Mwinyi alileta upinzani uliofutwa, Samia anaenda kuileta katiba mpya, Kwa hili inabidi niweke hisia zangu pembeni kwa wazanzibari

Mwinyi alileta upinzani uliofutwa, Samia anaenda kuileta katiba mpya, Kwa hili inabidi niweke hisia zangu pembeni kwa wazanzibari

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
1655920604621.png


Yes, mimi kiukweli ni mmoja wa watu ambae huu muungano sijawahi kuupenda hata kidogo hasa pale ninapoona uongozi wa bara tunachangiana na wazanzibar lakini huko kwao ni wao wenyewe wanajiongoza, huwa inaniuma mno.

Ila kuna kitu nimetafakari hapa juu ya mchango wa hawa wenzetu wanaposhika madaraka. Nimeona kwamba ,Mwinyi alifanya kitu ambacho huenda tungewapata arais kama wa Bara aliekolezwa na siasa za Nyerere sidhani kama kingetokea, Mwinyi aliweza kuleta vyama vya upinzani mwaka 1992, kumbuka kwamba zamani kulikuwa na vyama pinzani lakini Nyerere alifuta.

Tukija kwa huyu mama, nae ana mambo yake huwa simwelewi lakini ameweza kuwapa ahueni hata wapinzani ambao kipindi kilichopita walipata taabu mno ambayo hawakuistahili, licha ya hivyo swala la katiba mpya tunaona kuna mwanga wa matumaini wa kuwepo katiba mpya japo raisi anaenda hatua kwa hatua, ni siku za mwanzo kabisa za uongozi wake alimtembelea hata Warioba na kunamengi yanaendelea juu ya Katiba,

mfano leo hii nimemuana Shaka akizungumzia katiba na ninamnukuu "Chama cha Mapinduzi tunasisitiza umuhimu wa uwepo wa Katiba mpya kwa kuzingatia mazingira ya sasa na kuona namna bora ya kufufua, kukwamua na kukamilisha mchakato wa katiba mpya kwa masilahi mapana ya taifa na maendeleo kwa ujumla" ukiangalia kwa makini unaona kaisa behind the scenes yupo rais wetu nyuma ya hayo maneno, Hakika ni swala la timing tu inaetwa katiba mpya

Mark my words, Mkombozi ataeliokoa taifa hili atakuwa mzanzibari .

Hata saa mbovu kuna muda inaoneha muda wa kweli
 
Baada ya mchakato wa katiba mpya mama tumuapishe atuongoze miaka mitano ya mpito
 
Kuna wapuuzi husema eti Nyerere alishinikiza kuwe na vyama vingi! Wakati Nyerere huyo huyo aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kumnanga Mwinyi eti hapokei ushauri ( kwa kukataa kwake kuendeshwa) wa watu wengine zaidi ya mkewe!

Ajabu! Mzee Mwinyi hakujibu mpaka alipokuja kujibu baadhi ya hoja wakati akihutubia kuaga bunge kuelekea
 
Kuna wapuuzi husema eti Nyerere alishinikiza kuwe na vyama vingi! Wakati Nyerere huyo huyo aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kumnanga Mwinyi eti hapokei ushauri ( kwa kukataa kwake kuendeshwa) wa watu wengine zaidi ya mkewe!
Ajabu! Mzee Mwinyi hakujibu mpaka alipokuja kujibu baadhi ya hoja wakati akihutubia kuaga bunge kuelekea
Nyerer alikuwa hawezi kuridhia nchi yenye vyama vingi yule mzee, ni yeye ndie aloefuta vyama hapo mwanzo.
 
Hiyo Katiba mpya itakuja kwa malengo ya kusimika aina fulani ya utawala kwa faida ya watawala.

Unajidanganya. Hii sio kwa ajili ya watu.

The invisibles behind the scenes have their own motives for the new constitution.

Tutafahamiana tu hapo baadae.
 
Mwinyi hajaleta vyama vya upinzani kwa utashi wake.

Ulikua ni msukumo wa mabeberu.
Huo msukumo haukuwa kwa Tanzania tu
ni Afrika nzima na Libya ikiwemo, lakini mpaka Gadafi wanamuua hakukubaliana na mfumo wa vyama vingi.
My point. Msukumo tu bila utashi wa anaesukumwa ni kazi bure.
 
Mleta mada unasumbuliwa na maradhi gani? Ndie nyinyi humu kila siku munakuja na nyuzi za kulalamikia Muungano, Sasa jipu linataka kutumbuliwa mnageuka hamutaki.
 
Kuna wapuuzi husema eti Nyerere alishinikiza kuwe na vyama vingi! Wakati Nyerere huyo huyo aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kumnanga Mwinyi eti hapokei ushauri ( kwa kukataa kwake kuendeshwa) wa watu wengine zaidi ya mkewe!

Ajabu! Mzee Mwinyi hakujibu mpaka alipokuja kujibu baadhi ya hoja wakati akihutubia kuaga bunge kuelekea
Ongeza nyama mkuu

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom