Mwili wangu huwa unanuka mpaka sina raha ya kuishi

Mwili wangu huwa unanuka mpaka sina raha ya kuishi

Mkuu kama una hilo tatizo sema nukusaidie utapona ndani ya week Tatu. Namshangaa anayetafuta ushauri kaebda mazima. Ni dawa za uhakika. Mimi sio mshirikina mkuu. Ila ukijichanganya siyo mbaya pia
Mi natafuta dawa ya kumtengeneza MTU kma uko vizuri tutafutane
 
mkuu oga jipake mafuta yasiyokuwa na harufu kali sana... pia punguza vyakula yenye viungo vingi kula vyenye viungo vya wasatni .. halafu watu wa tiba madala wanaweza kukueleza na matunda ya kutumia au juice kusafisha taka mwilini mwako.. make sure unavaa chupi za cotton usirudie chupi,,, shave kuwe safi kupake mafuta ya vaselini kuwe kuzuri..........halafu kama unakunywa pombe au unavuta sigara embu achana na ulabu kwa muda ,.. lazima uwe mwaaa

Wewe ni daktari? Nataka nije unitibu.
 
Pole sana, yalimkuta jamaa yangu chumba alichokitumia chuoni nasikia hadi leo (10 yrs)
 
Usifanye chochote nenda hosipitali. Hakuna pafyumu ya kupaka sehem za siri. Ila unaweza kutumia deodorant inayokausha inakuwa kama na ute flani wa yai. Ukiipaka inazuia kulowana huko chini. Pia hizo ni dalili za fangasi. Kama unaogopa basi chikua vidonge vinaitwa gsufluvin unakunywa kimoja mara mbili kwa siku. Kwa muda wa wiki 6pia wakati huo nenda hospitali ya serikali wambie wakupe whitefield utakuwa unapaka muda wote unaokunywa dawa mpaka miezi 3
 
Yawezekana ni fungus. Jaribu kutafuta matibabu.

Njia nyinhine uwe unaoga maji ya ugali. Yaani baada ya kupika ugali loweka sufuria kwa muda mrefu hadi maji yapate harufu hiyo ya ugali, wastani masaa manne 4, kisha baada ya kuoga kwa medicated soap hasa Securex, ukimaliza kujisafisha na maji masafi., oga sasa na hayo maji ya ugali mwili mzima hasa sehemu hizo. Kisha acha ukauke bila kujifuta na taulo.
 
Pole sana. Nashauri yafuatayo:
1. Nenda hospital
2. Fuatilia tiba ya Mkuu Rais 2020 ( Mchawi/Mganga)
3. Tumia maji ya moto yenye limao glasi moja kwa 2weeks, kila asubuhi.
4. Kunywa supu ya kitunguu swaumu bakuli moja daily kwa 1week hii itabadili harufu yako kuwa ya kitunguu
Hatua zote kama majibu ni zero basi ingia kwenye maombi ... Kwani binadamu si watu wema. Hizo ni hatua zilizo chukuliwa na jamaa zangu zikawasaidia.
 
Habarini wanafamilia,

Utotoni mwangu nilikuwaga hata sinuki lakini nilivyojiunga na shule ya boarding nikaanza kunuka kuanzia form 2. Basi nimekuwa ninanuka mpaka leo nimeishakuwa mtu mzima na ninategemea kuoa. Kazini kwangu hata kabla sijapishana na mtu basi huyo mtu ataanza kuziba pua na kama yuko mbali basi akiniona tu utamwona anatema mate au kuvuta koromeo la koozi kuashiria kwamba anajiandaa kukabiriana na harufu yangu mbaya.

Nimejitahidi sana mpaka kufikia kuzoea ratiba ya kuoga mara 3 kwa siku lakini wapi, nikioga nina kuwa salama kwa masaa mawili ya mwanzo lakini baada ya hapo ninakuwa kero kwa watu. Harufu mbaya inayowatesa wenzangu mimi siisikii lakini wao inawashinda. Nimekuwa nikiharibu siku za watu kila mara.

Sehemu ambayo nimekuja kugundua kwamba inato harufu hii ni kwenye mapumbu (Samahani kwa kutumia lugha kali lakini sina namna ya kuweka tafsida ya hili neno bila kuharibu maana). Nimekuwa nikiosha sana pumbu zangu usiku, mchana na asubuhi lakini haija saidia. Hakuna mtu duniani anayejitahidi kuoga kama mimi. Kuna ndugu zangu wengine anaweza asioge hata wiki lakini mimi nikioga muda huu baada ya masaa 3 ninanuka balaa. Mimi ni mtu mwembamba tu na wala umbo langu sio kubwa na wala sina mafuta mafuta lakini, hii harufu inaninyima raha ya kuwepo duniani.

