Mwitikio wa Serikali na Wengine juu ya Mengi kutaja mafisadi!

Mwitikio wa Serikali na Wengine juu ya Mengi kutaja mafisadi!

kwa nini serikali inawajibia mafisadi???kwani wao wenyewe hawawezi kujibu??au hawazioni mahakama?



this is the million dollar question... This is the question!

Kuna haja ya makala za uchambuzi juu ya hili swali.
 
Ndugu yangu inaonekana kuwa umekata tamaa na huenda hali hiyo imesababishwa na kukosa mikakati thabiti ya kujadili hoja mbalimbali ili zilete manufaa. SIZE]


Kwa upande mmoja upo right, na kwa upande mwingine umepotea. Labda kama unajijua vzr. Unapokubali kuacha kujadili na kuelekea kutenda lolote linaweza kutokea. Wale wote walioko somalia, DRC, Iraq na Kenya sio kwamba wewe ndo umeshindwa au wao hawajui utaratibu. Mkwawa na wale mashujaa waliopigana vita ya majimaji na hata Mwalimu walikuwa wanajua taratibu.

Wajibu wa kupamba au kuleta mabadiliko si wajibu wa mtu mmoja katika jamii, hata huyu Dkt Slaa itafika wakati kama binadamu atachoka tu. Kitu cha msingi ilikufikia mabadiliko kwanza nikujiuliza wewe mwenyewe kama uko tayarii kubadilika. !

Kuna tofauti kubwa sana kati ya Anne Kilango na Dr. Slaa, Kakobe na Mokiwa, Mwanakijiji na Manyenyere, Selous na wewe. Akichoka Dr sisi tutapambana ila kwa staili tofauti. Yeye yupo CHADEMA ni ahaha. Mapambano Slaa is very strategic, Mkjj anahamasisha tutoke kwenye kujadili tukae cheche. Mfumo unaotaka wewe utafanya kazi kule UK, Au, US nk. Naona hata kwa Mandela wanashindwa. Mfumo wa utawala bora na haki ya binadamu ni mzuri mno lakini ujinga wangu na wewe unapelekea kufanya haya na wakati huo huo unajitetea. Watu wanakula posho watengeneza sheria ambayo haina meno? what the hell are you doing? Mifumo hii ndo iliwafanya hata huko Kongo wakashindwa kuvumiliana. If they need change, they must show it immediately and output must be tangible and sensible.

Pili, jiulize are you doing the right things, either nyumbani kwako, kazini, shule nk. Endapo utakosa kujiuliza mambo kama hayo hutaweza kuwa na mikakati ya kweli ya msingi kabisa ya kuweza kuleta mabadiliko...matokeo yake utakuwa vulnerable na influences...2010 utaweza kushawishika kupiga kura kwa upande wa khanga na pilau.
Maana yangu ni kwamba tusipofanya mambo kwa kuzingatia utaratibu basi hatutaweza ku-influence changes at all, tusahau, tutakuwa wapiga kelele tu!

Ukinijua huna haja ya kuniuliza hili swali
 
Suala ni tuhuma kuifikia serikali. Njia nitakayoitumia kuifikishia serikali tuhuma za jinai, zitategemeana na uwezo nilio nao na mazingira yangu.

Kama ukipata ushahidi wa jinai yoyote unalazimika kutoa taarifa kwa Jamhuri na ni kosa ikiwa utaficha ushahidi vile vile wakati unao. Sasa mi sijajua njia zinazokatazwa kutumika kuipelekea Jamhuri taarifa.
 
Hii ni kwa Pundamilia,

Wizi ni kosa la jinai (criminal). Mwenye uwezo wa kumfikisha mwizi mahakamani na kumsomea mashtaka ni Jamhuri. Raia ukishuhudia wizi, kama anaibiwa mwenzako, au jamii au mwenyewe, huna uwezo wa kwenda kumshitaki mwizi mahakamani.

