Mwita Waitara: Serikali inaua wananchi wangu wa Tarime vijijini. Tume zinaundwa na hakuna majibu

Mwita Waitara: Serikali inaua wananchi wangu wa Tarime vijijini. Tume zinaundwa na hakuna majibu

Namsikiliza mbunge wa Tarime vijijini ana hoja nzito juu ya raia ambao ni wananchi wa jimbo la Tarime vijinini anatoa ushahidi wa majina na ya raia waliopigwa risasi na waliouwawa na waliojeruhiwa.

Blah blah za George Simbachawene zikataka kumziba Waitara. Spika akaomba ushahidi juu ya tuhuma hizi. Mwita Waitara kasema anaoushahidi na atauwakilisha.

Migogoro ya ardhi kati ya wananchi jimbo lake na hifadhi ya Serengeti ni mkubwa. Na askari wa Tanapa wanatuhumiwa kuua raia wa wakazi wa Tarime vijijini.

Mwita anatakiwa kuwasilisha ushahidi ifikapo siku ya Jumanne.
Nawaambia kila siku uzeni meno ya tembo mjenge uzio kwenye Vijijini vinavyopakana na hifadhi kuzuia binadamu na Wanyamapori hamsikii..
 
Askari anapossbabisha kifo chochote kisichotokana na hukumu ya Mahakama huyo kaua na kuvaa kwake crown maana yake serikali inawajibika
Kwa hiyo askari akiwa amevaa "crown" kwenu hawezi kuwa na maamuzi yake binafsi?!

Mnadhani askari ni kama robot wa serikali?
 
Anaposema serikali imeua wananchi wake ana hakika hao askari wa wanyamapori wanaofanya hivyo wametumwa na serikali?

Kwangu hii ni sawa na yule kijana wa Babati aliyeuwawa akiwa mikononi mwa polisi, au yule wa Mtwara nae aliyeuwawa akiwa mikononi mwa polisi, halafu mtu aseme serikali imewaua, anyway ngoja apeleke ushahidi wake.

Natumai ofisi ya Spika haitauficha huo ushahidi kama kawaida yao, itauleta mbele ya umma kila mtanzania ajionee.

..katika mazingira hayo serikali inatakiwa iwashtaki polisi walioua wananchi ili ieleweke kwamba matukio hayo hayana baraka za serikali.

..pia serikali iwalipe FIDIA ndugu wa marehemu waliouawa au kuumizwa na polisi wake wakatili na wazembe.
 
Namsikiliza mbunge wa Tarime vijijini ana hoja nzito juu ya raia ambao ni wananchi wa jimbo la Tarime vijinini anatoa ushahidi wa majina na ya raia waliopigwa risasi na waliouwawa na waliojeruhiwa.

Blah blah za George Simbachawene zikataka kumziba Waitara. Spika akaomba ushahidi juu ya tuhuma hizi. Mwita Waitara kasema anaoushahidi na atauwakilisha.

Migogoro ya ardhi kati ya wananchi jimbo lake na hifadhi ya Serengeti ni mkubwa. Na askari wa Tanapa wanatuhumiwa kuua raia wa wakazi wa Tarime vijijini.

Mwita anatakiwa kuwasilisha ushahidi ifikapo siku ya Jumanne.
MSALITI HUYO

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom