Wewe NIbo wacha ufezuli ,hivi unamjua Lipumba au unamsikia tu,eti wapo kwenye upinzani kwa kulisha familia zao,Lipumbwa analipwa dola ndugu kama huelewi kutokana na ile elimu aliyonayo ambayo inasemekana ni watu wachache sana hapa duniani wenye kuweza kufikia na kuwa na kipaji alicho nacho ,huu unaosema wewe si dharau bali ni uchafu ,Mengi nini Mengi nani Mengi anaishi kwa kuuza magazeti na kudanganya umma ,leo amepata ulua na kufadhiliwa na hao hao mafisadi wenzake ,leo amekuwa mtu kwa WaTz sababu anawakoromea wenzake kwa kutumia vyombo vya redio.
Mengi na hao wahindi na wengine ambao ameogopa kuwataja wote ni chungu kimoja,Mengi anatumia umasikini wa WaTanzania kuwadhalilisha kwa kuwagaia vijipesa na kutaka kuwatawala akili zao ,Mengi hana lolote zaidi ya kutaka kujionyesha msafi kwa kuwageukia wenziwe ,wote ni nzige ndani ya Tanzania , mengi amezidiwa kete ndio anageuka ili tumuone ni bora na mtetezi lakini ukweli amekoseshwa tonge ndio hasira zake,Mengi kawataja watu watano tena kutoka upande wa wenye asili ya kiasia ,hivi alishindwa nini kuwataja wenye asili ya Congo ,Mengi ametafuta ubaguzi kwa kugawa weusi na weupe .kwa ufupi anawalinda mafisadi weusi na kuwakandamiza weupe ,hili si la kuachiwa hata sekunde moja Mengi ni mbaguzi kwa kitendo hiki anatumia dau la mafisadi kutaka kuwagawa WaTanzania ambao ni watu kutoka mataifa mbalimbali,kama Mengi haelewi Tanganyika ilikuwa ni mbuga tu iliyotawaliwa na wanyama wakali na ukiitafuta historia ya wapi waTanganyika walitokea utafungua akili yako na kuondokana na tabia chafu ya ubaguzi tabia ambayo ilimuondoa Salim Ahmed mtu ambae alishika nyadhifa nyingi tena nyeti katika nchi hii ,ubaguzi ndio uliomhuzunisha na kumfadhaisha na kuwafanya waTz wote kuonekana hatuna maana ,Mengi ni adui wa Taifa hili ambae anataka kutumia rangi kutugawa na kututawala na vipesa vyake vya kuuzia magazeti sie walala hoi kwa nini asiwe kama mwenziwe muuza Icecream ambae ametulia ,Mengi baada ya kukusanya vipesa vya magazeti sasa anataka kufanya jeuri ,amewatenga watu weusi ili awavutie kwake na kuanza kuwanyanyasa na kuwatumia kutokana na umasikini wao,Mengi anataka kutumia vipesa vyake vya kuuza magazeti kuwarubuni wale aliowaacha kuwataja ili waweko upande wake ,kwa ufupi amezidi kuwagawa mafisadi ,yaani amewatenga mafisadi weupe na kuwalinda mafisadi weusi ,mengi mwoga amewataja hawa wahindi mavi kitambaani je angewataja na weusi si angekuwa ameshakamatwa na kuwekwa jela kwa kuvunja sheria ,Mengi amevunja sheria hilo halina mjadala mtajaribu kulikoroga na kulipamba lakini wahindi wameshaliona na wameshapata information za juu kabisa kuwa wakienda mahakamni basi Mengi hatoki ,endeleeni kumpa kichwa Mengi kama hakuuza makaratasi yake yote na fedha yake ikawa fedheha. Jamaa kadai shilingi tu,hivyo weka akili zenu vizuri sio mnamtomeza na yeye kujigamba na vyombo vyake vya redio shauri lake akiwasikiliza watu kama Nibo basi ajue hawamtakii mema ,hao wahindi haohao watamliza tu.
WADAU , THIS IS A BURNING ISSSUE.LETS NOT WATER IT DOWN:
-Wajanja wachache wanapo suka mtandao wa kuiba milioni 152 kwa siku kwa miaka miwili-Richmond
Rostam at el
-Wajanja wanaoopoa Bilioni 40 BOT-Kagoda
Rostam at el
-Mjumba ya thamani ya millioni500-800 yanapouzwa kwa Nssf kwa bilion 48
Manji at el
-Radar inapoongezwa bei ili wajanja wakate chao cha juu bil 40
Jeetu
-Ndege ya Rais inaponunuliwa kwa mabilioni harafu hairuki
Jeetu
Sasa mkuu ukikwazwa na hilo utaniita natafuta umaarufu?