Kazi yako ni kutoa ushirikiano kwa Jamhuri (kupitia jeshi la polisi), kwa kuiambia au kutoa taarifa na kuwa tayari kutoa ushahidi mahakamni utakapoitwa kama shahidi.

Mengi ameiambia serikali, si kwa kwenda polisi. Kwa kuwa ananguvu ya vyombo vya habari ametumia nguvu hiyo kuiarifu Jamhuri kuwa kuna mwizi ameonekana ameiba na ushahidi anao.

Sasa sioni tatizo hapo ndugu pundamilia. Kuiambia polisi au kuiambia jamhuri mpaka uende mwenyewe kituo cha polisi na makaratasi? Hivi mtu huwezi kupiga simu polisi ukasema Mimi fulani niko mahali fulani nashuhudia au nimeshuhudia tukio la wizi??

Sijaona kosa la raia kusema kuwa mali ya umma imefujwa na yeye anao ushahidi!! Vyombo husika vichukue hatua na baada ya kufanya uchunguzi vije mbele na viseme ushahidi hautoshi kuwafikisha mahakamani. Halafu walituhumiwa ni juu yao kufungua kesi ya madai.

Pundamilia unaposema Mengi ilitakiwa afuate taratibu; naomba uwe wazi ni taratibu zipi hizo?


Kipimapembe,

Kama ambavyo nilimsahihisha aliyejibu swali langu hapo awali, majibu yako yame-miss 'keyword' ambalo ni neno 'malalamiko'. Sasa katika majibu yako hili neno hukuligusa na ndiyo linajenga msingi wa jibu lako. Hebu incude hilo neno 'malalamiko; halafu uone kama maelezo yako uliyoyatoa hapo kama yatakuwa the same again.
Jaribu.

Nimelirudia lile swali hapo ili kukurahisishia usirudi nyuma sana.


Tom,

Hebu tafakari kwa mfano huu hapa chini:

Umeibiwa nguo zako na baada ya siku mbili tatu unamwona jirani yako amevaa shati kama lile la kwako lililoibiwa, je unachotakiwa kufanya nini, kuita press conference na kumuita mwizi au unafikisha malalamiko yako katika vyombo vya sheria?
 
Mengi kawa out hawa watu kama mafisadi, kama mtu anataka kumtaka Mengi ushahidi ili ku substantiate maneno yake nitaelewa.

Lakini habari ya kusema Mengi kachemka bila hata ya kujua Mengi ana ammunition gani, kesho keshokutwa unaweza kuaibika ukashindwa hata kumuomba radhi.

Mengi si mahakama na hana wajibu wala mamlaka ya kupitisha hukumu, yeye anatoa maoni yake kama mtanzania huru, kama mtu anajiona kapakaziwa na Mengi mahakama ziko, anaweza kufungua mashtaka.

Yaani hao walioitwa mafisadi wenyewe hawajasema viwaziri visharukia issue? Whats wrong with this picture, some puppeteering going on here?

You know what, hawa mawaziri uchwara huwa hawafikirii wanaporopoka mbele ya kadamnasi!, Hebu kumbuka walivo mjia juu Dr. Slaa kipindi kile alipotaka peleka hoja ya mafisadi bungeni kwamba ni muongo anatafuta umaarufu and the likes, sasa kesi zilizoko mahakamani wanaweza zielezea vipi? Afu wanajifanya wamesahau, na kujiweka mbele eti wanapambana na ufisadi, eti serikali ndo inajukumu hilo, kama inalo mbona imebweteka tu haifanyi lolote? badala yake inasubili mzalendo anye jitokeza kusema uozo uliopo ndo ina muandama?

Nadhani inabidi tupate waandishi wa kuwa wanawaumbua viongozi kutoka na kauli zao wanazo kuwa wamezitoa hapo nyuma na baadae kuja kuwaumbua mbele ya safari, wakifanyiwa hivo wawili watatu pengine watajifunza na kuwa makini badala ya kuwa wanaropoka kwa kujisikia tu kwa hizo dhamna walizo beba kwa muda!
 


this is the million dollar question... This is the question!

Kuna haja ya makala za uchambuzi juu ya hili swali.



Skills4ever!

Umenigusa it seems you are a great thinker!!!! Inanibidi niache kazi ninayoifanya ambayo its equally important nichangie na wajamii forums!

Tulishasema hawa mawaziri wengi wao ni kaput they are chosen for personal needs period!! na satili ni ile ile ya Salva kwa kupitia kwa makuwadi some ministers were given mere favours! Others for simply having had intimate relationships with the presida and associates period.

Sofia Simba na Mkuchika wanachunguza nini? Wote wako kwenye payroll za mafisadi na nina ushahidi!!! Mkuchika George alipokuwa DC wa Ilala alikuwa anamtembelea Manji pale kwenye maduka ya Honda kuchukua dola pamoja na Yusuf Makamba!!! hata IGP Said Mwema then RCO wa Dar!!!If they want nitawapa picha next time around!! MSIJE TU MKAFUNGIWA watch out!!!

Mafisadi walitajwa wapo na wana msururu wa mawakili uchwara let them go to court!!! Kwa nini serikali iwasemee!! Au ndio wamewaweka mfukoni!!!

As I said Mengi might be miopioc kwa muono wake ili ufanyike ufisadi there must be players na nilisema wako waswahili kibao from the police force,Jeshi Ikulu,Usalama wa taifa, TRA, and all kinds sitawataja wote kwani ni wengi who helped the ufisadi na wanajulikana wana mimali like hell tuwahoji! Huwezi ukawatenga na PAPA au whatever you call it!!
But the bottom line is hatuna utawala its all bull shit!!

Haya tuone kama akina MASILINGI /Manji they came and went :Masha walishindwa kumchukulia Mengi hatua with a lot of pomposity and law jargons/barons akina SOFIA na Bra zao wataishia na kuuza sura tu ?
 
FP,
Sina hakika kama umejaribu kuelewa nilichomaanisha kwenye post yangu. Na pia sikuona sababu kwa nini usiniulieze (kama hukunielewa) badala ya kuamua kutoa conclusion yenye kuonesha dharau kwa maoni yangu ambayo hayakuhusu wewe na si lazima uyakubali.

Kwa kuwa tumekuwa tukisema kuwa tunahitaji siku moja hili suala lifike mahakamani, na Mengi mwenyewe alisema hivyo kwamba kama wanaona wameonewa waende mahakamani, huoni kuwa kwa maelezo hayo ya Waziri Simba jamaa wakienda mahakamni tutaipata ile fursa tuliyokuwa tunaitafuta siku nyingi? Kama huoni hiyo basi eleza jinsi unavyoona wewe na siyo kujaribu kushusha hadhi ya wenzio kwa kuwapandia mgongoni!

Ndugu Mwenzangu, sikukudharau. kama ulichukulia hivyo NISAMEHE, nilichofanya ni kushangaa.

Back to mada. Kwanini Waziri awajibie wafanyabiashara waliotuhumiwa?

kwanini wasijibu wenyewe?

Hilo tu.
 
Je Simba na Mkuchika wanazungumza kwa niaba ya nani? Serikali au waliyotajwa na Mengi? Watu wengi wamewahi kuchafuliwa na magazeti lakini hata siku moja serikali hakuwahi kutoa tamko lolote kuzipinga.
Hao waliyotajwa , kama wanaona wamekosewa, wange either kwenda mahakamani au kwenye media council (regulatory body ya media) na kutoa malalamiko yao na siyo kwenye chama tawala/ serikali.
Hatujui Simba na Mkuchika walivyotoa tamko pia walikuwa wanazungumza kwa niaba ya chama maana wote wnna wadhifa kenye chama.
Simba ni kiongozi wa wananchi, kwa nini aseme "Kama kuna mwandishi wa Niphashe, atupishe".
Hiki kitendo cha wliyotajwa kwenda kwa Simba na Mkuchika kinaonyesha jinsi wao walivyo karibu nao.
 
