokitaja, usishike shike wanawake za watu Mikono.

Ni ushauri tuu!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Morogoro
Huyo mwijaku ndo nani kwanza? Maana nasikia sikia tu mwijaku mwijaku mi nikawa nadhani ni dawa ya kuharisha ya kimasai, kumbe ni mtu?
 
Back
Top Bottom