Mwingira, Mwingira, mbona kama hujui maandako aau Biblia unayotumia ni tofauti na ninayoisoma,kumbuka katika Kitabu cha Mithali 17:13 Neno la Mungu linasema "Yeye arudishaye mabaya badala ya mema ,Mabaya hayataondoka nyumbani mwake"
Wewe kama Mtumishi wa Mungu hupaswi hayo uanyoyasema kwa mtumishi mwenzako achilia mbali muumini wa kawaida.
Kumbuka katika Neno la Mungu tunaonywa sana ukijidhania kuwa unajua neno hujui bado bali wanaompenda Mungu wamejulikana naye(1Wakorintho 8:2-3) hivyo usidhanie kutumia Neno la Mungu kuwa unalifahamu sana kuliko wengine umepotoka.
Mwingira kwanini unakuwa kwazo 2Wakorintho 6
"Tusiwe kwazo la namna yeyote katika jambo lolote ili utumishi wetu usilaumiwe"
Kwanini unaruhusu kuwa kwazo kwa wengine na kupata lawama juu ya utumishi wako.
Katika Neno la Mungu mambo mengi yamekatazwa kwa hawa watumishi wa Mungu lakini ndiyo kama vile wanayafumbia macho
Tito 1:7-9 "Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno kwa kuwa ni wakili wa Mungu asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake asiwe mwepesi wa hasira,asiwe mgovi asiwe mpenda mapato ya aibu bali awe...........................
Lakini haya ndiyo tunayashuhudia kwenu nyie watumishi mnasimama wapi?
Katika kitabu cha Yakobo napo kuna mambo mengi tu ya kujifunza.
tumeonywa juu kuwalaani watu walioumbwa kwa sura na mfano wa Mungu
Yakobo 3:9 "kwa huo twamhimidi Mungu baba yetu,na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu"
Unatumia ulimi huo kumlaani mtu badala ya kumbariki tena Mtumishi mwenzako,na huo huo unatumia kumwomba na kumtukuza Mungu.
Mwingira na Kakobe kumbukeni tumekuwa tukiona upendeleo unaofanyika toka kwa watumishi kwa kuwajali wenye navyo.
ila kwa babu sijasikia upendeleo na ni hiyo shilingi 500 ni kwa wote
Yakobo 2:1 "Ndugu zangu,imani ya Bwana wetu Yesu Kristo ,Bwana wa utukufu,msiwe nayo kwa kupendelea"
ndiyo hayo kama si mwana efatha,au huko kwingineko unaonekana hufai kupata baraka zilizopo kwneye neno,ndiyo maana kwa babu wala hajapendelea uwe nayo ,mpagani utapata huduma ya uponyaji.
ONYO
Kumbuka Mungu hawezi kuwaacha watu wake wateseke hata siku moja katika mikono ya watumishi walo kondoo na kuwatelekeza.
Kwa wale wasomaji wa Bibli wakasome Ezekiel 34:1-31
Ila nitanukuu michache kwa faida ya wengine mstari wa 4 unasema
"wagonjwa hamkuwatia nguvu,wala hamkuwaponya wenye maradhi,wala hamkuwafunga waliovunjika............
Kweney mstari wa 10 Neno linasema Bwana MUNGU asema hivi;Tazama,mimi ni juu ya wachungaji;nami nitawataka kondoo zangu mikononimwao;nami nitawaachisha hiyo kaziya kwalisha kondoo;nao wachungaji hawatajilisha wenyewetena;nami nitawaokoa kondoo zanguvinywani mwao,wasiwe tena chakula chao.
watumishi wengi wamekuwa wakichukulia matatizo ya watu mtaji hasa magonjwa,bila kujua kuwa hilo Mungu halimfurahishi.
Hivyo mkumbuke kama mlitegemea kuwanyonya tu kondoo wa Bwana badala ya kuwatumikia hawezi kuruhus hali hiyo tena.
Loliondo ilikuwa eneo ambalo hakuna mtanzania ambaye angependa kuishi huko ndiyo maana hata kaya zipo chache sana 500,ila leo tuanona jinsi gani wingi wa watu huko toka mataifa mabalimbali wanaelekea huko
Isaya 60:15-22
"Na kwa kuwa umeachwa na kuchukiwa hata hapana mtu aliyepita nadani yako (Loliondo/Babu)
nitakufanya kuwa fahari ya milele
Furaha ya vizazi vingi
Utanyonya maziwa ya mataifa(mataifa mbalimbali yanaenda huko)
Utanyonya matiti ya Wafalme(viongozi wengi wanaelekea huko)
MWISHO NATAMKA BARAKA KWA LOLIONDO NA BABU
Isaya 54:17
Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu juu yako utahukumiwa kuwa mkosa.Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA,na haki yao inayotoka kwangu mimi asema BWANA"
SIFA NA UTUKUFU NI KWA MUNGU KWA HUDUMA YA UPONYAJI INAYOPATIKA LOLIONDO
NA KILA MWENYE PUMZI ASEME AMEEN