Mwingira wa EFATHA awaita Viongozi ya Serikali ni washenzi

Mwingira wa EFATHA awaita Viongozi ya Serikali ni washenzi

Haya anayasema saa hii wakati anatoa mahubiri yake hapa kanisani.

Anadai ameonyeshwa serikali wamemtuma mtu aje hapa kanisani ku spy ndipo alipoanza wewe uliyetumwa ni mshenzi na mambo yako ni ya kishenzi sababu waliokutuma ni washenzi.

Haya ngoja nirudi kupata mahubiri nitarudi tena
Sasa Mtu akifanya tabia za kishenzi na akang'amulika huoni huo ni ushenzi unakuwa sifa.Kama unaona ushenzi ni tusi basi achana na kufanya huo ushenzi!
 
Haya anayasema saa hii wakati anatoa mahubiri yake hapa kanisani.

Anadai ameonyeshwa serikali wamemtuma mtu aje hapa kanisani ku spy ndipo alipoanza wewe uliyetumwa ni mshenzi na mambo yako ni ya kishenzi sababu waliokutuma ni washenzi.

Haya ngoja nirudi kupata mahubiri nitarudi tena
Neno "serikali" is too universal...

Hujui kuwa hata shetani ana serikali yake...?

It's obviously, aliyetumwa pia anatoka kwenye hiyo serikali ya kishetani...!!
 
UKWELI KUHUSU WABUNGE KINA DADA NA KUPENDA MANABII KUTAFITA UPAKO NA UTAWALA
Kwa kutumia udhaifu huu Mwingira kakung'uta wake za watu wengi ,akina dada wakiwemo wabunge orodha inatisha lakini ukitaka kufahamu zaidi fuatilia ndoa na mdogo wa mke wa Gray Mgonja .Ndoa hiyo ilipaswa kufungwa Efatha lakini ikatishwa baada ya bi Arusi kufanyiwa deliverence kama hiyo. Familia ya Mgonja iliwahikufungua mashitaka kule USA lakini watawala wakazuia kipindi kile yupo Hazina!!!


Hata hivyo hii ni sehemu ya mgogoro uliojitokeza Mhakama kuu kanda ya DSM katika kesi namba 266/2010 iliyofunguliwa na Nabii Josephati Mwingira , mlalamikaji(Mwingira )anamulalamikia Eliya Hubert mbuya kuvunja mkataba wa kumupa sehemu ya kiwanja katika plot namba 548(a) eneo la Kawe Beach ambapo Mwingira amejenga nyumba ya thamani ya

Tshs 1,000,000,000 na kuishi humo.
Katika kesi hiyo Mbuya anatetewa na Wakili Michael Ngalo ambaye anajibu malalamiko ya Josephate Mwingira kama ifuatavyo:

That the plantiffs claim and assertion that he is a holy spiritual leader, apostle and prophet are matters whose varaciy and authenticity are only known to God and cannot be admitted or denied by the defendant but the defendant aver that the plantiff is a Founder and oversee of Efatha Ministry with a tittle of a Managinging director and also a trustee and chairman of its board of trustee of the Registered Trustee of Efatha ministry who in his personal capacity sexually assaulted and raped the Defendants wife and defiled the defendant house on plot number 548 Kawe Beach Kinondoni DSM in despite of his claim for holiness as a spiritual leader .

