Mwili wa Daktari Dismas Chami aliyekuwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ulyankulu waokotwa maeneo ya Malolo, Tabora

Mwili wa Daktari Dismas Chami aliyekuwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ulyankulu waokotwa maeneo ya Malolo, Tabora

Aramun

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2023
Posts
461
Reaction score
2,213
Mwili wa Dr. Dismas Chami aliyekuwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ulyankulu, Tabora umeokotwa maeneo ya Malolo, Tabora asubuhi ya leo. Dr.Chami aliondoka nyumbani (Kaliua) Jumatano ya September 4 na kumuaga mkewe kuwa anakwenda mjini Tabora kikazi na angerejea kesho yake. Hata hivyo hakurejea na simu zake hazikupatikana
1726312474881.png

Familia ilimtafuta kwa wiki nzima bila kujua alipo, lakini ilipofika Jumatano ya September 11 simu zake zilipatikana. Hata hivyo alipopigiwa hakupokea. Baadae alituma sms kwa mke wake iliyosomeka "Nisamehe sana, baada ya dakika chache sitakuwa nanyi duniani. Simamia kila kitu nilichokiacha. Pesa zote zipo CRDB bank, simamia watoto wasome. Kwaheri"

Baada ya kutuma sms hiyo, simu yake ilizimwa na hakupatikana tena. Polisi kwa kushirikiana na familia waliendelea kumtafuta bila mafanikio. Hatimaye leo mwili wake umeokotwa maeneo ya Malolo, ukiwa umechomwa sindano. Pembeni ya mwili huo kuna madawa mbalimbali ya hospitali ambayo inadaiwa yalitumika kujidunga/kudungwa.

Bado haieleweki kama amejiua mwenyewe kwa kujidunga madawa au ameuawa na watu waliomdunga madawa hayo. Haijafahamika pia kama sms aliyotuma kwa mkewe alituma kwa utashi wake au alikuwa chini ya shinikizo. Polisi wamesema wanachunguza chanzo cha kifo chake kujua kama kimetokana na migogoro ya kifamilia, Msongo wa mawazo, madeni, ugomvi binafsi au sababu nyinginezo. Rest easy Dr. Chami.!

20240914_133347.jpg


Credit: Malisa GJ, X Page
 

Attachments

  • 20240914_133350.jpg
    20240914_133350.jpg
    113.8 KB · Views: 10
Mwili wa Dr.Dismas Chami aliyekua Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ulyankulu, Tabora umeokotwa maeneo ya Malolo, Tabora asubuhi ya leo. Dr.Chami aliondoka nyumbani (Kaliua) jumatano ya September 4 na kumuaga mkewe kuwa anakwenda mjini Tabora kikazi na angerejea kesho yake. Hata hivyo hakurejea na simu zake hazikupatikana.

Familia ilimtafuta kwa wiki nzima bila kujua alipo, lakini ilipofika jumatano ya September 11 simu zake zilipatikana. Hata hivyo alipopigiwa hakupokea. Baadae alituma sms kwa mke wake iliyosomeka "Nisamehe sana, baada ya dakika chache sitakua nanyi duniani. Simamia kila kitu nilichokiacha. Pesa zote zipo CRDB bank, simamia watoto wasome. Kwaheri"

Baada ya kutuma sms hiyo, simu yake ilizimwa na hakupatikana tena. Polisi kwa kushirikiana na familia waliendelea kumtafuta bila mafanikio. Hatimaye leo mwili wake umeokotwa maeneo ya Malolo, ukiwa umechomwa sindano. Pembeni ya mwili huo kuna madawa mbalimbali ya hospitali ambayo inadaiwa yalitumika kujidunga/kudungwa.

Bado haieleweki kama amejiua mwenyewe kwa kujidunga madawa au ameuawa na watu waliomdunga madawa hayo. Haijafahamika pia kama sms aliyotuma kwa mkewe alituma kwa utashi wake au alikua chini ya shinikizo. Polisi wamesema wanachunguza chanzo cha kifo chake kujua kama kimetokana na migogoro ya kifamilia, Msongo wa mawazo, madeni, ugomvi binafsi au sababu nyinginezo. Rest easy Dr.Chami.!