Kipimapembe,

Kama ambavyo nilimsahihisha aliyejibu swali langu hapo awali, majibu yako yame-miss 'keyword' ambalo ni neno 'malalamiko'. Sasa katika majibu yako hili neno hukuligusa na ndiyo linajenga msingi wa jibu lako. Hebu incude hilo neno 'malalamiko; halafu uone kama maelezo yako uliyoyatoa hapo kama yatakuwa the same again.
Jaribu.

Nimelirudia lile swali hapo ili kukurahisishia usirudi nyuma sana.


Tom,

Hebu tafakari kwa mfano huu hapa chini:

Umeibiwa nguo zako na baada ya siku mbili tatu unamwona jirani yako amevaa shati kama lile la kwako lililoibiwa, je unachotakiwa kufanya nini, kuita press conference na kumuita mwizi au unafikisha malalamiko yako katika vyombo vya sheria?


Pundamilia nami kwa upande wangu sioni kwamba Mengi kafanya kosa kubwa sana given the circumstances.
Hivi kweli unafikiri ukizingatia hawa jamaa akina rostam walivyo 'heavy weights' hili swala lingefika popote kama angeenda na makaratasi yake TAKUKURU au pale kituo cha polisi Oysterbay?
Naomba nitumie mfano huo huo uliotumia wewe:

Umeibiwa nguo zako na baada ya siku mbili tatu unamwona jirani yako amevaa shati kama lile la kwako liliobiwa, UKIMCHEKI JAMAA NI BOUNCER WA NGUVU NA MARA KADHAA POLISI WENYEWE WANAONEKANA KUMWOGOPA KWANI SI MARA YA KWANZA KUSIKIA AMEIBA WASIFANYE KITU, je utakachofanya ni kujitoa mhanga kuiambia jamii msaidiane au unafikisha malalamiko yako katika vyombo vya sheria ambavyo on countless occasions vimeonyesha incompetence ku deal na huyu heavy weight!!!??


Kumbuka kipindi flani DPP na AG walisema kabisa bungeni kuwa mtandao wa hawa mafisadi ni mkubwa na wana hela sana kiasi ambacho serikali ikienda kwa pupa wanaweza yumbisha mambo nchini. IMAGINE THEY SAID SO in PUBLIC yani hio ni njia mbadala ya kusema hatuwawezi!!
 
Last edited:
Skills4ever!

Umenigusa it seems you are a great thinker!!!! Inanibidi niache kazi ninayoifanya ambayo its equally important nichangie na wajamii forums!

Tulishasema hawa mawaziri wengi wao ni kaput they are chosen for personal needs period!! na satili ni ile ile ya Salva kwa kupitia kwa makuwadi some ministers were given mere favours! Others for simply having had intimate relationships with the presida and associates period.

Sofia Simba na Mkuchika wanachunguza nini? Wote wako kwenye payroll za mafisadi na nina ushahidi!!! Mkuchika George alipokuwa DC wa Ilala alikuwa anamtembelea Manji pale kwenye maduka ya Honda kuchukua dola pamoja na Yusuf Makamba!!! hata IGP Said Mwema then RCO wa Dar!!!If they want nitawapa picha next time around!! MSIJE TU MKAFUNGIWA watch out!!!

Mafisadi walitajwa wapo na wana msururu wa mawakili uchwara let them go to court!!! Kwa nini serikali iwasemee!! Au ndio wamewaweka mfukoni!!!

As I said Mengi might be miopioc kwa muono wake ili ufanyike ufisadi there must be players na nilisema wako waswahili kibao from the police force,Jeshi Ikulu,Usalama wa taifa, TRA, and all kinds sitawataja wote kwani ni wengi who helped the ufisadi na wanajulikana wana mimali like hell tuwahoji! Huwezi ukawatenga na PAPA au whatever you call it!!
But the bottom line is hatuna utawala its all bull shit!!

