Mwili wa DMX ukitolewa hospitali New York kwenda kwenye hifadhi ya maiti

mashabiki watakua wengi ni kizazi cha 90s hawa
samahani, hv hoja ni nini haswa hapa?

ila jamaa linapokuja suala la hardcore hipo hop hakuwa na mpinzani na mpaka watoto wa 2010 wanamuelewa
 
I wish nikuunge na my son who used that makitu for more than 20 years ila now is free.

Poleee.


X wangu ambaye ni mama watoto amekuja tumeongea usiku mzima. Nimekubali anisaidie, kesho atanipeleka kwa wataalamu. Yaani hapa, I have to do it or I will die. Nikiwaangalia watoto wangu moyo inaniuma. Yaani leo ni siku ya mwisho. Kesho inabidi nichukue hatua
 
Pole sana Pagan....
Natamani kujua vingi, nitakuuliza unifahamishe i know nothing kuhusu hivi vitu.
Pole
 
Pole sana Pagan....
Natamani kujua vingi, nitakuuliza unifahamishe i know nothing kuhusu hivi vitu.
Pole


Hivi vitu viko vya aina mbalimbali, na kila mtu ana ugonjwa wake. Ukifika hatua ya kujipiga sindano ujue hiyo ngoma ishakuwa nagwa. Wauzaji wa haya madude wanachojali ni pesa tu, wanakuua huku wanatabasamu
 
Nadhani itapendeza tukimsaidia kaka yetu pagan. Sina shaka humu kuna wataalam wa Rehab..
Tunawasihi mseme JAMBO if you are in a position to extend help.
 
Nadhani itapendeza tukimsaidia kaka yetu pagan. Sina shaka humu kuna wataalam wa Rehab..
Tunawasihi mseme JAMBO if you are in a position to extend help.


Kesho nakwenda kwa daktari wa familia, yeye ndio atanipangia wapi pa kwenda. Nakumbuka mwaka jana aliniambia njoo tuongee hili swala, matokeo ilikuwa kila akinipigia simu sipokei mwisho akaona isiweze tabu akaachana na mimi. Lakini sasa nimekubali tuanze process
 
Poleni sana. Ilianzaje anzaje na imekwendaje hadi sasa. Naomba ufunguke maana utasaidia wengi na pia itakuweka wewe free na kuanza kuchukua hatua. Pole sana mkuu
 
Poleni sana. Ilianzaje anzaje na imekwendaje hadi sasa. Naomba ufunguke maana utasaidia wengi na pia itakuweka wewe free na kuanza kuchukua hatua. Pole sana mkuu

, Mkuu kuna kipindi nilikaa Magomeni Kagera, watu niliokuwa napiga nao misele ndio bad choice
 
Mungu akutangulie kaka!
 
Hivi vitu viko vya aina mbalimbali, na kila mtu ana ugonjwa wake. Ukifika hatua ya kujipiga sindano ujue hiyo ngoma ishakuwa nagwa. Wauzaji wa haya madude wanachojali ni pesa tu, wanakuua huku wanatabasamu
Aseehh!pole sana rafiki I do hope utavuka hili janga!
 
Amen
 
👊👊
 
Jina lake linaambatana nae
 
I wish vitu unavyoongea vingekuwa kweli. Hivi vitu uviskie kwa majirani
Pole sana, nakuonea huruma sana, Ndugu wadogo kwa Baba yangu mdogo wote wameathiriwa na hiyo hali, najua nini unaoongea, Hii habari ione kwa jirani na sio kwenye famili.
Ila hatma yako iko mikononi mwako, katika maisha yangu nimejua ya kuwa hamna nisichoweza kufanya, Na hata wewe hivyo hivyo, unaweza kuacha kama ulivyoanza. Jaribu kuwa mtu wa ibada(maombi), Funga, funga inafungua vifungo vingi sana, ukiweza kufunga kwa mwezi unatoka hapo.
 
Nakumbuka nilianzaga hii kitu way back 1997 nikiwa nasoma naishi kinondoni kwa manyanya, enzi hizo pamechafuka sana KINO but mshua aliniwahi nikiwa early stages akanihamisha mkoa ndio ikawa pona yangu ila nshapoteza cousin kwa hii kitu addict.

Ni starehe ambayo mtumiaji ukimuwekea unga hapa na Demu mkaaaaaliiiii pembeni atachangua ngada coz raha yake huwezi isimulia ile stim aisee.

Pole mkuu tafuta solution mapema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…