Ni heri sasa watu wanapoongea maana wakiamua kutenda kama Anna Kilango alivyosema "patakuwa hapakaliki hapa"
-
Hawa walikuwa wanajulikana kabla hata ya Mengi kuwarusha hewani,
wanaotafuta umaarufu ni wakina Lipumba kwa kupinga ukweli unaojulikana ili mradi aonekane nae amezungumza
Vyovyote vile, lakini hii haibatilishi kwamba alio wataja ni mafisadi papa na ushahidi upo hata humu JF umeanikwa nje nje. They have to face it regardless of their race, they are thieves! We cant let them kwa kutafuta vijisababu kwamba hoo tunabaguliwa, nooo, kwani wako wahindi wangapi mbona wao hawajatajwa?
Granted, Nipashe si New York Times (ambao nao hukosea pia, lakini husahihisha) lakini hili wamezidisha.
Waliotajwa na Mengi hawakutajwa kwa sababu ya "uTanzania wao wa asili ya Asia" hasha.
Wametajwa kwa sababu ya ufisadi.Kwa hiyo kama wametokea kuwa Watanzania wenye asili ya Asia, hii haimaanishi wamekuwa mafisadi kwa sababu wao ni Watanzania wenye Asili ya Asia, tuna mafisadi wengi Watanzania weusi, na watanzania wenye asili ya Asia wengi ambao si mafisadi.
Kwa hiyo hilo andiko la Nipashe, ambalo linaweza kutafsirika kuwa "Mengi kawatolea uvivu watanzania wenye asili ya Asia" lina mislead kwa kuonyesha tatizo kuwa ni utanzania wenye asili ya Asia, badala ya kusisitiza vita dhidi ya ufisadi.
Mengi naye analeta maswali mengi kwa kutaja Watanzania wenye asili ya Asia tu, ina maana wao tu ndio mafisadi?
Nia yetu wote ni kuhakikisha mafisadi wanachukuliwa hatua, lakini walichoandika Nipashe inamaanisha watanzania wote wenye asili ya kiasia ni mafisadi papa kitu ambacho si kweli. Kitu kama hiki kingeandikwa huko kwa Obama unapopasema ingekua bonge la soo. Nipashe wamechemsha.
Mwezi uliopita kuna msamaria mwema alitoa taarifa kwa mamlaka ya chakula na madawa kuhusu uwepo wa dawa feki za malaria.
Mtu huyo alizawadiwa na serikali ikazi burn dawa hizo.
Mbona kwenye hili la Mengi kuna kigugumizi na matokeo yake mawaziri wanawatetea watuhumiwa????
Mzee wa Upako (Mch Lusekelo) jana nae alihoji, " iliyetoa taarifa za DECI alizawadiwa na Deci ikashughulikiwa, iwaje Mengi atoe taarifa halafu ashughulikiwe yeye???
Wadau hivi huyu Sofia Simba nyuma yake kuna akina nani? Binafsi siamini ni mafisadi pekee wako nyuma yake inaonekana huwa anatumwa specifically kutoa matamko yenye utata ili kutokana na haiba yake ya mtu wa hovyo hovyo basi watu makini wa-assume ni kauli yake tu sio ya serikali. Nakumbuka alivyo-comment baada ya Kitine kuongelea mambo muhimu ya nchi, leo tena anajiunga kuwatetea wafanyabiashara badala ya kuongelea matatizo mbali mbali yanayowakabili wananchi. Kauli zake hizi za ajabu ajabu nafikiri angeongea waziri makini kama Mama Sitta au Shamsa Mwangunga kila mtu angeshtuka, lakini kwa vile kaongea kilaza ndio maana watu wanapuuza! Hivi CV yake ikoje, embu wadau iwekeni hapa tumjadili!
Angekuwa member hapa JF angeshajifunza kufikiri kabla ya kusema, sidhani kama ni member!
Very diplomatic. Sophia Simba sijui ni member hapa JamiiForum asome hii? 🙂
Ni lazima Pinda amtetee Mengi. Atamtetea nani. Hana political weight Tanzania. Ni lazima ajitengenezee mkakati wa kubakia kwenye nafasi hiyo hata baada ya uchaguzi ujao. Mtaona mwaka huu na mwaka ujao kila mwenye uwezo atakayejitokeza atamtetea ili mradi naye atengeneze force kwa maandalizi ya uchaguzi ujao na kurtetea nafasi yake ya uwaziri mkuu. Vinginevyo mtamlaumu akianza tena kulia hadharani.
watu wanaodai Bw.Mengi anajipendekeza kwa Rais Jakaya Kikwete na kubainisha kwamba 'ni bora kujipendekeza kwa Rais kuliko kwa mafisadi papa.'