Haya tuone kama akina MASILINGI /Manji they came and went :Masha walishindwa kumchukulia Mengi hatua with a lot of pomposity and law jargons/barons akina SOFIA na Bra zao wataishia na kuuza sura tu ?


Wewe ni mmoja wa watu ninaopenda michango yao. Keep it up!!
 
Kwa nini hao akina Rostam wasijibu wenyewe kama anayosema Mengi yamewaumiza! Serikali kuingilia na kuwasemea akina Rostam inaleta maswali mengi.

By Sijala tangu juzi
 
Tom,

Hebu tafakari kwa mfano huu hapa chini:

Umeibiwa nguo zako na baada ya siku mbili tatu unamwona jirani yako amevaa shati kama lile la kwako lililoibiwa, je unachotakiwa kufanya nini, kuita press conference na kumuita mwizi au unafikisha malalamiko yako katika vyombo vya sheria?


Ndugu,

Mfano wako ni mzuri, lakini hauendani na tukio hili hata kidogo au kwa lugha nyingine mfano wako ni mfu!
Hao mafisadi hawajamwibia Mengi, wameiba raslimali za nchi ambazo watawala wetu wanajukum la kuzilinda kwa kushilikiana na wananchi, Na Mengi kama mtanzania amejitolea kutoa maoni yake ambayo anaushahidi, kwa hiyo Polisi, na waendesha mashitaka wanatakiwa wawahoji na kupeleka mashitaka Mahakamani huko ndiko mbivu na mbichi zitajulikana.
 
NILIKUWA DODOMA WAKATI WA UCHAGUZI WA UWT NA SOPHIA SIMBA ALIKUWA AKIGAWA KATI YA Sh 150,000 na 200,000 KWA WAJUMBE, JE, HUYO ANAWEZA KUPIGA VITA RUSHWAA? UNADHANI ATAWATENGA WALIOMPA FEDHA ZA KUGAWA?
 
ninapongeza kauli za serikali kwani watanzania wote tuna haki sawa na hakuna wa kumuhukumu mwengine pasi na mamlaka halali yaani mahakama. Kama mengi ana ushahidi wa madai yake na ana vielelezo kwanini hakuviwasilisha katika mamlaka husika ili anaowatuhumu wachukuliwe hatua zipasazo? Hivi leo hii kila mtu anayemtuhumu mwenzie atinge maelezo amchafue kwa nia ya aliyechafuliwa aende mahakamani? Hakuna mantiki hata kidogo, watu wote wafuate sheria na utaratibu uliopo na si kutumia nafasi maalum kupindisha mambo.

Endapo serikali ingekaa kimya maana yake ina kubaliana na uendeshaji wa nchi bila ya kuzingatia utawala bora.

Serikali haipo kwa ajili ya wanyonge tu bali hata akina mengi na rostam. Ni vema basi ni lazima ikemee yale yote mabaya ikiwa ni pamoja na kauli za uchochezi, kuchukua sheria mikononi, ufisadi nk.
Serikali yetu iko imara wakati wote na iendelee kufanya kazi kwa faida ya wananchi wote bila ya kuwaonea aibu watu wachache kama mengi wanaotaka kutimiza matakwa yao binafsi kwa mgongo wa mafisadi nk.

Tuziachie mamlaka husika zifanye kazi ya kutoa hukumu na si vinginevyo.

u must be kidding man !
 
