Mengi kawa out hawa watu kama mafisadi, kama mtu anataka kumtaka Mengi ushahidi ili ku substantiate maneno yake nitaelewa.
Lakini habari ya kusema Mengi kachemka bila hata ya kujua Mengi ana ammunition gani, kesho keshokutwa unaweza kuaibika ukashindwa hata kumuomba radhi.
Mengi si mahakama na hana wajibu wala mamlaka ya kupitisha hukumu, yeye anatoa maoni yake kama mtanzania huru, kama mtu anajiona kapakaziwa na Mengi mahakama ziko, anaweza kufungua mashtaka.
Yaani hao walioitwa mafisadi wenyewe hawajasema viwaziri visharukia issue? Whats wrong with this picture, some puppeteering going on here?