Wakili Michael Ngalo anaendelea katika Kipengele Cha nane kama ifuatavyo:
That in the meantime and then Unknown to the Defendant the Plantiff had sexually assaulted and raped the Defendant wife in the defendants house while the Defendant was at his place of work and managed to bribe the defendants wife into silence about the incident and later an adulterous association persited between the Plaintiff and the Defendants wile for a period of three years until God compelled the Defendant wife to make confession to the defendant about the adulterous association with the Plantiff.
Kwa ufupi Mbuya anamtuhumu Mwingira kuwa amekuwa ana mbaka mkewe aitwaye Bertha Evarist Mbuya kwa nyakati tofauti tangia mwaka 2003 hadi alipotubu mwenyewe mwaka 2009.
Maelezo yake yanaonyesha kuwa , Mbuya na Mkewe walijiunga na Kanisa la Efatha na kujitoa katika huduma hiyo kwa kuchangia michango mingi ikiwa ni pamoja na kutoa uwanja katika nyumba aliyojenga Mwingira.Mbuya anasema, mwaka 2009 mkewe( Bertha) alitubu kwake na kumwambia kuwa siku moja mwaka 2003 akiwa kazini ,yeye (mke) alizini na Nabii Josephati Mwingira ndani ya nyumba yao iliyopo karibu na nyumba ya Mwingira!!!
Bertha alimweleza Mbuya kuwa aliamua kutubu baada ya kupata ugonjwa mbaya uliomusumbua kwa muda wa miaka mitatu ambapo katika kumwomba Mungu alisikia sauti ikimwambia ili apone ni lazima atubu dhambi ya uzinzi kwa mumewe.
Baada ya kusikia hayo Mbuya na mkewe walikwenda kumukabili Nabii Josephati Mwingira na kumukuta yupo na Mkwewe (Elikunda Mwingira). Bertha aliweka wazi uzinzi aliofanya na Mwingira mbele ya kikao cha watu wane ambapo Mke wa Mwingira alikiri kusikia habari za uzinzi huo na Bertha alomba radhi kwa Elikunda (mke wa Mwingira) ambapo alimusamehe lakini Mwingira hakujibu chochote.
Nimesoma Kitabu cha wito wa Nabii Josephati Mwingira kaitka ukurasa wa 3 kichwa cha habari Safari ya kwenda Mbinguni katika eneo hilo Nabii Mwingira anasema kwamba :

Malaika mmoja akaniongoza ,tukaenda mpaka kwenye lango. Tuka ingia katika lile lango na kupelekwa moja kwa moja alikokuwako BWANA YESU. Nikaona watu wengi sana wako kule; siyo Malaika ila ni watu kabila mbali mbali Waafrika na Wazungu. Sikuongeanao ila katika hali ya kuangalia angalia, nikawatambua Ibrahim, Mussa na Eliya. Kulikuwa na hali ya kumwelewa kila niliyemwona kwamba huyu ni furani na huyu ni Fulani. Kisha akanipeleka kwa BWANA YESU.
Ukitafakari simulizi hizi za Nabii Mwingira unaweza kujua kuwa aliyekuwa anaandika alikuwa bada na ulevi kichwani !!!
Kwa mujibu wa bible , Ibrahimu, Mussa na Eliya walitoweka muda mrefu sana kama ya Kristo kuja duniani na hata Mwingira haja zaliwa sasa ni ajabu sana kuona kuwa miaka ya 2000 Nabii Mwinira alikwenda Mbinguni na kuwatambua hao kwa kuangalia angalia badala ya kutambulishwa!!!
Mtu usiye mjua wala kumuona huwezi kumutambua bali kutambulishwa hata mtu mlevi na Nabii wa Uongo hawezi kukosea hatua hii. Sasa Mungu ametupa Ufunuo wa Kuwapima Manabii wa Uongo na kuwa kuwahoji.

Bibilia inasema tutamtambua mtu kwa matendo yake ya Mwili ili kubaini Roho ilimo ndani yake.

Kutokana na maombi ninayofanya sasa hivi , Roho wa Bwana amenifunulia mambo mazito ndani ya Wito wa Mwingira , ambayo ningependa Makanisa wayajue.

Tarehe 23/9/1978 ,Bi Mary Mtetemela na Stivin Weston Mtetemela walifunga Ndoa yao katika kanisa la katoliki Mkoa wa Kilimanjaro, Parokia ya KILEMA ambapo ndoa hiyo ilifungwa na REV Joseph Babu.
Katika ndoa hiyo Mch Christopher Mtikila alikuwa best man na Catherin Adolf alikuwa msimamisi wa Kike. Muda mfupi baada ya kufunga ndoa hiyo , Wanandoa walianza kuishi pamoja karibu na nyumba ,familia ya Mzee Adolf Einstein (mwenye asili ya Ujerumani) ambaye ni baba yake Catherini,
Catherini na Bi Mary walikuwa marafiki wakubwa kiasi cha Mary kumuchagua Catherini kuwa msimamizi wa ndoa yake.

Kipindi hicho ambacho Catherini alikuwa hajaolewa na anaishi karibu na Wanandoa hao alianza uhusiano wa Ngono na mume wa Mary na kuleta Vurugu kubwa.

Katika vurugu hizo tarehe 14/11/2003 Mary alikatwa mapanga katika hali ya kupambana ambapo mtuhumiwa namba moja alikuwa Catherini na taarifa hizi ziliripotiwa polisi Mwanza.

Baada ya hapo , Stivin Weston Mtetemela na Caherini Adolf waliamua kuhamia DSM na baadaye kujijenga Kibaha.
Bw stivi Weston Mtetemela anatajwa kuwa Mkandarasi na mjenzi wa Viwanja vya ndege, ambapo alijenda viwanja vya ndege kikiwemo ,kile cha Dodoma, msoma,Zanzibar na Songosongo.

Mr Mtetemela alikuwa na kampuni inayoitwa MILO Construction iliyosajiriwa tarehe 30/6/1979 na mwaka 2005 ilipata tenda ya kujenga kanisa la Efatha (Kwa mjibu wa Kibao cha ujenzi kilichowekwa Efatha), linalo ongozwa na anayejiita Nabii na Mtume Mwingira na kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo kabla hajaanza kuugua ugonjwa wa figo na kukimbizwa India mwaka 2008.
Katika kipindi chote cha ujenzi huo Catherini na Mtetemela walikuwa wanaishi kama mke na mume na Mwingira aliwabariki.
Wakati Mtetemela akiwa hoi kitandani , Catherini alifanya mambo mawili mazito kwa kushauliwa na Nabii Mwingira.
Moja walibadili jina na umiliki wa Kampuni ya MILO- Construction na kuita ACASTE-Construction (Afred Catherin Aldof.) ambayo mpaka sasa anasema ni mali yake.

Mwaka huohuo , wakati Mtetemela alikuwa hajitambui, catherini alifanya njama za kufunga ndoa kupitia kanisa la Efetha ambapo Mwingira alitoa maelekezo kwa catherin kwenda kutengua ndoa ya Mary na Mtetemela ambapo walikenda Baraza la Maaskofu kurasin na kuwakuta wahusika huku Mtetemela akiwa ameachwa kwenye gari akiwa hajitambui.
Catherin aliwakilisha vyeti vya ndoa kati ya Mary na Mtetemela ili kuvunja ndoa hiyo ili apate kufunga yeye na Mtetemela.

