semenya Binafsi nimeshukuru na kufurahi na changamoto yako, lakini naomba kukuliza wewe mwenyewe ungekuwa kwenye kamati ya kuscreen watu wa kuwapa Nobel Prize ungeweza kumteteaje mwalimu JKN kuwa apewe na anastahili hiyo award/prize? Maana katika bandiko lako unasema kafanya mengi kwa bara la Africa mengi yepi? Nobel Prze zilianzishwa na mtu ambaye alilaani vita JKN alipigana vita na Uganda, vita ambayo hata hapa JF tumequestion mantiki yake. Sababu alizosema tulikuwa nazo za kwenda uganda leo hii wengi wetu hatuzioni?? wangapi walikufa Uganda? kwa kufa kiasi hicho cha watu tayari anakuwa disquliafied kupata NOBEL.
Ukiangalia hotuba zake, tafuta hata You tube zipo utaioona hotuba moja anayosema kuwa aliombwa apatanishwe na Idd Amin lakini kwa maneno yake mwenyewe anasema aliwauliza watu wanaosema kuwa aache kumpiga Idd Amini kuwa walikuwa wapi??? Sasa Mkuu Nobel Prize haaziendi kwa Jicho kwa jicho, zinaenda kwa ukipigwa shavu la kushoto geuza la kulia.
Desmond Tutu siku moja alipokuwa anatembea mtaanzai aliona Mob wanamtandika kijana alienda akamwangukia juu akamfunika watu wakaanza kumpa kibano yeye mpaka alipookolewa na dola. Nelson Mandela alipoteza uraia wake kwa kuchoma Passport, kuna watu wameadnika Historia kubwa sana kama akina Steve Biko, Chris Hann, Bob Moses lakini bado hawajatambuliwa.
JKN alihamisha watu kutoka kwenye vijiji vyao kwa nguvu, watu wengi walipigwa na migambo, walichomewa nyumba zao, walipoteza mifugo, waliliwa na simba, acha waliokufa kwa maralia, Taifodi, vipindupindu kwenye maeneo waliyowekwa yasioyofaa kwa maisha ya Binadamu.
JKN alitaifisha mali za watu kwa azimio lake la arusha (hii ni sawa na anachofanya comrade Mugabe-Jongwe)
Pitia vigezo vya Nobel alafu toa mchanganuo cha alichofanya JKN kuweza kutunukiwa hiyo Prize. Ni Mtazamo Tu