Pundamilia nami kwa upande wangu sioni kwamba Mengi kafanya kosa kubwa sana given the circumstances.
Hivi kweli unafikiri ukizingatia hawa jamaa akina rostam walivyo 'heavy weights' hili swala lingefika popote kama angeenda na makaratasi yake TAKUKURU au pale kituo cha polisi Oysterbay?
Naomba nitumie mfano huo huo uliotumia wewe:

Umeibiwa nguo zako na baada ya siku mbili tatu unamwona jirani yako amevaa shati kama lile la kwako liliobiwa, UKIMCHEKI JAMAA NI BOUNCER WA NGUVU NA MARA KADHAA POLISI WENYEWE WANAONEKANA KUMWOGOPA KWANI SI MARA YA KWANZA KUSIKIA AMEIBA WASIFANYE KITU, je utakachofanya ni kujitoa mhanga kuiambia jamii msaidiane au unafikisha malalamiko yako katika vyombo vya sheria ambavyo on countless occasions vimeonyesha incompetence ku deal na huyu heavy weight!!!??


Kumbuka kipindi flani DPP na AG walisema kabisa bungeni kuwa mtandao wa hawa mafisadi ni mkubwa na wana hela sana kiasi ambacho serikali ikienda kwa pupa wanaweza yumbisha mambo nchini. IMAGINE THEY SAID SO in PUBLIC yani hio ni njia mbadala ya kusema hatuwawezi!!

Tanzania ni nchi inayofuata utawala wa sheria. Hisia za kuwaona akina Rostam, Manji, Mengi nk kuwa ni heavy weights mbele ya sheria ni potofu.

Tuchambue mambo kwa kina na yakinifu. Hata kama tunaona Mengi amefanya jambo la kutupendeza, lakini je amelifanya sawasawa? Je, kama amekosea tusiseme kuwa amekosea? Hapa ndipo ninapotofautiana na wale wanaona kuwa amefanya sawasawa. Mimi ninasema kuwa mengi ana ushahidi juu ya matendo maovu kwanini aendelee kuukalia? anafaidika nini?

Mfano wako ulioutoa wa Bouncer labda nitaogopa ku-deal naye kama nipo Somalia, nchi ambayo haina serikali. Lakini kwa Tanzania kwangu hakuna heavy weight wala bouncer. Hao unaowafikiria wewe kwamba ni wazito inategemea na unyonge wa hisia zako. sifikirii kumuhofia mtu kwa vile ninaheshimu demokrasia na utawala wa sheria.
 
NILIKUWA DODOMA WAKATI WA UCHAGUZI WA UWT NA SOPHIA SIMBA ALIKUWA AKIGAWA KATI YA Sh 150,000 na 200,000 KWA WAJUMBE, JE, HUYO ANAWEZA KUPIGA VITA RUSHWAA? UNADHANI ATAWATENGA WALIOMPA FEDHA ZA KUGAWA?

Je una ushahidi juu hilo unalolisema?
 
Ndugu,

Mfano wako ni mzuri, lakini hauendani na tukio hili hata kidogo au kwa lugha nyingine mfano wako ni mfu!
Hao mafisadi hawajamwibia Mengi, wameiba raslimali za nchi ambazo watawala wetu wanajukum la kuzilinda kwa kushilikiana na wananchi, Na Mengi kama mtanzania amejitolea kutoa maoni yake ambayo anaushahidi, kwa hiyo Polisi, na waendesha mashitaka wanatakiwa wawahoji na kupeleka mashitaka Mahakamani huko ndiko mbivu na mbichi zitajulikana.

Walau ungejaribu kujibu hilo swali labda ningelijua uwezo wako ni wa kiasi gani na nikusaidiaje. Lakini kwa vile umejibu nje ya swali basi ninaamini hilo ni jibu la swali tofauti na nililoliuliza.
 
Kipimapembe,

Kama ambavyo nilimsahihisha aliyejibu swali langu hapo awali, majibu yako yame-miss 'keyword' ambalo ni neno 'malalamiko'. Sasa katika majibu yako hili neno hukuligusa na ndiyo linajenga msingi wa jibu lako. Hebu incude hilo neno 'malalamiko; halafu uone kama maelezo yako uliyoyatoa hapo kama yatakuwa the same again.
Jaribu.

Nimelirudia lile swali hapo ili kukurahisishia usirudi nyuma sana.