Maaskofu wa Katoliki waligoma kutii maagizo hayo kwa maelezo kuwa ni kinyume na bibilia lakini pia wakahoji kuwa ni kwa nini maamuzi hayo yanafanywa huku mwanaume akiwa hajitambui??
Baada ya hapo, Catherin alirejea Kwa Mwingira na kumupa taarifa hizo zilizo mhuzunisha. Nabii Mwingira aliamua kufungisha ndoa hiyo kinyume na bibilia na utaratibu wa serikali pia.
Tarehe 18/7/2009 Stivin Weston Mtetemela alifariki dunia na mazishi yake yalifanyika tarehe 21/7/2009 eneo la Kibaha.
Aliyeongoza mazishi hayo ni Nabii Josephati Mwingira na katika mazishi hayo alimuzia Mary Mtetemela kuweka udongo Kwenye kaburi na kumutambua Catherin kama mjane halali wa marehemu, mwenye masikio na asikie maneno haya!!!
Hivi ninavyo zungumuza Catherini amekalia mali zote za Marehemu na mwanzono mwa mwaka huu alimutukana Mch mtikila matusi ya nguoni wakati anamsihii aachie mali za marehemu. Catherini anajieleza kuwa yeye ndiye mke halali wa Mtetemela na kwamba alianza kufanya naye mapenzi wakati yeye yupo form-two. Wakati wa mabishano hayo , Catherin alimtukana Mtikila centra polis DSM Mbele ya SSP PILI ambapo hadi naandika makala haya ametupwa rumande na yupo SEGEREA kwa kudharau taratibu za dhamana katika kesi kutukana matusi ya nguoni namba 648/2012 mahakama Ilala. Huyu ndiyo muumini wa Mwingira!!!
Baada ya kupata ushuhuda huu nimeanza kupata picha kuwa YESU yu Mawinguni wapendwa tujiandae kwa unyakuo kwa kujitakasa na kuombeana!!!
Ni jambo la kushangaza kuwa Mwingira ambaye aliwahi kuwa Mkatoliki anadharau ndoa za Kikatoliki na hapa ipo hatari ya wanawake wanao abudu efatha na waliofunga ndoa kanisa Katoliki wakaona ndoa zao hazina maana mbele ya Mwingira na wakaanza kufikiria vinginevyo.
Ukweli ni kwamba KILA AMWACHAYE MKEWE NA KUOA MWINGINE AZINI NA AMUOYE YEYE ALIYE ALIYEACHWA NA MUMEWE AZINI . Tunaweza kupata maneno haya katika vifungu vifuatavyo ili kuimarisha ndoa zetu na kuwa tayari kwa safari ya kwenda Mbinguni na siyo kwa Mwingira kwani hana Mbingu!!!
(1Wakor 7:10-11, Mathayo 5:32, Mathayo 19;9, Luka 16:18)
Kumbuka kushika sana neno kipindi hiki cha dalili za Sodoma na Gomora.
Nimeamua kuishia hapa na sasa naenda kwenye maombi ili kupata mengi zaidi, Mungu awabariki sana.
Duh..!!
 
Mali za Nabii Mwingira zachafua hali ya hewa

Toleo la 2575 Sep 2012











257_mwingira.jpg





  • Wanakijiji wadai kukatwa masikio, ‘kubabuliwa' mwili kwa vyuma vya moto
  • Ni shamba alilonunua kwa mamilioni ya shilingi





HALI si swari kwa wanavijiji vya jirani na Shamba la Mifugo la DAFCO-Malonje, mkoani Rukwa lililouzwa kwa Nabii Josephat Mwingira wa Kanisa la Efatha, uchunguzi wa Raia Mwema, umebaini.
Baadhi ya wanavijiji hao wanadai wamedhalilishwa na kutendewa vitendo vya kikatili. Kati ya vitendo hivyo ni pamoja na baadhi yao kukatwa masikino na kuunguzwa sehemu mbalimbali za miili yao kwa kutumia vyuma vya moto.
Shamba hilo ambalo liliuzwa kwa Nabii Mwingira kwa zaidi ya shilingi milioni 600 likitajwa kuwa na ukubwa wa hekta 15,000, mbali na Kijiji cha Malonje linazungukwa na vijiji vingine vya Ulinji, Sandulula na Sikaungu, ambavyo vipo Kata ya Molo, Manispaa ya Sumbawanga.
Taarifa za kiuchunguzi zinabainisha kuwa wanaofanyiwa vitendo vya kikatili ni wanavijiji ambao wamekuwa wakipita ndani ya shamba hilo na hata wengine wanaoendesha shughuli za kilimo.
Uchunguzi wa timu ya waandishi wetu umebaini kuwa mtu yeyote hufanyiwa vitendo hivyo bila kujali umri wake wala jinsi. Tayari mwanakijiji mmoja amekwishakatwa masikio na wengine kuadhibiwa kwa kuchaniwa nguo na baadhi kutandikwa viboko.
Katika mlolongo wa adhabu hizo, wamo pia wanaodaiwa kukatwa mapanga, kuunguzwa kwa kutumia vyuma vya moto mwilini. Kasoro iliyojitokeza baada ya uchunguzi wa waandishi wetu kuhusu matukio hayo ni kwamba, sehemu kubwa ya waathirika wa matukio hayo hawakuwa tayari kuripoti katika vyombo vya dola kwa hofu ya kuogopa kuteswa zaidi na baadhi ya walinzi wa shamba hilo.
Mmoja wa wananchi hao ambaye ni Mkazi wa Kijiji cha Malonje, Nuru Togwa (30), amemweleza mwandishi wetu kwamba yeye ni mlemavu kwa sasa, baada ya kukatwa masikio yote mawili kwa wakati mmoja kutokana na kudaiwa kupita ndani ya shamba hilo.

