Mwl. Nyerere alianzisha miradi mingi kuliko hii tunayoisika: . Alikosa " Whistle blowers" kwa sababu ya mfumo wa chama kimoja, ikafa yote. Tujifunze

Mwl. Nyerere alianzisha miradi mingi kuliko hii tunayoisika: . Alikosa " Whistle blowers" kwa sababu ya mfumo wa chama kimoja, ikafa yote. Tujifunze

Kididimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2016
Posts
4,153
Reaction score
3,800
Ni maoni yangu:
Kwa kuwasikiliza viongozi wetu wa juu wa chama, kuna dalili ya kurudi mfumo wa utawala wa chama kimoja.
.Sina takwimu ni Watanzania wangapi wangependa iwe hivyo,japo hakuna aliyejitokeza waziwazi ndani ya chama Tawala kusemea hii trend.

Athari mojawapo kubwa ni kuwa na utawala wenye kusikiliza upande mmoja wa shilingi kama ilivyokuwa katika utawala wa Mwl. Nyerere. Maana yake tutakuwa na proposers tu wa mbinu za kukuza uchumi, huduma za jamii nk .

Hii kwa hali ya Ufisadi na ujanja wa viongozi wetu,huenda tukajikuta kwenye hali ileile hasa mwishoni mwa enzi za Mwl. Nyerere. Tulijenga Viwanda vingi, vikahujumiwa na walewale wenye chama huku wakiwaficha wananchi.

Na ndiyo maana Mwl. Nyerere miaka ya 90, akashupalia mfumo wa vyama vingi. Kimsingi hakutaka upinzani uongoze nchi,bali uwepo kuikosoa serikali kwa yale mabaya.

Na kwa njia hiyo, wananchi wangechambua na kupata ukweli. Pia ungefanya viongozi waliopo madarakani kuwa makini zaidi.

Kwa hali ilivyo sasa na uzoefu wa Uchaguzi wa Serikali za mitaa wa Nov. 2019, kuna uwezekano huu:

1. Vyama vya upinzani vikasusia, uchaguzi Mkuu 2020 kikabaki chama kimoja.
2. Maana yake tutakuwa na uchaguzi au uteuzi wa upande mmoja, bunge la chama kimoja nk.
3. Tutaanza kuoneana aibu kiutendaji. Yawezekana ukali uliopo sasa ukatoweka kwa vile hakuna mshindani.
4. Huo utakuwa mwanzo wa kurudi tulikotoka.
 
Na hii ya mwalimu kupigania upinzani uchwara huku akitaka CCM iendelee kutawala milele ni tatizo kubwa.
Asingefanya hivyo inawezekana tusingekuwa na hii Tanzania kama unavyoiona. Watu wanachukulia amani yetu kama ni haki yao. Hawamini kuwa hapa watu wanaweza kuanzisha hata uasi nchi ikasambaratika.

Ccm wamebweteka sana na kukinai ilhali nchi ina mafukara mamilioni waliokata tamaa. Hawa ni wabaya kuliko wale Walibya waliokuwa wameshiba
 
Theory yako siyo Correct; miradi ya Nyerere "iliyokufa"-kwa maana yako ingawa mingi ilibadilishwa ownership tu, ni ile ya kibiashara kama vile viwanda na mashirka ya umma, lakini miradi yote ya infrastructure mingi ndiyo tumekuwa tunategemea mpaka leo.

Umeme wa Bwawa la Nyumba ya Mungu, Umeme wa Kidatu na Umeme wa Mtera ni mradi ya Nyerere na wala hatujawahi kuwa na mradi mwingine wa Hydropower kuazia hapo, wala siamaini kweli kuwa miradi hiyoimekufa. Uwanja wa ndege KIA na uwanja wa ndege DAR Terminal 2 ni miradi ya Nyerere ambayo imekuwapo hadi leo hadi mwaka jana tu ndipo tumeparta terminal 3 ambayo almanusra ingekuwa ni mali ya wachina. Reli ya Tazara bado ipo hadi leo ingawaje soko lake limekuwa siyo imara kama mwanzo kutokana na Ukombozi wa Afrika ya Kusini. Miradi ya barabara ndiyo inayozorota ingawa ilidumu sana- mfano Barabara za Dar kama Pugu Road (Nyerere), Port Access Road (Mandela), Morogoro Road, Bagamoyo Road( Mwinyi), na zile za mikoani kama Dar-Arusha, Dar-Tunduma, Morogoro-Dodoma, Mwanza-Sirari zote zilijengwa wakati huo, na huwezi kusema kuwa miradi hiyo ilikufa ilhari ilifanya kazi kwa takriban miaka 30. Baadaye zilizorota kutokana na kukosa maintanance kwa vile waswahili hatukuwa na utamaduni na wala hata neno la maana ya "maintanance" wakati huo hadi mwishoni mwa miaka ya tisini ndipo tukabuni maneno ya "Ukarabati" na "Ukarafati"
 
Mwalimu alikosea sana hii nchi. Sijui kwanini hawatokei viongozi wa kumkosoa
Haya ndiyo mawazo mgando kabisa ya "it is always someone's fault". Nyerere aliondoka madarakani miaka 35 iliyopita, muda ambao ni mrefu kuliko alioutumia yeye mwenyewe kuwapo madarakani, zaidi ya ule tuliotawaliwa na wajerumani, karibu sana na ule tuliotawaliwa na waingereza. Alitawala nchi wakati dunia haina internet, dunia ikiwa katika vita baridi, Afrika ikiwa inagubikwa na ukoloni. Tangu ameondoka madarakani je tuliobaki tumefanya nini?

Wakati Nyerere anaondoka madarakani, China ilikuwa ni nchi maskini sana, Rwanda ilikuwa kwenye vita za wenyewe kwa wenyewe walikiwa wanachinjana hovyo hovyo, Irelanda walikuwa ni vita ya wenyewe kwa wenyewe lakini leo nchi hizo zimebadilika, kwa nini sisi hatutaki kujibadilisha lakini kila mara tunakimbilia kumlaumu Nyerere?

Kama Nyerere ndiye mbaya wetu leo, kwa nini tusiwalaumu akina Mangungo ambao basically ndio waliogawa nchi kwa Wajerumani.
 
Miradi ya Mwalimu Nyerere ilikufa / ilianza kufa wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere mwenyewe, sababu kubwa ilikuwa ni corruption na mismanagement, mfumo mzima ulikuwa ni kuhudumia politburo na familia zao tu, nani asiyekumbuka magari ya mashirika kupeleka watoto shule, concubine saluni, watoto wanasomeshwa Ulaya na mashirika ya umma, Nyumba za mashirika ya umma wanaweka ndugu zao n.k., ....
 
Back
Top Bottom