View attachment 3095615

View attachment 3095616


Credit: Malisa GJ, X Page
Huu ujumbe umenichoma, Mungu aikomboe nchi yetu kwenye hili janga lililoshika kasi.

Hii sio Tanzania yangu!
 
Mwili wa Dr.Dismas Chami aliyekua Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ulyankulu, Tabora umeokotwa maeneo ya Malolo, Tabora asubuhi ya leo. Dr.Chami aliondoka nyumbani (Kaliua) jumatano ya September 4 na kumuaga mkewe kuwa anakwenda mjini Tabora kikazi na angerejea kesho yake. Hata hivyo hakurejea na simu zake hazikupatikana.

Familia ilimtafuta kwa wiki nzima bila kujua alipo, lakini ilipofika jumatano ya September 11 simu zake zilipatikana. Hata hivyo alipopigiwa hakupokea. Baadae alituma sms kwa mke wake iliyosomeka "Nisamehe sana, baada ya dakika chache sitakua nanyi duniani. Simamia kila kitu nilichokiacha. Pesa zote zipo CRDB bank, simamia watoto wasome. Kwaheri"

Baada ya kutuma sms hiyo, simu yake ilizimwa na hakupatikana tena. Polisi kwa kushirikiana na familia waliendelea kumtafuta bila mafanikio. Hatimaye leo mwili wake umeokotwa maeneo ya Malolo, ukiwa umechomwa sindano. Pembeni ya mwili huo kuna madawa mbalimbali ya hospitali ambayo inadaiwa yalitumika kujidunga/kudungwa.

Bado haieleweki kama amejiua mwenyewe kwa kujidunga madawa au ameuawa na watu waliomdunga madawa hayo. Haijafahamika pia kama sms aliyotuma kwa mkewe alituma kwa utashi wake au alikua chini ya shinikizo. Polisi wamesema wanachunguza chanzo cha kifo chake kujua kama kimetokana na migogoro ya kifamilia, Msongo wa mawazo, madeni, ugomvi binafsi au sababu nyinginezo. Rest easy Dr.Chami.!

View attachment 3095615

View attachment 3095616


Credit: Malisa GJ, X Page
Hizo SMS zilivyoandikwa tu unaona Kanyanga.

Zikipatikana SMS zake za nyuma labda tutaona kitu.
Exactly.

Sms fake ya kutengenezwa yenye nia ovu ya kutaka kuwaghiribu watu ili wasijue kiini halisi Cha Mauaji hayo.
Just a spinning Propaganda.

Hali mbaya kabisa Kama Hii inanikumbusha wakati ule wa nyakati za mwisho mwisho kabisa kabla ya kuanguka kwa Utawala dhalimu wa Dikteta Mobutu Sesseseko aliyekuwa Rais wa zamani wa Zaire (Sasa Congo DR), Watu wengi sana walikuwa wakitekwa na kuuawa katika Mazingira ya kutatanisha Sana kama hivi inavyotokea hivi sasa hapa Tanzania. Maiti za Watu wakosoaji wa Utawala wake zilitakapaa mitaani, kila siku Wananchi walikuwa wanaokota miili ya Watu mitaani.
Aidha, kila siku (hususani nyakati za usiku) ndege na helikopta za Jeshi zilikuwa zinatua nyumbani kwa Rais Mobutu kijijini kwake Gbadolite zikiwaleta 'Mateka' waliokusanywa kutoka katika miji na mikoa mbalimbali iliyopo kwenye nchi hiyo ya Zaire ili wàweze kuteswa mbele ya Rais Mobutu mwenyewe akishuhudia kwa macho yake na mwishowe mateka hao waliuliwa kikatili sana. But all in all, mwisho wa dhahama yote hiyo, Dikteta Mobutu aliishia kumteka hata Mkuu wake wa Majeshi (CDF) General Mahele na kumuua kikatili kama nguruwe pori, na hapo ndipo Utawala wake wa kidikteta ulipofika mwisho wake.

Watanzania tuzidishe sala na maombi kwani kunakaribia kukucha, Wakimaliza kututeka sisi Wananchi basi watageukiana wao kwa wao, kama ilivyofanyika nchini Zaire kwa Rais Mobutu.
 
Back
Top Bottom