"Kwa sasa ni zaidi ya miaka mitano tangu nilipokutana na ukatili huo ambao sitokuja kuusahau maishani mwangu. Nilikuwa nikitoka Ziwa Rukwa wakati wa asubuhi nikiwa nimebeba kikapu chenye samaki wabichi kuelekea mjini Sumbawanga.

"Sumbawanga ndiko kwenye soko la samaki, lakini nikiwa njiani ghafla watu watano wakanisimamisha na kuniamuru nikae chini. Wakanitaka nitoe maelezo ya kwa nini nimepita kwenye njia zilizoko shambani humo ili hali tayari kuna zuio?

"Lakini kabla hata ya kuanza kujieleza nilianza kupata kipigo kutoka kwa hao walinzi ambao walikuwa na silaha za jadi. Wakanichukua hadi kwenye kambi yao na kuendelea kunipiga na baadaye walinifunga kamba miguuni," anaeleza Nuru Togwa.
Kwa mujibu wa maelezo yake, baada ya kumpiga na kumfunga kamba walinzi hao walimkata sikio kwa kutumia panga. Anadai walimkata sikio moja baada ya jingine kwa panga, naye kubaki katika maumivu makali na alivunja damu nyingi hadi kupoteza fahamu.


"Baada ya hapo naelezwa kwamba nilifikishwa polisi na kisha hospitali ya mkoa kwa matibabu. Baada ya kutoka hospitali niliwekwa rumande kwa kosa la kuiba ngano magunia 40 na siku iliyofuata nilifikishwa Mahakama ya Mwanzo mjini Sumbawanga.
"Kesi hiyo iliahirishwa kwa zaidi ya mara tisa mahakamani na kisha nami kuachiwa huru kutokana na upande wa walalamikaji kutohudhuria mahakamani kwa muda wote huo wa kesi,"anasema.
Anasema baada ya hapo, hakujua namna gani anaweza kusaidiwa kudai haki yake lakini baada ya siku chache alishauriwa kuwatafuta watumishi wa Kitengo cha Haki za Binadamu mkoani Rukwa na kuwaeleza kile kilichomsibu, lakini hata hivyo, walishindwa kumsaidia kama alivyotarajia.
"Mchumba wangu aliyetarajia kunioa (anamtaja jina), alinikataa na hadi sasa sijawahi kupata mchumba mwingine. Nahisi kuwa mnyonge nisiye na thamani tena ndani ya jamii," anaeleza kwa masikitiko.
Kikongwe naye akumbana na madhila
Si Nuru Togwa pekee katika kadhia hiyo, bali pia wamo wengine akiwamo kikongwe Alesi Maarifa (77) ambaye mwishoni mwa mwaka 2010, alikamatwa na walinzi wa shamba hilo, akatandikwa bakora.

Huyu anasema alikamatwa wakati akipita kandokando ya shamba hilo. Katika mazungumzo yake na mwandishi wetu, bibi huyo anakumbuka maumivu makali aliyopata akisisitiza "yalikuwa makali sana" kwa kuwa hakuwahi kupigwa kwa muda mrefu katika utu uzima wa
ke.

