Hii ni kwa Pundamilia,
Wizi ni kosa la jinai (criminal). Mwenye uwezo wa kumfikisha mwizi mahakamani na kumsomea mashtaka ni Jamhuri. Raia ukishuhudia wizi, kama anaibiwa mwenzako, au jamii au mwenyewe, huna uwezo wa kwenda kumshitaki mwizi mahakamani.
Kazi yako ni kutoa ushirikiano kwa Jamhuri (kupitia jeshi la polisi), kwa kuiambia au kutoa taarifa na kuwa tayari kutoa ushahidi mahakamni utakapoitwa kama shahidi.
Mengi ameiambia serikali, si kwa kwenda polisi. Kwa kuwa ananguvu ya vyombo vya habari ametumia nguvu hiyo kuiarifu Jamhuri kuwa kuna mwizi ameonekana ameiba na ushahidi anao.
Sasa sioni tatizo hapo ndugu pundamilia. Kuiambia polisi au kuiambia jamhuri mpaka uende mwenyewe kituo cha polisi na makaratasi? Hivi mtu huwezi kupiga simu polisi ukasema Mimi fulani niko mahali fulani nashuhudia au nimeshuhudia tukio la wizi??
Sijaona kosa la raia kusema kuwa mali ya umma imefujwa na yeye anao ushahidi!! Vyombo husika vichukue hatua na baada ya kufanya uchunguzi vije mbele na viseme ushahidi hautoshi kuwafikisha mahakamani. Halafu walituhumiwa ni juu yao kufungua kesi ya madai.
Pundamilia unaposema Mengi ilitakiwa afuate taratibu; naomba uwe wazi ni taratibu zipi hizo?