Tom,

Hebu tafakari kwa mfano huu hapa chini:

Umeibiwa nguo zako na baada ya siku mbili tatu unamwona jirani yako amevaa shati kama lile la kwako lililoibiwa, je unachotakiwa kufanya nini, kuita press conference na kumuita mwizi au unafikisha malalamiko yako katika vyombo vya sheria?

Pundamilia,

Nimesema kwanza swali lako halishabihiani hasa na suala linalojadiliwa. Hata hivyo kwa muktadha wa swali lako jibu lako ni hivi. Malalamiko yako utayafikisha kwenye vyombo vya sheria kwa njia utakayoona inafaa. Suala hapa ni njia utakayotumia kuvifikia vyombo vya sheria. Njia yoyote itakayopeleka taarifa kwa vyombo vya sheria itafaa.

Lakini vilevile njia utakayotumia itategemeana na ukubwa wa kosa au jinai yenyewe. Kwa mtu aliyezungushia ukuta kwenye mtaa mzima na kutangaza kuwa ni eneo lake na huruhusiwi kutoka humo ndani ya ukuta na ukaona majirani zako hawajui kinachoendelea, kupiga kelele ili majirani wote wajue na polisi walio kituo cha jirani wajue inaweza kuwa njia sahihi. au?
 
Mengi aliuliza hawa watu kiburi chao kinatoka wapi? Sasa tumepata jibu kutoka kwa mhusika mwenyewe na wenzake -- Sophia
 
Pundamilia,

Nimesema kwanza swali lako halishabihiani hasa na suala linalojadiliwa. Hata hivyo kwa muktadha wa swali lako jibu lako ni hivi. Malalamiko yako utayafikisha kwenye vyombo vya sheria kwa njia utakayoona inafaa. Suala hapa ni njia utakayotumia kuvifikia vyombo vya sheria. Njia yoyote itakayopeleka taarifa kwa vyombo vya sheria itafaa.

Lakini vilevile njia utakayotumia itategemeana na ukubwa wa kosa au jinai yenyewe. Kwa mtu aliyezungushia ukuta kwenye mtaa mzima na kutangaza kuwa ni eneo lake na huruhusiwi kutoka humo ndani ya ukuta na ukaona majirani zako hawajui kinachoendelea, kupiga kelele ili majirani wote wajue na polisi walio kituo cha jirani wajue inaweza kuwa njia sahihi. au?

Kipimapembe,
Nimekusoma, lakini unaposema ukubwa wa kosa au jinai una maanisha nini sijakuelewa kwani ninajua mimi katika sheria hakuna double standards na ndiyo maana wanasema sheria ni msumeno.
Pia kwa faida ya kuelimishana ni hivi, unapokuwa na malalamiko dhidi ya mtu mwingine kwa mfano unahisi fulani ndiyo kakuibia nguo zako, basi unapeleka malalamiko hayo katika vyombo husika yaani Polisi ili uchunguzi/upelelezi uweze kufanyika na hatua nyingine ziwezekuchukuliwa.
Vinginevyo unaweza kumuagiza Attorney/Advocate awasilishe madai yako dhidi ya mtuhumiwa wako. Hizi ndiyo njia ambazo Mengi alitakiwa kuzifuata kama mwananchi mwingine yeyote. ikumbukwe kuwa hata sisi wa Vingunguti tunaposimama na Mengi mbele ya sheria hakuna tofauti, sheria inakuwa kama msumeno inakata kotekote.
Kuendelea kumtetea kwa kitendo alichokifanya ni saswasawa na kuendelea kubariki maovu yaendelee. Kazi kubwa ya JF ni kurekebisha makosa na wala siyo kupamba watu. Pesa za Rostam au Mengi ni kwa ajili ya matumbo yao na hazisaidii kuweka standards za JF kama vile wachache wanavyofikiria. Tuendelee kumkoma nyani mchana kweupe.
 
Back
Top Bottom