Kutokana na kutofahamu Kiswahili vyema,katika mazungumzo yake na mwandishi wetu bibi huyo akiwa na mkalimani maalumu anasema; "Nilipigwa na kitu kizito kichwani na kuanguka chini na kubebwa hadi kwenye kambi ya walinzi. Huko wakachukua panga lililopashwa moto kwa muda mrefu, wakanichoma kwenye mapaja, mgongoni na sehemu mbalimbali za mwili wangu.

"Hadi leo ni
meachwa na makovu ya kudumu mwilini mwangu kutokana na vidonda vilivyosababishwa na mateso hayo" anasema bibi huyo na kuongeza: "Nilishindwa kutoa taarifa katika vyombo vya dola kutokana na kutokuwa na uelewa wowote wa masuala hayo. Ilibidi nijitibu mwenyewe vidonda kwa kutumia dawa za asili hadi nikapona.

Mwandishi wetu pia alizungumza na Diwani wa Kata ambayo shamba hilo lipo, Festo Mwananjela, ambaye katika maelezo yake licha ya kukiri wananchi wake kuteswa, anasema; "Wananchi hawakushirikishwa kwenye mchakato wa kuuzwa kwa shamba hili, baada ya mwekezaji kukabidhiwa alikuta kuna mazao ya wananchi, lakini aliyaharibu bila ya kuwalipa fidia.
"Njia ambazo awali zilikuwa zikiunganisha kijiji kimoja na kingine kupitia shamba hilo zikafungwa na yeyote anayepita katika njia hiyo ya awali anakamatwa na walinzi na kisha kuteswa."
Taasisi ya Haki za Binadamu
Mkurugenzi wa Kituo cha Haki za Binadamu Mkoa wa Rukwa, Dk. John Masiya, anazungumzia suala hilo kwa kukiri kufikiwa na malalamiko ya wanakijiji hao kuhusu mgogoro huo wa ardhi.
Kwa mujibu wa Dk. Masiya, katika malalamiko yao wanakijiji hao wanadai kukatazwa kulima kwenye mashamba yao ya awali yaliyopo ndani ya shamba la DAFCO na walimwandikia barua Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga wakati huo, Meja (mstaafu) Bahati Matala.
"Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ilishauri suala hilo lishughulikiwe na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, lakini sikuwahi kupokea malalamiko kuhusu watu kupigwa, kuchomwa moto na wengine kukatwa masikio," alisema Dk. Masiya.
Kauli ya Naibu Waziri Mwanri
Serikali, kupitia kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri, hivi karibuni iliagiza uongozi wa Mkoa wa Rukwa kushughulikia kero zote zinazowahusu wananchi wa vijiji hivyo ndani ya mwezi mmoja.
Kati ya hatua zilizopendekezwa na Mwanri ni pamoja na na kupitiwa upya mkataba wa mauziano ya shamba hilo la mifugo la DAFCO ili kubaini ukiukwaji wowote wa mkataba baina ya pande mbili husika.
Mwanri akiwa ziarani mkoani Rukwa hivi karibuni alidai agizo la kupitiwa upya kwa mkataba huo linazingatia ukweli kwamba mwekezaji aliyenunua shamba hilo amebadili matumizi ya eneo hilo. Kwa mujibu wa Mwanri, badala ya kuendesha shughuli za ufugaji sasa mwekezaji huyo analima mazao mbalimbali kinyume cha mkataba.
Mwanri anasema; "Serikali haiwezi kuvumilia kuona wawekezaji ambao wamekuwa wakiidanganya. Kuna haja ya kupitiwa upya kwa mkataba huo vinginevyo kama atakuwa ameshindwa kutimiza masharti mkataba huo usitishwe mara moja".
Hata hivyo, tayari Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Stella Manyanya ameunda tume kwa ajili ya kushughulikia kero hizo baina ya wananchi wa vijiji hivyo na mwekezaji huyo, lakini ni zaidi ya miezi miwili sasa imepita huku majibu ya tume hiyo yakiendelea kusubiriwa kwa hamu na wananchi ili hatimaye kuhimitisha mgogoro huo uliodumu kwa miaka kadhaa sasa.
Msimamo wa Efatha Ministry
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mkoa wa Rukwa wa Efatha Ministry, Mchungaji Michael Meela, alimweleza mwandishi wetu kwa njia ya simu kwamba, hafahamu kuhusu watu kufanyiwa udhalimu wa aina yoyote.
Mchungaji huo anasema anachokijua yeye ni kwamba walinzi wake katika shamba hilo wamekuwa wakipigwa na wanakijiji na zaidi ya hapo, kesi za kupigwa walinzi zimekuwa zikiripotiwa Polisi. Hata hivyo, hakufafanua kuhusu idadi ya kesi ambazo zimeripotiwa.
"Suala la kero zinazodaiwa kuwapo katika vijiji vinavyolizunguka shamba hilo ni masuala ya kisiasa ambayo hayana tija yoyote kwa Efatha," alisema mchungaji huyo.
Msimamo wa polisi Rukwa
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda, amemweleza mwandishi wetu kwamba taarifa zilizoripotiwa kwake hivi karibuni zinahusu walinzi wa shamba hilo kuporwa silaha na baadhi ya wanakijiji pamoja na wizi wa ng'ombe wawili wa mwekezaji huyo. Anasema uchunguzi kuhusu matukio hayo unaendelea.
"Jambo jingine ninalofahamu ni kuibuka kwa uhasama mkubwa kati wananchi wa vijiji vinavyozunguka shamba hilo na walinzi wa DAFCO, lakini hakuna taarifa ya watu kalalamika kuhusu kupigwa wala kufanyiwa vitendo vyovyote vya kikatili na kumsababishia ulemavu wa maisha.
"Polisi wapo kwa ajili ya kusikiliza watu wote hivyo kama kuna vitendo vya baadhi ya watu kujichukulia sheria mkononi na kufanyiwa unyama wa aina yoyote ile, wajitokeze na kutoa taarifa ili vyombo vya dola viweze kushughulikia na hatimaye sheria kuchukua mkondo wake," anasema Kamanda Mwaruanda.
Mi nadhani kama mwigira, aliamuru wanavijiji wakatwe masikio, ilikuwa kwa ni njema tu, ya kuadabishana,,
Huwezi ukakatisha kwenye ardhi ya mtu bila ruhusa na ukaachiwa tu hivi hivi[emoji23]
 