Mimi ni mpole ukiniona lakini kiuhalisia mimi nilikuwaga mtundu sana na huu upole wangu wa sasa ni siri yangu, upole wangu ni kwa sababu ninanuka kwa hiyo sina amani ya kujitutumua mbele ya jamii inayo nizunguka. Inanibidi niwe mpooooole na tulivu hata muda mwingine nimekuwa mtu wa ndio mzee, sawa mkuu, ilimradi tu kuharakisha mtu asisimame na mimi kwa muda mrefu akaisikia harufu yangu kali akawa ananikimbia kwenye korido. Marafiki zangu wa kweli ambao tumeishi nao muda mrefu mpaka nimefanya pua zao kuzoea harufu yangu na wala hawaoni kama ninanuka, ukiwauliza watakwambia jinsi mimi nilivyo mtundu, mcheshi na mpenda sifa tena machepele kweli kweli dakika mbili mbele, lakini ni kwa hawa tu ambao kwao mimi sinuki bali ni shujaa na roll model wao pia.

Wadau naombeni msaada sana katika hili ili niweze na mimi kujihisi ni mtu wa kawaida kwa kuondokana na hili tatizo nguli katika maisha yangu.

Natanguliza shukrani zangu kwenu.
kiufupi wewe haunuki. tena bora ungesema unanuka kwapa lakini siyo kengele. una ugonjwa wa kisaikolojia unaitwa olfactory reference syndrome (ORS). ni aina ya delusions (false beliefs). Reference maana yake una refer tabia za wengine na kunuka kwako. mtu akikihoa, akijishika pua, akipiga chafya, akifungua dirisha, au hata mbwa kubweka wewe unahisi ni kwasababu unanuka.

wengi wenye hii shida unakuta hiyo harufu wao hawajawahi isikia. wengi huuliza watu wanaowaamini ikiwa wananuka, wakiambiwa hawanuki wanaona watu hao wamewadanganya kwa kuogopa kuwaambia ukweli. wengi huoga au kupiga mswaki mara nyingi,huvaa chupi au nguo nyingi na hujinusanusa. hii ishu ina haribu sana kazi, mahuiano na maisha kiujumla.

nashauri muulize mtu unayemuamini iwapo unanuka na jielimishe zaidi kuhusu ORS.
 
Mkuu nenda hospitali na kisha tembelea beach mara kwa mara ukaoge yale maj bahari
 
Utakuwanna fungal infection inaitwa Tinea Cruriz, ni common sana kwa wanaume kutoka na joto ,huwa ijakuwa kati ya mapaja na mapumbu ila yako itakuwa chronic, huwa inatibika kirahisi kwa dawa za kupaka ziko nyingi sana na kwa bei rahisi kabisa, ikiwa chronic itakubidi unywe dawa za kunywa, wala sio ishu kubwa hiyo. Nenda kamuonape Daktari Mohammed Amiti
 
Mohamed amiti hata usiende hospitali. Nakuelekeza dawa ukaitumie na mrejesho utauleta mwenyewe hapa baada ya week Tatu mpaka nne.
Mdogo Wangu alisumbuliwa sana na hilo tatizo ila sasa limekuwa ni historia kwake
 
Kuna zile strong perfume ambazo ukijipulizia kwenye shati au suruali inakaa hata wiki bado ipo hata ukifua shati au suruali, ila ni expensive kidogo zinaenda mpaka laki moja
Ukipuliza hyo umeharibu kabisa
 
Pole sana mkuu...
Umejaribu kuwaona madaktari? Wanaweza wakawa na njia ya kukusaidia.
Kuna rafiki yangu alikua anatafuna vitunguu saumu, kuanzia chumba chake hadi yeye mwenyewe mkipishana njiani alikua ananukia kitunguu saumu. Jaribu kutafuna vitunguu saumu labda harufu itapungua.
Pia nunua sabuni ya kuogea emperial... Ina harufu nzuri na hubaki mwilini.
Tafuta zile poda za watoto, zile za zamani zenye chupa ya blue. Hii poda inaziba sana harufu. Ukitoka kuoga jikaushe vizur, paka mafuta ya mgando haswa kwenye sehemu nanazosem zinatoa harufu alafu paka hiyo poda... Usiogope kujikandika.
Nunua spray au perfume yenye harufu kali, achana nao watakaoumizwa na harufu hiyo. Isiwe kali sana ikawa kero. Kuna spray moja inaitwa "BOD", ina harufu nzuri na haitoki kwenye nguo ata ukifua.

Cha ziada ni endelea kujiweka msafi, usirudie kuvaa nguo na be cheerful
 
Pole, cha kwanza jikubali.Tambua kila mwanadamu ana kilema(udhaifu) katika sehemu ya mwili wake,au akili awe amejijua au la.Pia waone wataalamu wa afya ikishindikana omba au uombewe kwa jina la Yesu nahisi ni pepo limekuchafua.
Amina! Yaani huyu ata sishangai! Kuna ndugu yetu tulikua tunaishi nae, akitoka bafuni huwezi ingia hiyo harufu itakayokua imebaki humo... Yaani alikua ananuka hadi nyumba nzima ikawa na harufu yake, akikaa kwenye kochi sebleni mwingine hawezi likalia. Cha ajabu nimekutana nae juzi kati kwenye harusi ya bro mwingine, hana hata kiarufu zaidi ya kunukia spray. Hii hali itaisha mkuu.
 
Back
Top Bottom