Huyu jamaa mbona maraisi wakiwa waislam anaropoka sana?
 
Haya anayasema saa hii wakati anatoa mahubiri yake hapa kanisani.

Anadai ameonyeshwa serikali wamemtuma mtu aje hapa kanisani ku spy ndipo alipoanza wewe uliyetumwa ni mshenzi na mambo yako ni ya kishenzi sababu waliokutuma ni washenzi.

Haya ngoja nirudi kupata mahubiri nitarudi tena
Washenzi ndiyo, kwani Uongo? Mfano mzuri Sabaya, Makonda, Kingai, Sirro, Mahita, Jerry Muro, Ali Happiness

Washenzi na wahuni tu
 
Ukiona umeanza kuwaelewa Chadema anza matibabu ya akili haraka sana
 
Kuna ile Kampuni ya FUNGUKA SECURITY ambayo inamilikiwa na Mwingira ndiyo ilipanga njama za kuwateka Walinzi wa Kiwanda cha jirani na kuwafunga Kamba baada ya kuwatesa chini ya uongozi wa Mwingira kwa Kikao kilichofanyika Kibaha.

Neno hilo linatumika na Mwingira ijapokuwa yeye si mtu wa Kwanza kutumia Bible kufanya uchafu!!
Upo usemi anao wadanganya akina mama kuwa akifanya zinaa na mtume anapata baraka !!!
Siyo tu washenz,bali CCM wote ni majibwa Koko
 
Back
Top Bottom